PreGE2025 Rais Samia: Hatutamvumilia kiongozi wa dini anayechochea chuki na uhasama dhidi ya Serikali, mkawadhibiti!

PreGE2025 Rais Samia: Hatutamvumilia kiongozi wa dini anayechochea chuki na uhasama dhidi ya Serikali, mkawadhibiti!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Akizungumza kwenye Baraza la Eid El-Fitri kumbi wa JNICC Dar es salaam, leo tarehe 31 Machi, 2025, Rais Samia amesema nchi yetu (Tanzania) imeendelea kuwa na Umoja na Mshikamano kwasababu viongozi wa dini wamejiepusha na mahubiri yenye uchochezi na kuleta mafarakano.

Aidha ameongeza kuwa Serikali hatosita kuwachukulia hatua kali baadhi ya Viongozi wa dini walio na mwelekeo wa kuhubiri na kupandikiza chuki na uhasama dhidi ya Serikali.

"Tushikilie msimamo wa imani, udhibiti wa nafsi zetu na wajibu wetu katika kuikuza na kuitunza amani yetu nchini. Niwaombe katika madhehebu na makundi yenu mbalimbali muweze kuwadhibiti wale wachache miongoni mwenu walio na mwelekeo wa kuhubiri na kupandikiza chuki kwa wananchi dhidi ya Serikali yao. Waache kufanya hivyo. Ni vyema sote tujue kuwa katika mifarakano na hasama hakuna atakayeibuka mshindi, bali kutatokea hasara na majanga,"

 
Viongozi wa dini watawathibiti vipi wakati inajulikana wao hawana serikali serikali anayo yeye mwenyewe sa100?
 
Wewe umeshindwa kuwashughulikia watesi wetu waliomuua mzee kibao

Kusema kifo ni kifo unafikiri ukuhatarisha usalama wa wananchi wa Tanzania?

Vipi kauli yako kwa familia ya kibao unaona ilikuwa sawa?

Ondoa boriti kwenye jicho lako ndio uulize kibanzi ndani ya jicho la mwenzio

Samia ni Rais useless toka tupate Uhuru wa nchi hii
 
Akizungumza kwenye Baraza la Eid El-Fitri kumbi wa JNICC Dar es salaam, leo tarehe 31 Machi, 2025, Rais Samia amesema nchi yetu (Tanzania) imeendelea kuwa na Umoja na Mshikamano kwasababu viongozi wa dini wamejiepusha na mahubiri yenye uchochezi na kuleta mafarakano.

Aidha ameongeza kuwa Serikali hatosita kuwachukulia hatua kali baadhi ya Viongozi wa dini walio na mwelekeo wa kuhubiri na kupandikiza chuki na uhasama dhidi ya Serikali.

Mwamakula
 
No reforms no elections


Yaan tuna Rais wa Hovyo kabisaaa kabisaaa



Yeye na serekali wawe wannatenda haki, haki hawatendi unataka nini??!
Namshangaa!
Anataka viongozi wa dini wote wamsifie tu kama wale wajinga waliosoma dua eti ya kumlinda sa100 na mabaya...ndicho anachotaka tu hicho!!.
 
Hata magufuli alisema hivyo hivyo Ile 2020 lakini yaliyotokea Kila mtu anajua.

Kumuamini mwanasiasa tena wa ccm ni kazi sana.

Juzi tu 2024 wameiba uchaguzi wa serikali za mitaa na kuwaengua wapinzani halafu Leo anatoa hizo kauli .. inatia hasira sana...

Mwaka 2024 uchaguzi wa serikali za mitaa umesimamiwa na makada wa ccm ngazi za kata.

Sehemu zingine walizosimamia walimu wasio makada wakatishwa wasipitishe mpinzani....

Sehemu zilizokuwa na upinzani kama BADI, MALAMPAKA wilayani Maswa mkoani Simiyu wakaambiwa wachukue fedha waachie ngazi au wapewe kesii...

HAWA NDIO CCM NI HATARI MNO ....

Leo unadai uchaguzi utakuwa wa huru na haki hilo haliwezekani KAMWE CCM mmeshajitengenezea kansa ya wizi wa uchaguzi..

Aliyekuwa Mkuu wa wilaya Maswa kafanya hujuma kubwa uchaguzi wa serikali za mitaa 2024 lakini umeamua hujuma ile aipeleke na Bunda kwenye upinzani mkali baada ya hapo umpeleke Mbeya Kwa sugu.. ..Leo unadai uchaguzi utakuwa wa huru na haki!!?

CCM wananchi tunajua Kila kitu kinachoendelea.
 
Akizungumza kwenye Baraza la Eid El-Fitri kumbi wa JNICC Dar es salaam, leo tarehe 31 Machi, 2025, Rais Samia amesema nchi yetu (Tanzania) imeendelea kuwa na Umoja na Mshikamano kwasababu viongozi wa dini wamejiepusha na mahubiri yenye uchochezi na kuleta mafarakano.

Aidha ameongeza kuwa Serikali hatosita kuwachukulia hatua kali baadhi ya Viongozi wa dini walio na mwelekeo wa kuhubiri na kupandikiza chuki na uhasama dhidi ya Serikali.

Kuna dalili ya "nyundo" inakuja.
 
Akizungumza kwenye Baraza la Eid El-Fitri kumbi wa JNICC Dar es salaam, leo tarehe 31 Machi, 2025, Rais Samia amesema nchi yetu (Tanzania) imeendelea kuwa na Umoja na Mshikamano kwasababu viongozi wa dini wamejiepusha na mahubiri yenye uchochezi na kuleta mafarakano.

Aidha ameongeza kuwa Serikali hatosita kuwachukulia hatua kali baadhi ya Viongozi wa dini walio na mwelekeo wa kuhubiri na kupandikiza chuki na uhasama dhidi ya Serikali.



..aanze na Mufti Zubeir anayepiga kampeni za waziwazi kushabikia Ccm, na kuichonganisha serikali na wananchi.
 
Viongozi wa dini nchini wametakiwa kutumia nyumba za ibada (Misikiti na Makanisa) kuendelea kuwakumbusha na kuwaelimisha waumini umuhimu wa kumtumikia Mwenyezi Mungu kama wanavyofanya mara zote, sambamba na kuhubiri umuhimu wa kutunza amani katika nchi.

Rai hiyo imetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati akihutubia Baraza la Eid El-fitr kitaifa, hafla iliyofanyika jioni ya leo, Jumatatu Machi 31.2025 ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam ambapo katika maelezo yake ameweka wazi kuwa serikali haitovumilia viongozi wa dini wanaotumia nyumba za ibada kusambaza chuki dhidi ya serikali sambamba na kuhubiri uvunjifu wa amani kwenye nchi.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Sambamba na hilo, Rais Samia pia ametoa wito kwa viongozi wa dini kutoruhusu kutumika kisiasa badala yake wajikite kwenye majukumu yao ya kila siku.
 
Back
Top Bottom