Rais Samia, kwani wanaume tumekufanya nini?

Rais Samia, kwani wanaume tumekufanya nini?

Mpwayungu Village

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2021
Posts
14,575
Reaction score
31,013
Nimekuwa nikifuatilia hotuba za Rais Samia, yaani muda mwingi anatumia kumpamba mwanamke na kutunyooshea vidole wanaume. Hii hali anayokuja nayo Rais siyo salama maana huko mbele itapelekea watanzania wasiwe na imani naye tena. Huwenda si yeye tu hata wanawake kwa ujumla atakuwa amewatia doa.

Mnataka wanawake mpendwe vipi? Tayari Mama Samia ni rais anataka nini tena? Yaani imefika hatua anateua viongozi wengi wanawake kutukomoa wanaume, badala ya kuteua viongozi kulingana na weledi, sifa na utashi. Siyo kuangalia jinsia kama unavyofanya.

Ninavyo muona huyu Rais Samia yaani anatamani hata leo Spika awe mwanamke, Jaji Mkuu awe mwanamke, Mkuu wa Majeshi awe mwanamke. Uteuzi wa hovyo wa Waziri wa Ulinzi pamoja na Mabalozi mbalimbali umeyathibitisha haya.

Achilia mbali majukumu aliyonayo mwanaume ndani ya familia, hebu tuangalie yafuatayo halafu tuone wanawake tunawanyanyasa kama Afghanistan au tumewapa vipaumbele vya kutosha?

1. Nafasi za viti maalumu haziwahusu kabisa wanaume ni wanawake tuu, tena ni nyingi kiasi cha kukaribiana na viti vya majimbo. Yote haya Rais Samia hataki kuridhika, hivi wanawake mpendwe vipi?

2. Wizara nyeti nyingi zimekaliwa na wanawake. Mbali na kuwa Taifa la Marekani ni kongwe kidemokrasia lakini sijawahi kusikia mwanamke akaiongoza pentagon. Ila hapa tuna Waziri wa Ulinzi mwanamke na hakuna aliyehamaki.

3. Wanawake hupewa vipaumbele kuliko wanaume kwenye selection za shule, vyuo pamoja na ajira. Bila pingamizi inawezekana kabisa mwanaume akawa na daraja la kwanza lakini akaachwa akachukuliwa mwanamke mwenye daraja la Tatu. Hapa sasa tunafuata gender equity au?

4. Rais Samia nakuomba zingatia katiba na ilani ya Chama Cha Mapinduzi ambacho japo ni kichefuchefu mbele ya watanzania. Maana hakuna mtanzania anataka katiba hii wala CCM lakini, tunaomba ufuate ajenda zenye vipaumbele kwa taifa kuliko kujinadi ukike wako kila siku jambo ambalo halina tija kwa wananchi.

NB: Haya ni maoni tu maana nina haki kikatiba ya kumkosoa kiongozi yeyote na siku zote unapokosolewa ndiyo unakuwa imara.
Asante
 
Wananchi wanataka katiba mpya sio malumbano
Screenshot_20210928-153207.jpg
 
Alafu ijumaa anakwenda kuswali huyu.

Wakati msaafu unaeleza kwa kina nafasi yake kama mwanamke na nafasi ya mwanamme.

Bimkubwa analalamika sana na anasahau aliyetoa uwezo, mamlaka na jinsia ipi iongoze ni mwenyezi Mungu, hizi anazoleta ni hisia za kushindwa pia ni ishara ile spirit of self-exaltation inamwangukia na kumuonyesha yeye ni nani from early creation!.
 
Mama yuko sawa.

wacha aweke uwiano, nchii itajengwa na watanzania wote kwa pamoja.

nimefurahishwa sana na teuzi zake.

Katika Marais wote waliowahi kupita Rais Samia ndiye Rais Pekee anaye zingatia sana uwiano ktk Idara zote za Serikali.

maaana kwekweli kulikuwa na tatizo kubwa sana la kukosekana kwa uwiano hata hivyo bado tatizo lipo kwani haliwezi kumalizwa mara moja kwani lilijengwa kwa miongo mingi sana!!.

