Akilihuru
JF-Expert Member
- May 20, 2022
- 1,444
- 2,833
- Thread starter
- #201
Kinachowamaliza wakongomani ni mambo matatu hapo chini:Hii ni fedheha kwa nchi kubwa kwa idadi ya watu, raslimali na eneo kama DRC kudharauliwa na ka nchi kadogo!
1) Kwanza hawana umoja kama taifa, mkongo wa kinshasa hajishughulishi na yanayoendelea Goma na wa Goma hana muda na yanayoendelea Lubumbashi. Wanaoongea lingala wanajiona ndio wakongo original huku wakiwaita wenzao wanaoongea kiswahili kuwa ni watanzania au warundi. Wanaoongea kiswahili nao wanawaona wale wa lingala kama washamba fulan japo wamezaliwa capital centre lkn wanashindwa ujanja na maarifa na wale waliozaliwa katika miji mingine kama vile Lubumbashi, Katanga nk. Ndio maana unaona maelfu ya watu wanakufa huko kivu katika mapigano wakati huo huo Fally Pupa yupo zake kinshasa anatumbuiza, hajui, hajali au kuguswa na kile kinachoendelea huko mashariki mwa nchi yao.
2) Pili wakongo wamebezi sana kwenye mambo ya starehe kama vile ulevi, kwenda club kukata rhumba kiliwanzenza nk. So linapokuja swala la kuwataka kupigana wanakuwa hawana option nalo ni ile tu sometimes wanajikuta wanalazimishwa tu kupigana ili kuokoa maisha yao, familia zao nk.
3) Tatu serikali imewekeza sana katika mambo mengine yasiokuwa na maana huku ikiacha yale ya msingi kama vile ya ulinzi kujiendea tu kiholela kwa kuamini kuwa yanayoendelea huko kivu hayawezi kuwafikia wao walio katika serikali kuu huko kinshasa.
Kwahiyo tusitegemee kuona maajabu yoyote kutoka kwenye jeshi la Congo pale watakapoingia vitani na Rwanda, sanasana utakuta askari wa Congo akivua magwanda kutupa silaha na kujichanganya na raia kukimbilia Tanzania au Burundi kuomba hifadhi ya kikimbizi.