Rais Samia apokea ujumbe kutoka Burundi

MoureenAbel

Member
Sep 24, 2021
29
43
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, leo tarehe 14 Januari, 2022 amepokea Ujumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Évariste Ndayishimiye uliowasilishwa kwake na Mjumbe Maalum ambaye ni Waziri wa Masuala ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Vijana, Michezo na Utamaduni wa Burundi Mhe. Ezechiel Nibigira, Ikulu, Chamwino Mkoani Dodoma.

Mhe. Nibigira amemshukuru Mhe. Rais Samia kwa kukubali kupokea Ujumbe huo Maalum na kufikisha salamu kutoka kwa Mhe. Rais Ndayishimiye na kumjulisha kuwa hali ya Burundi ni salama na tulivu, hivyo kupelekea wananchi wake kuendelea na shuguli mbalimbali za kujiletea maendeleo.

Amesema Mhe. Rais Ndayishimiye amemtuma kufikisha ujumbe huo wenye lengo la kukuza zaidi uhusiano kati ya Tanzania na Burundi katika masuala ya kiuchumi.
 
Rais fisadi Kupokea ujumbe kutoka Burundi wakati anahamasisha ufisadi kwenye serikali yake tena kupitia TV ya Taifa, haiwezi kuleta maendeleo katika nchi🐒🐒🐒
 
Why always Burundi.
Mimi ningefurahi sana tungekua na ukaribu na Rwanda maana Kuna mengi ya kujifunza toka Rwanda. Lkn Burundi kila siku vita
 
Nadhani Burundi watakua na Jambo Lao flani maana juzi huyo Waziri aliyekuja kumuona bi. Mkubwa alikua Rwanda akipeleka ujumbe kutoka kwa Rais wa Burundi.Ni ajabu maana hizo nchi haziivi kabisa.
 
Burundi amekuwa mshirika mwaminifu kuliko nchi yeyote ile toka tujipatie uhuru
Wema tuliowatendea wametulipa mara mia mbili
Ni Burundi pekee anayetumia bandari ya dar kwa 99%
Wanaohoji urafiki wetu na Burundi itakuwa ni watu wa vijiweni wasuojua kitu
 
Why always Burundi.
Mimi ningefurahi sana tungekua na ukaribu na Rwanda maana Kuna mengi ya kujifunza toka Rwanda. Lkn Burundi kila siku vita
Rwanda labda tujifunze udikteta tu, tumewazidi kila kitu.
 
Tanzania tumerudi nyuma sana kidiplomasia. Kungekuwa na wa kumshauri mama aitishe mkutano Dodoma au Arusha wa kuwapatanisha Rwanda, Burundi na Uganda. Ashirikishwe rais Felix wa DRC (AU) na rais Kenyatta au Cyril Ramaphosa na Antonio Guterres (Katibu UN). Hiyo ingetupa a lot of kudos na kuturudisha katika ulingo wa Diplomasia ya Afrika. Mkutano kama huo ukifanikisha mapatano, Tanzania itaonekana kituo cha mapatanisho na hata mizozo mingine: Ethiopia/Tigray, Egypt/Ethiopia etc. ikaletwa kutatuliwa kwetu. Lakini kwanza yabidi tuonekane ni watu wa busara. Kuendelea na kesi za kijinga za Mbowe nk hakutupi sifa hiyo kabisa!
 
Umeshaambiwa urais ni taasisi kama humpwndi raia basi penda nchi yako Tanzania acha chuki za waziqazi unaonekana unamattizo ya akili tu hapo
Kati ya mimi na yeye anaehamasisha ufisadi ni nani mwenye matatizo ya akili?Urais kuwa taasisi inaondoa ukweli kuwa Samia amehamasisha serikali yake iwe ya kifisadi?

Urais kuwa taasisi inaondoa athari za Samia kuhamasisha ufisadi katika serikali yake?Mimi kukemea kitendo cha Samia kuhamasisha ufisadi katika serikali yake ni chuki?

Mimi kuipenda nchi yangu inaondoa vipi athari za Samia kuhamasisha ufisadi?
 
Back
Top Bottom