Rais Samia ashauriwe kuvunja Bunge kwa sababu hii

Samiaagain2025

JF-Expert Member
Dec 2, 2020
2,926
3,054
Kuna kila sababu ya mheshimiwa rais wa JMT ashauriwe avunje bunge kwa maslahi mapana ya Taifa.

Kuna sababu kuntu mojawapo ni hizi:

1. Wabunge, ambao ni wawakilishi wa wananchi wanadai mishahara yao iongezwe ili hali wakijua uchumi wa nchi ni tete:
  • Deni la taifa liko juu
  • Miradi ya nchi ni mikubwa fedha hamna
  • Vijana wanalia mitaani hawana ajira
  • Wakulima hawana ruzuku za kilimo ili wazalishe kwa tija
  • Watoto wanakaa chini baadhi ya shule na pia mazingira ya shule zetu si rafiki
Bora bunge livunjwe au itokee namna yoyote ili tusiwe na wabunge wachumia tumbo kama hawa.

NB: Hili ni bunge au halmashauri ya chama?
 
What's in it for her?

Kwenye dunia ya looking after Numero Uno, such a thing as you are proposing is impossible.
 
Wabunge wenyewe wameingia kwa hisani za mwendazake, wangekuwa wamechaguliwa kwenye uchaguzi halali mbona pasingekalika hapa.
 
Mimi naona auchune tu, kwani Kuna aliyelazimishwa kugombea ubunge? Zipo kazi nyingi za kufanya.
 
Back
Top Bottom