Dr Adam Francis
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 464
- 687
Siamini katika kuvunja katiba, vyovyote iwavyo ningependa uchaguzi ufanyike mwaka huu, kukiwa na ushiriki wa vyama vyote na CHADEMA kikiwepo.
Kama sauti yangu ingekuwa inasikika ningemshauri Rais, serikali iachane na kuisakama CHADEMA, binafsi naona matumizi ya mkono wa dola dhidi ya CHADEMA na viongozi wake vinamharibia kuliko kumjenga rais.
Mafanikio na kazi ilizofanywa na CCM hususani kwenye miundombinu, elimu na afya ni dhahiri, anayepinga na hilo ana lake jambo.
Tuliomaliza shule za msingi miaka ya 2000, hatujasahau mabadiliko makubwa yaliyoletwa na shule zilizobezwa kwa kupachikwa jina la shule za kata. Kabla ya shule za sekondali za kata, nakumbuka kutoka katika shule zetu za msingi walikuwa wanachaguliwa watoto wawili au watatu kujiunga na kidato cha kwanza, waliobaki walikuwa wakiingia mtaani. Nani anayebisha kuwa leo hii tuna madaktari, wahandisi, wachumi, wahasibu n.k walilelewa na hizi zilizoitwa shule za kata?
Namshukuru Mungu nimepata bahati ya kuizunguka nchi hii, kabla na baada ya miundombinu ya barabara hii tuliyonayo sasa. Huko tulikotoka, safari ya kibaha Dar, ungeweza kulala njiani, mm nikiwa moja wa mashuhuda mwaka 2007, nilipoenda Dar kwa mara ya kwanza. Sitasahau tuliingia kibaha saa moja na nusu tukafika ubungo saa saba usiku, huku mwenyeji wangu akiwa anaishi Gongo la mboto.
Ndugu zangu safari ya Mbeya Arusha ililazimu uzunguke kupitia Chalinze na Segera kwasababu hakukuwa na barabara ya Iringa-Mtera-Dodoma, pia Dodoma-Kondoa-Babati-Arusha ilikuawa Vumbi.
Tusisahau Dar to Mwanza tulikuwa tunazungukia Kenya kupitia Namanga na Silari kwasababu hakukuwa na barabara. Ni mwaka wa 2012 tu hapo, safari yangu kwa bus toka Moshi kwenda Kigali kupitia Tinde, Kahama, Bukombe, Lunzewe, Lusomo nilipita kwenye vumbi sehemu kubwa ya safari yangu wakati leo ni lami tupu.
Watu wa Lindi na Mtwara watakumbuka hali ilivyokuwa kabla ya daraja la Rufiji. In fact mikoa hii ilikuwa inafikika kwa njia mbili, meli na ndege. Ilifikafika wakati Lindi na Ntwara ilikuwa ni mikoa ya adhabu kwa watumishi wanye issue za kinizamu.
Katika sehemu zilizokuwa nyuma nchi hii ni mikoa ya magharibi, Katavi na Kigoma. Nakumbuka 2017 naenda kuripoti kazini hospitali ya manispaa ya Mpanda kutoka Dar nilitembea juu ya mkeka mpya wa rami toka Dar kupitia Sumbawanga mpaka naingia Mpanda sikuona Vumbi. Leo hii sio tu kupitia Mpanda, hali hii utaiona hata ukipitia Tabora.
Waulize wakazi wa Kigoma daraja la Maragalasi lipo hatua gani? Sikuhizi wanaotoka kigoma kuja Dar hawatambuliwi tena kwa kufika wamechafuka vumbi jekundu. Yote hii ni kazi ya CCM.
Yapo mambo binafsi naweza nisikubaliane nayo, mathalani namna upinzani unavyoshughulikiwa, lakini lknapokuja swala la maendeleo niliyoyashuhudia kwa macho yangu, siko tayari kuusaliti utashi wangu, CCM imefanya vizuri.
