Rais Samia akifanya haya, Wapinzani watakuwa na wakati mgumu

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,519
41,030
Matatizo mengi ya Tanzania, kwa kiasi kikubwa yanasababishwa na uongozi mbaya unaolindwa na sheria mbaya na Katiba mbovu.

Rais Samia, kwa dhamira yake, anaonekana ni mtu anayependa haki - hili amelitamka mara kadhaa.

Rais Samia anapenda demokrasia ya vyama vingi - hili alilitamka hata kule Nairobi aliposema, 'Nawapongeza Wakenya kwa demokrasia na namna bunge linavyojadili mambo mbalimbali kwa uhutu. Huwa napenda kuangalia Bunge la Kenya".

Rais Samia anaamini katika uchumi wa kisasa - ameliongea sana hili alipokemei TRA kwa primitivity katika ukasanyaji kodi.

Kwenye katiba mpya, alisema, hili lisubiri kwanza lakini hakusema moja kwa moja kuwa hatashughulikia.

Agenda kubwa za siasa za upinzani ni:

Katiba nzuri na bora
Haki za wananchi
Uhuru wa kujieleza na maoni
Uhuru wa vyombo vya habari
Sera rafiki za kodi
Sera rafiki za uwekezaji, biashara na uchumi kwa ujumla.

Kama Rais Samia akayatekeleza hayo yote, kama anavyoonekana kufanya, wapinzani watakuwa na wakati mgumu wa kupata agenda ya uchaguzi 2025.

Mapungufu makubwa ya utawala wa Rais Samia, mpaka sasa, ni kwamba yale mambo yote ambayo Rais ameonekana kuyachukia, ametoa tu kauli lakini hajafanya chochote kwenye sheria zinaruhusu hayo maovu kutendeka. Akilifanya hilo, itakuwa ni furaha na faida kwa Watanzania wote wanaolipenda Taifa lao.

Rais Samia, ni Mama, akiyafanya hayo yote niliyoyataja kwa kuyawekea sheria, wagombea kutoka vyama pinzani, ambao uwezekano mkubwa watakuwa wanaume, itakuwa ni ngumu sana hata kutoa zile kauli kali kali dhidi ya huyu Mama, wapiga kura wanaweza wasikuelewe, hasa kama watatoa kauli za kumdhalilisha Mama ambaye atakuwa amefanya mema mengi.

Uchaguzi ujao, Mungu akitujalia uhai, tutarajie siasa za kistaarabu kwa kiwango ambacho hakijawahi kuwepo.
 
Mama Samia ni wa kumpima kwa vitendo na sio maneno.

Kwa mfano, mpaka sasa hajaonyesha kwa vitendo kubadili sheria kandamizi/za hovyo hata moja mpaka hili Bunge linaisha.
 
Agenda kubwa za siasa za upinzani ni:

Katiba nzuri na bora
Haki za wananchi
Uhuru wa kujieleza na maoni
Uhuru wa vyombo vya habari
Sera rafiki za kodi
Sera rafiki za uwekezaji, biashara na uchumi kwa ujumla.

Kama Mama Samia akayatekeleza hayo yote, kama anavyoonekana kufanya, wapinzani watakuwa na wakati mgumu wa kupata agenda ya uchaguzi 2025.
Mkuu Bams nikuulize swali. Katika nchi za Marekani, Uingereza, Australia nk, kuna mfumo wa vyama vingi na vyote vinakuwa na nguvu sana. Kwa mfano, Marekani Democrats na Republicans wote wana nguvu sana.

Ndio kusema nguvu za vyama vya upinzani katika nchi hizi ni kwa sababu nchi hizo hazina mambo uliyotaja? Maana unasema Samia akiyafanya basi upinzani utakwisha. Na huko kwingine ambako upinzani una nguvu kama USA, ni kwa kuwa hayo mambo hayajafanyika?
 
