Ugonjwa wa Korona uliibuka ktk serikali ya awamu ya tano na katika jitihada za kupambana nao , ikajengeka imani kuwa ni ugonjwa uliotengezwa katika maabara kwa dhumuni maalum hususani katika nchi za Afrika. Baada ya muda katika kupambana na ugonjwa huo nchi mbalimbali zikajitangaza kupatikana kwa dawa na chanjo ya ugonjwa huo , lakini aliekuwa mkuu wa nchi kwa wakati huo aliwaaminisha wananchi kuwa hizi chanjo sio salama kabisa kwa maisha ya binadamu na kwasababu ilikuwa kauli ya mkuu wa nchi basi ikaiingia vizuri sana katika akili za watanzania.
Mbaya zaidi taasisi za dini pamoja na taasisi za afya nazo zikakubaliana kwa asilimia 100 kuwa chanjo sio salama kabisa hivyo wananchi watumie dawa za kienyeji na sio chanjo . Hivi sasa mkuu wa nchi yupo katika kampeni juu ya kuwapatia wananchi wake chanjo japo kwa hiyari lakini changamoto kubwa iliyopo ni je; watanzania wapo tayari kwa kiasi kupokea chanjo hiyo? tukumbuke tu kuwa lengo la WHO ni kuwapatia chanjo wananchi wote , je Rais Samia na wananchi watatimiza lengo hilo ili misaada iendelee kumiminika nchini?
Changamoto nyingine ni chanjo gani ndio bora? Je, chanjo kutoka Uchina, Urusi, USA, UK, Canada ambayo itatumiwa na WHO na Je, Watanzania wanaamini chanjo kutoka nchi gani?
Hivi karibuni Waziri mkuu wa Uingereza aliugua ugonjwa wa Korona na mpaka sasa yupo Karantini japokuwa alipata chanjo mara mbili.
USHAURI KWA WIZARA YA AFYA
Wizara ya Afya ifanye kampeni kubwa ( massive kampeni) usiku na mchana ili kuondoa fikra hasi zilizozagaa katika mawazo ya watu.
Kazi iendeleee.
Mbaya zaidi taasisi za dini pamoja na taasisi za afya nazo zikakubaliana kwa asilimia 100 kuwa chanjo sio salama kabisa hivyo wananchi watumie dawa za kienyeji na sio chanjo . Hivi sasa mkuu wa nchi yupo katika kampeni juu ya kuwapatia wananchi wake chanjo japo kwa hiyari lakini changamoto kubwa iliyopo ni je; watanzania wapo tayari kwa kiasi kupokea chanjo hiyo? tukumbuke tu kuwa lengo la WHO ni kuwapatia chanjo wananchi wote , je Rais Samia na wananchi watatimiza lengo hilo ili misaada iendelee kumiminika nchini?
Changamoto nyingine ni chanjo gani ndio bora? Je, chanjo kutoka Uchina, Urusi, USA, UK, Canada ambayo itatumiwa na WHO na Je, Watanzania wanaamini chanjo kutoka nchi gani?
Hivi karibuni Waziri mkuu wa Uingereza aliugua ugonjwa wa Korona na mpaka sasa yupo Karantini japokuwa alipata chanjo mara mbili.
USHAURI KWA WIZARA YA AFYA
Wizara ya Afya ifanye kampeni kubwa ( massive kampeni) usiku na mchana ili kuondoa fikra hasi zilizozagaa katika mawazo ya watu.
Kazi iendeleee.