Kama tukimpima Raiis Samia kwa kazi zake, sote tutakubaliana, tunakila sababu ya kumuchagua tena amalizie kazi aliyoianza.
Kama sauti yangu ingekuwa inasikika ningemshauri Rais, serikali iachane na kuisakama CHADEMA, binafsi naona matumizi ya mkono wa dola dhidi ya CHADEMA na viongozi wake vinamharibia kuliko kumjenga rais.
Mafanikio na kazi ilizofanywa na CCM hususani kwenye miundombinu, elimu na afya ni dhahiri, anayepinga na hilo ana lake jambo.
Tuliomaliza shule za msingi miaka ya 2000, hatujasahau mabadiliko makubwa yaliyoletwa na shule zilizobezwa kwa kupachikwa jina la shule za kata. Kabla ya shule za sekondali za kata, nakumbuka kutoka katika shule zetu za msingi walikuwa wanachaguliwa watoto wawili au watatu kujiunga na kidato cha kwanza, waliobaki walikuwa wakiingia mtaani. Nani anayebisha kuwa leo hii tuna madaktari, wahandisi, wachumi, wahasibu n.k walilelewa na hizi zilizoitwa shule za kata?
Namshukuru Mungu nimepata bahati ya kuizunguka nchi hii, kabla na baada ya miundombinu ya barabara hii tuliyonayo sasa. Huko tulikotoka, safari ya kibaha Dar, ungeweza kulala njiani, mm nikiwa moja wa mashuhuda mwaka 2007, nilipoenda Dar kwa mara ya kwanza. Sitasahau tuliingia kibaha saa moja na nusu tukafika ubungo saa saba usiku, huku mwenyeji wangu akiwa anaishi Gongo la mboto.
Ndugu zangu safari ya Mbeya Arusha ililazimu uzunguke kupitia Chalinze na Segera kwasababu hakukuwa na barabara ya Iringa-Mtera-Dodoma, pia Dodoma-Kondoa-Babati-Arusha ilikuawa Vumbi.
Tusisahau Dar to Mwanza tulikuwa tunazungukia Kenya kupitia Namanga na Silari kwasababu hakukuwa na barabara. Ni mwaka wa 2012 tu hapo, safari yangu kwa bus toka Moshi kwenda Kigali kupitia Tinde, Kahama, Bukombe, Lunzewe, Lusomo nilipita kwenye vumbi sehemu kubwa ya safari yangu wakati leo ni lami tupu.
Watu wa Lindi na Mtwara watakumbuka hali ilivyokuwa kabla ya daraja la Rufiji. In fact mikoa hii ilikuwa inafikika kwa njia mbili, meli na ndege. Ilifikafika wakati Lindi na Ntwara ilikuwa ni mikoa ya adhabu kwa watumishi wanye issue za kinizamu.
Katika sehemu zilizokuwa nyuma nchi hii ni mikoa ya magharibi, Katavi na Kigoma. Nakumbuka 2017 naenda kuripoti kazini hospitali ya manispaa ya Mpanda kutoka Dar nilitembea juu ya mkeka mpya wa rami toka Dar kupitia Sumbawanga mpaka naingia Mpanda sikuona Vumbi. Leo hii sio tu kupitia Mpanda, hali hii utaiona hata ukipitia Tabora.
Waulize wakazi wa Kigoma daraja la Maragalasi lipo hatua gani? Sikuhizi wanaotoka kigoma kuja Dar hawatambuliwi tena kwa kufika wamechafuka vumbi jekundu. Yote hii ni kazi ya CCM.
Yapo mambo binafsi naweza nisikubaliane nayo, mathalani namna upinzani unavyoshughulikiwa, lakini lknapokuja swala la maendeleo niliyoyashuhudia kwa macho yangu, siko tayari kuusaliti utashi wangu, CCM imefanya vizuri.
Kama tukimpima Raiis Samia kwa kazi zake, sote tutakubaliana, tunakila sababu ya kumuchagua tena amalizie kazi aliyoianza.