Usichukue sana maneno ya wana tweeter ukazani yana beba matatizo ya wananchi wa kawaida na ambao ni wategemezi wa serikali.

Hii nchi inatatizo mengi na ya msingi kuliko yao ya uhuru wa habari na kujieleza.

Mama apige kazi.
 
Wenda mama mkuu may be akawa anatamani kuyafanya ila wale wajiitao wenye chama chao, wabunge ambao wapo pale KWA mbeleko wa mwendazake ,hawataki sikia katiba MPYA ambayo pia itazaa tume huru ya uchaguzi maana wanajua hawatarudi,

Kuyafanya haya itambini mama kufanya maamuzi magum , ili Taifa liendelee kumkumbuka hata asipogombea 2025, au chama chake kushinda 2025 ali Hali tiyari ni Rais na ataendelea kuwa Rais mstahafu sambamba na kupatiwa stahiki zake ,

Swali je ?
Mama yuko tiyari kuamua kwamba liwalo na liwe hasa la katiba KWA manufaa mapana ya Sasa na yabadae KWA taifa,????
 
Usichukue sana maneno ya wana tweeter ukazani yana beba matatizo ya wananchi wa kawaida na ambao ni wategemezi wa serikali.

Hii nchi inatatizo mengi na ya msingi kuliko yao ya uhuru wa habari na kujieleza.

Mama apige kazi.

Uhuru wa habari unazuia vipi matatizo ya wananchi kutatuliwa? Au hamtaki kutekeleza mambo ya msingi kwa kichaka kuwa mnatatua matatizo ya wananchi? Mama hana siasa za kishamba Kama za yule dhalimu, lakini hana jipya kwenye mustakabali wa nchi. Hapo alipo hana maamuzi yoyote zaidi ya kutekeleza matakwa ya ccm ya kubaki madarakani kwa shuruti. Na anakosa nguvu ya maamuzi kwani wahafidhina wa ccm wanaona kama yuko kwenye hicho cheo kwa hisani, na sio kwa mujibu wa katiba!
 
Katiba bora ni pale utakapokubali kuwapa madaraka upinzani.

Hata katiba iwe bora vipi, kama wataendelea Kushindwa malalamiko yako pale pale.
 
Matatizo mengi ya Tanzania, kwa kiasi kikubwa yanasababishwa na uongozi mbaya unaolindwa na sheria mbaya na Katiba mbovu.

Rais Samia, kwa dhamira yake, anaonekana ni mtu anayependa haki - hili amelitamka mara kadhaa.

Rais Samia anapenda demokrasia ya vyama vingi - hili alilitamka hata kule Nairobi aliposema, 'Nawapongeza Wakenya kwa demokrasia na namna bunge linavyojadili mambo mbalimbali kwa uhutu. Huwa napenda kuangalia Bunge la Kenya".

Rais Samia anaamini katika uchumi wa kisasa - ameliongea sana hili alipokemei TRA kwa primitivity katika ukasanyaji kodi.

Kwenye katiba mpya, alisema, hili lisubiri kwanza lakini hakusema moja kwa moja kuwa hatashughulikia.

Agenda kubwa za siasa za upinzani ni:

Katiba nzuri na bora
Haki za wananchi
Uhuru wa kujieleza na maoni
Uhuru wa vyombo vya habari
Sera rafiki za kodi
Sera rafiki za uwekezaji, biashara na uchumi kwa ujumla.

Kama Rais Samia akayatekeleza hayo yote, kama anavyoonekana kufanya, wapinzani watakuwa na wakati mgumu wa kupata agenda ya uchaguzi 2025.

Mapungufu makubwa ya utawala wa Rais Samia, mpaka sasa, ni kwamba yale mambo yote ambayo Rais ameonekana kuyachukia, ametoa tu kauli lakini hajafanya chochote kwenye sheria zinaruhusu hayo maovu kutendeka. Akilifanya hilo, itakuwa ni furaha na faida kwa Watanzania wote wanaolipenda Taifa lao.

