Rais Samia hatagombea Urais Uchaguzi mkuu 2025

Rais Samia hatagombea Urais Uchaguzi mkuu 2025

Shocker

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2012
Posts
2,175
Reaction score
4,180
Mnahitaji kulijua hilo, kilichotokea WaZanzibari wanakiita ngekewa, baada ya kufariki mpendwa wao Rais Magufuli, budi haikuwepo ni lazima Mh. Samia Suluhu akamate sukani na kulivusha Taifa hili la Tanzania, hakutegemea ila alijua akifa anarithi Urais hadi hapo 2025 kama atakuwa hai, utakapofanywa Uchaguzi Mkuu.

Kuna hawa WaTanzakikikoko ambao tumewaona bungeni wakianza kupiga chapuo na kusema ni yeye hadi 2030,nawambia waTanzakikikoko hao, wasijipitishe kwa Samia wala wasijipendekeze,kwanza waelewe Samia hawafanani na Magufuli hata kidogo labda kwa kadi za chama nazo namba pia tofauti.

Siku atakuja kukuliza au kukuulizeni mbele ya watu aka mkutano. Je, aliwatuma au aliwambia mseme au mumsemee hayo kuwa ataendelea kugombea hadi 2030? Na ninavyomjua hakawii

Nyinyi mnaomtangazia hayo ndio mnaomjengea maadui ndani na nje ya Chama na ndio mnaokigawa Chama katika kambi au timu,sasa wewe au nyinyi ndio Timu Samia ndani ya CCM.

Hii nafasi ipo wazi kwa mwanachama yeyote wa CCM hasa wa upande huo wa T/Bara, lakini sio kuanza uchuro, Samia mpaka 2530 ndivyo alivyokwambia? Unaacha mambo muhimu ndani ya bunge na kujipanga kwa hoja kuwatetea wananchi na hela inayodaiwa imepotea unaenda kuwaletea watu habari za miaka mitano inayokuja, na yote haya kwa sababu wabunge wengi humo hawakushinda walipitishwa kimagumashi na Tume ya Uchaguzi ya Magufuli, mna tamaa kupiga kigoma ili huyu Rais Samia aanze kukicheza ili mkatize kama mlivyokatiza.
 
Kwani huyu hatumuongezi muda wa kuongoza!
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Wewe unamsemea SSH ukiwa kama nani? Wewe unayajua yaliyomo moyoni mwake?
Mimi kama mwanafamilia aka Waarabu wa Pemba.

Sasa nyie wasaka tonge mnaanza kujipitisha kwa kauli mbiu eti mpaka 2030, WaTanzakikikoko ,mnatamaa ya huruma ya Uchaguzi, nani asie jua kuanzia diwani mpaka Marehemu nyote mliondoka na kura za wizi na sio kura maana uchaguzi uliopita upigaji kura haukuwa na faida yeyote si ya mtu kushinda wala kushindwa.

Huyu Samia miyamiya hagombei tena si kwa kuwa hawezi kugombe hataki,anawaachia machogo yenyewe yatoane roho ndani ya CCM, Kwani lile onyo hukulisikia aliposema wale wenye kuutaka Urais hapo 2025 waache,hakumaanisha yeye atagombea ,alimaanisha jambo lingine kabisa.
 
Mkuu kuwa na stamala kidogo, Msimamo ni ule ule Mitano(5) tena na Kazi iendeleee.
 
Mmeanza ramli chonganishi wachawi nyie!
 
Wewe ni mwanafamilia wa SSH?
Unaweza kututhibitishia hilo?
Si nimeshakuelekeza kuwa msimpake na kumvika kilemba cha ukoka,tumewaona pale bungeni mishipa ya shingo imewatoka eti Mheshimiwa Raisi Samia ataendelea hadi 2030, ufupi nimeshawamegea kuwa hilo halipo kwake Samia anamalizia urithi ,awaachie wenyewe zigo lenu.
 
Kwani nani asiyejua mama anachapa kazi, na kuna muda itabidi apumzike.

Hii nchi inawasomi wengi bwana pia tunao watu wengi wenye shauku ya kuchapa kazi
"Upuuzi mtupu"
 
Mwingulu Nchemba, ameanza kampeni za kuutaka urais 2025. Na haifai.
 
Ndugu sio ramli chonganishi kuna watu wanataka kumfanya na yeye aonekane kama yule Marehemu .manguvu,magube,ubabe amri za papo kwa papo,kama haitoshi wanataka kumgeuza daraja, ili huko tuendako likizama wamtwishe yeye ,unaona sasa hivi kila kitu wanamshakizia yeye, atavaa viatu,atafuata nyayo na sasa wanamtwisha mzigo eti ataendelea mpaka 2030 ,na uhajkika ni timu zimeanza kupambana sasa ile wameweka mtego kuona itakavyochukuliwa.

Endeleeni na timu zenu na chaguweni mnaowaona watafaa kupeperusha bendera ya CCM kila timu mkutane kwenye uchaguzi mkuu kumpitisha ila kwa Samia sie kwake hii mitatu iliyobakia anaiona mingi sana.
 
Mimi kama mwanafamilia aka Waarabu wa Pemba.
Sasa nyie wasaka tonge mnaanza kujipitisha kwa kauli mbiu eti mpaka 2030 ,WaTanzakikikoko ,mnatamaa ya huruma ya Uchaguzi, nani asie jua kuanzia diwani mpaka Marehemu nyote mliondoka na kura za wizi na sio kura maana uchaguzi uliopita upigaji kura haukuwa na faida yeyote si ya mtu kushinda wala kushindwa.

Huyu Samia miyamiya hagombei tena si kwa kuwa hawezi kugombe hataki,anawaachia machogo yenyewe yatoane roho ndani ya CCM, Kwani lile onyo hukulisikia aliposema wale wenye kuutaka Uraisi hapo 2025 waache,hakumaanisha yeye atagombea ,alimaanisha jambo lingine kabisa.
Unajifariji,,Samia kugombea ni must kenge ww, sukuma gang
 
Mwingulu nchemba, ameanza kampeni za kuutaka urais 2025. Na haifai.
Naona umedukuwa,anapima upepo hata zile style akitoa ile neno akisita sita ili kusikiliza meza kama zitagongwa,na sio tegemeo ziligongwa chache sana. Kama anataka yeye ajitose tu na aanze kampeni sasa kwani Ndani ya CCM kunaonekana jivu kubwa lenye joto kali na moshi unafukuta,ila Samia atawaacha kwenye mataa na kuwatupia zigo lao wenyewe kwake si mitano tena bali ni mitatuimetosha.
 
Back
Top Bottom