Rais Samia Suluhu Hassan ataongoza hafla ya uzinduzi wa majengo ya Mahakama ya Tanzania leo Aprili 5, 2025, katika Mtaa wa Tambukareli, jijini Dodoma.
Majengo hayo ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuboresha miundombinu ya utoaji haki, kwa lengo la kuongeza ufanisi na kuimarisha upatikanaji wa huduma za kimahakama kwa wananchi.
Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi wa juu wa serikali, Mahakama na wadau mbalimbali wa sekta ya sheria.
Miradi hiyo ni pamoja jengo la makao makuu ya Tume ya Utumishi wa Mahakama, ambalo lipo mkabala na jengo la makao makuu ya Mahakama ya Tanzania.
Mradi wa pili utakaozinduliwa ni makazi za majaji ambayo yapo karibu na Chuo Kikuu cha Dodoma na mradi wa tatu ni jengo la makao makuu ya Mahakama ya Tanzania lenye jumla ya ghorofa tisa na ambalo helikopta inaweza kutua juu yake.
Fuatilia matangazo ya moja kwa moja hapa
Majaji wa Mahakama ya Rufani walivyowasili katika eneo la Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania panapofanyika hafla ya uzinduzi rasmi wa majengo ya Mahakama.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu Willium Lukuvi akisalimiana na baadhi ya viongozi waliowasili katika Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania panapofanyika Halfa ya Uzinduzi wa Majengo ya Mahakama ya Tanzania.
Rais Samia alivyopanda mti na kukata utepe uzinduzi wa majengo ya Mahakama ya Tanzania.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule; "Jengo jipya la Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania si tu kwa ajili ya huduma za kimahakama, bali ni urithi wa kipekee unaoleta hadhi, fursa za kiuchumi, na kuvutia wageni kutoka ndani na nje ya nchi."
"Muundo huo wa kipekee umebeba maono, heshima, na urembo unaoitangaza Tanzania kimataifa."
"Tunamshukuru Rais kwa kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania kupitia muundo huu wa kipekee wa Mahakama. Ni fahari kwa Dodoma, ni fahari kwa nchi."
Rais Samia Suluhu akizindua Jengo la Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania, Dodoma
"Jengo la Makao Makuu ya Mahakama ni la sita kwa ukubwa kati ya majengo ya Makao Makuu ya Mahakama duniani. Tanzania tuko pazuri sana na tuna haki ya kutembea kifua mbele, na ni la kwanza barani Afrika."
"Serikali imefanya makusudi kujenga mazingira mazuri kwa majaji wetu. Lakini mazingira haya yaendane na huduma bora zinazotolewa ndani ya majengo haya."
"Jengo jipya la Mahakama Kuu litafanya kazi na kutoa huduma bila kutumia karatasi, hatua inayolenga kuboresha utoaji wa haki kwa kutumia teknolojia za kisasa. Jengo hilo jipya litatumika kuendesha shughuli za kimahakama kwa mfumo wa kidijitali, hatua itakayosaidia kuongeza ufanisi na uwazi katika shughuli za utoaji haki."
"Tumearifiwa kuwa mahakama hii tunayoizindua leo inakwenda kutoa huduma bila karatasi, yaani paperless, ni mambo ya mtandao na teknolojia ndiyo yatatawala humu ndani,"