Viongozi wengine ktk Serikali wenye mamlaka za uteuzi ni vyema wakazingatia au kufuata nyayo za Mhe. Rais ktk teuzi mbalimbali wazo zifanya wasiegemee wala kujaza watu wa aina fulani wakati wengine wakiachwa nje hili halifai, tuzingatie uwiano kwa maana zote ili kujenga uzalendo kwa Taifa, sio kujaza watu wa aina moja tu ktk idara kama vile wengine hawafai au hawana uwezo!! hilo halina afya kwa mustakbali wa nchi.

azidi kujitahidi kurekebisha makosa haya ambayo kimsingi yaliathiri sana umoja na mshikamano wa nchi yetu.

uwiano kwa maaana zote ni muhimu sana ktk kuimarisha uzalendo wa nchi.

watanzania wote wenye sifa wanahaki sawa ya kuitumikia nchi yao.

Viva Rais Samia ViVA.
 
Mama yuko sawa.
wacha aweke uwiano, nchii itajengwa na watanzania wote kwa pamoja.
nimefurahishwa sana na teuzi zake.
Katika Marais wote waliowahi kupita Rais Samia ndiye Rais Pekee anaye zingatia sana uwiano ktk Idara zote za Serikali.
maaana kwekweli kulikuwa na tatizo kubwa sana la kukosekana kwa uwiano hata hivyo bado tatizo lipo kwani haliwezi kumalizwa mara moja kwani lilijengwa kwa miongo mingi sana!!.
Viongozi wengine ktk Serikali wenye mamlaka za uteuzi ni vyema wakazingatia au kufuata nyayo za Mhe. Rais ktk teuzi mbalimbali wazo zifanya wasiegemee wala kujaza watu wa aina fulani wakati wengine wakiachwa nje hili halifai, tuzingatie uwiano kwa maana zote ili kujenga uzalendo kwa Taifa, sio kujaza watu wa aina moja tu ktk idara kama vile wengine hawafai au hawana uwezo!! hilo halina afya kwa mustakbali wa nchi.
azidi kujitahidi kurekebisha makosa haya ambayo kimsingi yaliathiri sana umoja na mshikamano wa nchi yetu.
uwiano kwa maaana zote ni muhimu sana ktk kuimarisha uzalendo wa nchi.
watanzania wote wenye sifa wanahaki sawa ya kuitumikia nchi yao.
Viva Rais Samia ViVA.
Kumbe aangalie uwiano sio sifa
 
Hao ndio wapiga kura waaminifu.... we kacheze bao
 
Kumbe aangalie uwiano sio sifa
Tanzania itajengwa na watanzania wote bila kujali jinsia zao kabila wala dini.
wenye sifa wapo wengi sana ktk nchi hii yenye watu zaidi ya milioni 60.
Tatizo lilopo sasa ni UWIANO kuna aina moja ya watu imejazana sana ktk nafasi za serikali kuliko aina nyingine ya watu na wanazo sifa!!
takwimu zipo, jaribu kufanya utafiti kidogo tu ktk idara za serikali utabaini.
kinachotakiwa ni uwiano kwa maana zote kwa wale wenye sifa.
viongozi wasijifanye vipofu, wenye mamlaka za uteuzi wanajua hilo ila wakati mwengine wanafanya kwa mazoea bila kutafakari athari za mbeleni.
Pamoja na kuzingatia sifa lkn pia ni muhimu sana kuzingatia UWIANO ili kuimarisha umoja na uzalendo kwa Taifa letu.
 
Ni wakati wao huu mkuu; kuwa na subira na uvumilivu; wanawake ni mama zetu na dada zetu pia. Wacha wajinafasi maana sisi wanaume si tumefaidi mema ya nchi kwa miaka 60 sasa. Au hutaki dada yako pale nyumbani ainuliwe???
 
Back
Top Bottom