- Source #1
- View Source #1
Wakuu nimekutana na hizi taarifa je kuna ukweli wowote huko?
- Tunachokijua
- Vyama mbalimbali vya Siasa nchini Tanzania vipo katika mchakato wa kampeni kuelekea uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba 29, 2025. Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Rais Samia Suluhu Hassan alikuwa mkoa wa Pwani (Kibaha na Chalinze)
Madai
Kupitia mitandao ya kijamii ikiwemo Instagram, Septemba 29 zilisambaa grafiki zikiwa na utambulisho wa Clouds TV zikiwa zimebeba jumbe mbalimbali kumuhusu Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Rais Samia Suluhu Hassan. Miongoni mwa ahadi hizo ni;
- Kuwapa Bandari ya Bagamoyo DP World
- Kuwapa Waarabu shirika la TANESCO ili kuongeza ufanisi
- Hata wananchi wasipopiga kura CCM itashinda
JamiiCheck imefuatilia na kujiridhisha kuwa Taarifa hiyo Si ya kweli.
Kupitia mikutano ya kampeni ambayo Rais Samia aliifanya katika mkoa wa Pwani Septemba 28, 2025 hakuzungumza maneno hayo.
Akiwa Kibaha na Chalinze Rais Samia alinadi ilani ya chama chao na kueleza mambo watakayoyafanya katika mkoa huo ikiwa watapata nafasi. Miongonj mwa mambo waliyoya ahidu ni kuboresha miundombinu ikiwemo bandari.
Kuhusu umeme alisema kuwa wataweka vituo vya kupoza umeme Msufini, Mkuranga pamoja na Segereni Kibaha na Zinga, Kibaha.
Aidha grafiki zilizotumika kusambaza grafiki hizo ni za kughushi na hazijachapishwa na Clouds TV kama inavyoonekana. Hata hivyo ujumbe unaooenakana kutoka katika ukurasa wa X na kudaiwa kuwa umechapishwa na mgombea huyo ni wa kughushi na haujachapishwa katika ukurasa wake rasmi wa X.