Rais Samia kabambikiwa sakata la Mwanza?

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,007
JE NI KWELI KAAGIZWA? NI LAZIMA ASEME?

Sakata la CHADEMA na Polisi huko Mwanza lina harufu ya hujuma zifuatazo:

1. Je ni kweli Mh. Rais kaagiza kongamano lizuiwe?

2. Kama kaagiza kwa nini amuagize RPC badala ya IGP?

3. Je ni kweli RPC kasema hadharani kuwa kaagizwa na Rais au kachomekewa maneno na waandishi?

4. Kama ni kweli RPC amesema kuwa katumwa na Rais, kulikuwa na ulazima wa yeye kusema hivyo hadharani? Uwajibikaji wa pamoja uko wapi?

NIONAVYO MIMI:

Uhuru ni kitu pekee kinachotakiwa kulindwa kwa gharama zozote. Kwa hiyo:

1. Wanaokusanyika kupinga katiba mpya wawe huru kama wanaokusanyika kuunga mkono.

2. Vyombo vya ulinzi vilinde katiba visilinde watu, vyama, wala Viongozi.

3. Kuzuia watu kukusanyika ni kuandaa watu kutokusanyika watakapotakiwa kukusanyika. Matumizi ya nguvu ni tabia ya tawala zisizokubalika (Illegitimate). Utawala wetu unakubalika kwa hiyo ujitenge na matumizi ya nguvu.

4. Zipo dalili pevu za njama na hujuma za kufarakanisha utawala huu na wananchi katika sekta nyingi: uchumi, siasa, usalama, na Haki za Binadamu. Adui wa kwanza wa utawala huu si wapinzani, si awamu iliyopita, NI serikali yenyewe inayoelekea kufarakana na kujianika.
Mama asirithi marafiki wala maadui. Atengeneze marafiki na maadui wake.

Lisemwalo LINAWEZA kuwapo. Ondoa miwani utaliona.

Askofu Bagonza
 
Ndio ulazima wa yeye kusema hadharan ni kukwepa kulaumiwa ndio maana kasema mapema kua ni Maagizo kutoka juu.
 
Amri IPO kuna kila dalili.

Isipokuwa RPC hakupaswa kusema Rais kaamuru.

Rais ni Amiri Jeshi Mkuu.

Polisi wanaweza tumia nguvu kubwa kwakuwa RPC ameamriwa na Amiri.

RPC angetisha tu kwa njia zingine.

Hapo sasa uadui mkubwa wawananchi waliokuwa kwenye kongamano ni Rais
Mama amefeli sana ! masaa 48 tu kishafeli kwenye miamala na demokrasia , au kalogwa ?
 
Ulikuwa wapi alipokuwa anaambiwa hadharani kwamba anavunja katiba? Una mwendawazimu na kauli zake unazisikia hadharani loud and clear, uulize ili iweje tena wakati alichokisema umekisikia!?

Hivi alivokuepo yule ,mlikua mnajiuliza amri inatoka wapi?au mlishahukumu,,, hii double standard ndo unafiki wenyewe
 
Tutampelekesha mbio tu Tanzania ni yetu sote hana hati miliki. Haya mazingira ya kidikteta yanaweza kabisa kutuletea dikteta nyang’au mwingine.

Inasemekana mama kaamua liwalo na liwe kwa vile hana mpango wa kugombea 2025 , hana shida na kura zenu , kwanza hamkuwahi kumchagua kapata kindondokela tu
 
Nchi huwezi kuiendesha kama unavyolea mtoto..

Wafrika wengi hatujitambui ukimpa uhuru atakushika hadi matakoni hiyo haitoshi atakupaka na mafuta kabisa huku akikutolea maneno ya kebehi, hao ndio wafrika.

Hatujui tunachokihitaji kama taifa, hata hiyo katiba wakipewa bado haitowafaa watanzania wengi.

Katiba na tabia za asili za watanzania ni vitu viwili tofauti kabisa. Hizi ni tabia za mtu mfano wizi, rushwa, tamaa na uchu wa madaraka, kiburi, kutojali muda n.k hapo hata kama unakatiba nzuri bado kutakuwa na matatizo mengi kwenye mfumo wa uongozi na kwa wananchi.

Matatizo yetu kama vile:-
Mfumo wa elimu mbovu
Viongozi hawana miiko ya maadili ya uongozi
Kufanya kazi kwa mazoea
Ubinafsi kupitia udini na ukabila
teknolojia duni
Ujinga
Umasikini wa kifkra( hili ni janga kwa taifa)
Maradhi.
Siasa mbovu.

Ushauri wangu
× Bado tuna katiba nzuri japo sio bora sana ya kusifia, tatizo lipo kwa tabia za watu ambao hawafit kwenye hii katiba, hivyo basi tubadili tabia na mienendo yetu kwa viongozi na wanachi kwa pamoja.
 
Ulikuwa wapi alipokuwa anaambiwa hadharani kwamba anavunja katiba? Una mwendawazimu na kauli zake unazisikia hadharani loud and clear, uulize ili iweje tena wakati alichokisema umekisikia!?
Mtu kasema amri imetoka wapi, nyie mnakuja mnasema labda karogwa au mara mnahoji mode of delivery ya hiyo amri,huoni hyo ni double standard!kwahiyo watu wengine mnawa-take at their own words kama mwendazake hawa wengine mnaona Wanatania,,come on mkuu 🤣🤣,
 
Back
Top Bottom