Rais Samia, ni Mama, akiyafanya hayo yote niliyoyataja kwa kuyawekea sheria, wagombea kutoka vyama pinzani, ambao uwezekano mkubwa watakuwa wanaume, itakuwa ni ngumu sana hata kutoa zile kauli kali kali dhidi ya huyu Mama, wapiga kura wanaweza wasikuelewe, hasa kama watatoa kauli za kumdhalilisha Mama ambaye atakuwa amefanya mema mengi.

Uchaguzi ujao, Mungu akitujalia uhai, tutarajie siasa za kistaarabu kwa kiwango ambacho hakijawahi kuwepo.
Lissu Amsterdam mzima?
Asante kaka uwe na siku njema.
 
Uhuru wa habari unazuia vipi matatizo ya wananchi kutatuliwa? Au hamtaki kutekeleza mambo ya msingi kwa kichaka kuwa mnatatua matatizo ya wananchi? Mama hana siasa za kishamba Kama za yule dhalimu, lakini hana jipya kwenye mustakabali wa nchi. Hapo alipo hana maamuzi yoyote zaidi ya kutekeleza matakwa ya ccm ya kubaki madarakani kwa shuruti. Na anakosa nguvu ya maamuzi kwani wahafidhina wa ccm wanaona kama yuko kwenye hicho cheo kwa hisani, na sio kwa mujibu wa katiba!
Hana siasa za kishamba kama dhalimu, sasa kinachomzuia kufanya hayo matakwa yake ni kitu gani?
 
Mkuu Bams nikuulize swali. Katika nchi za Marekani, Uingereza, Australia nk, kuna mfumo wa vyama vingi na vyote vinakuwa na nguvu sana. Kwa mfano, Marekani Democrats na Republicans wote wana nguvu sana.

Ndio kusema nguvu za vyama vya upinzani katika nchi hizi ni kwa sababu nchi hizo hazina mambo uliyotaja? Maana unasema Samia akiyafanya basi upinzani utakwisha. Na huko kwingine ambako upinzani una nguvu kama USA, ni kwa kuwa hayo mambo hayajafanyika?
Hoja nzuri sana. Nadhani katika mataifa hayo, kinachotoa nguvu katika upinzani ni utofauti wa sera katika kufikia sera za kitaifa, na mbinu ambazo kila chama huwashawishi wapiga kura kuwa itazitumia.

Agenda za vyama haziwi kwenye ajenda za nchi bali kwenye namna ya kufikia sera ya kitaifa. Kwa mfano, sera ya nchi inasema, kila mwananchi ana haki ya kupata huduma bora za afya. Sera za vyama kwenye manifesto zao, kila chama kinaelezea namna chama hicho kitakavyotekeleza sera ya Taifa ya kumhakikishia kila mwananchi huduma nzuri ya afya.

Nakubaliana nawe, kama tuna vyama makini, upinzani utaendelea kuwa na nguvu kutokana na hoja mpya zitazokuwa zikiibuliwa kutokana na mazingira ya wakati husika.
 
Uhuru wa habari unazuia vipi matatizo ya wananchi kutatuliwa? Au hamtaki kutekeleza mambo ya msingi kwa kichaka kuwa mnatatua matatizo ya wananchi? Mama hana siasa za kishamba Kama za yule dhalimu, lakini hana jipya kwenye mustakabali wa nchi. Hapo alipo hana maamuzi yoyote zaidi ya kutekeleza matakwa ya ccm ya kubaki madarakani kwa shuruti. Na anakosa nguvu ya maamuzi kwani wahafidhina wa ccm wanaona kama yuko kwenye hicho cheo kwa hisani, na sio kwa mujibu wa katiba!

Ondoa kwanza mzimu wa mwendazake huko kichwani baada ya hapo soma tena.
 
Back
Top Bottom