Rais Samia kuziba masikio?

Rais Samia kuziba masikio?

Kama mtakumbuka hata Rais wa Awamu ya Tano alishupaza shingo na kuziba masikio kwenye mambo mengi waliyoyalalamikia wananchi. Alikuwa hashauriki, inshu ya Makinikia aliziba masikio na hakusikiliza ushauri wa mtu yeyote.

Mbaya zaidi alivuka mipaka na kuwadhuru, kuwapiga, kuwafungulia kesi za uongo, kuwatisha, na kuwaua wote waliokosoa. Mfano mzuri ni Tundu Lissu aliyemiminiwa risasi nyingi kwa kukosoa suala la Makinikia, lakini yote kwa yote aliishia kwenye aibu kubwa sana.

Ninaona Rais Samia anaelekea njia hiyo hiyo ya mtangulizi wake. Kwenye hili suala la Bandari za Tanganyika watu wameanza kutishwa, wengine wamefunguliwa kesi kwa mgongo wa nyuma, wengine wanaitwa kuhojiwa, Rais amekataa kusikiliza maoni ya wananchi, wengine wanaoanzisha maandamano ya amani wanakamatwa, na tunaweza kushuhudia watu wanauwawa.

Watanzania tuliombee taifa letu na tumuombe Mungu kwa ajili ya bandari zetu wanazopewa bure hawa wajomba wa Dubai.

Raisi Samia ameshupaza shingo na kuziba masikio.

Tanzania n zanzibar zatlina saizi mkataba wa madini
 
ACHA undumilakuwili wewe,kama haufanyi makusudi Tena kwa visent vya kuhongwa kuutetea huu ujinga unao itwa mkataba wa bandari basi akili zako ni afadhali za kuku
Aliyehongwa ni yule wakili Mwabukusi anayetumia nguvu kubwa kuwakashifu mawaziri ili eti wakasirike na kufanya maamuzi ya jazba!, mpuuzi kweli kweli huyo wakili.

Anatazamwa tu kama mjinga fulani hivi.
 
20230725_075921.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waarabu wa DP world ndio waliokuambia wanakuja kununua korosho?
Connections za biashara naongelea, ukiwa ni mtu wa karibu na kinachofanyika pale bandarini huwezi kuuliza maswali ya kitoto namna hii.

Na hili ni tatizo letu kitaifa, wanaoponda uwekezaji pale TPA hawana biashara yoyote na masuala mazima ya bandari.
 
Connections za biashara naongelea, ukiwa ni mtu wa karibu na kinachofanyika pale bandarini huwezi kuuliza maswali ya kitoto namna hii.

Na hili ni tatizo letu kitaifa, wanaoponda uwekezaji pale TPA hawana biashara yoyote na masuala mazima ya bandari.
Mkataba unasema uwekezaji kwenye bandari wewe unazungumzia korosho
 
Wanasiasa ni wanafiki wanatafuta millage tu Hila swala la bandari limeingiliwa na wanasiasa watafuta umaarufu na kasababisha kuonekana Lina chembechembe za udini na ubaguzi
Na wanaoleta udini ndio waligawa bandari zetu Bure kabisa
 
Wewe utakuwa una chuki binafsi na Magufuli, Magu alikuwa anaibuka kwenye mambo mengi yanayogusa nchi mfano issue ya sukari kupanda bei uliona kabisa serikali yake inapambana na kuwachukualia hatua wafanya biashara wote wanaoficha sukari kwenye magodown , issue ya corona uliona, korosho, mambo mengi ya kifisadi yeye ndio alikuwa anaibua tofauti na awamu za nyuma wapinzani ndio walikuwa wanaibua mambo mengi alikuwa lazima ayatolee ufafanuzi na alikuwa anatabia kila anapoenda mikoani hawezi kuondoka bila kutatua changamoto zao sambamba na kutumbua majibu.

Raisi wa sasa ndio ambaye hawezi kumkukuta anazungumzia masuala yanayogusa nchi na ni kwasababu uwezo wake mdogo kukabiliana na mambo yanagusa maslahi ya nchi
Yote aliyogusa ndio aliharibu zaidi.
Sukari aliharibu
Korosho aliharibu
MAKANIKIA aliharibu nk
 
Back
Top Bottom