Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 5,174
- 17,635
Rais Samia Suluhu Hassan amekabidhi magari 70 pamoja na vitendea kazi vingine kwa ajili ya kuimarisha usimamizi wa ardhi nchini.
Magari na vitendea kazi hivyo yamekabidhiwa kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Deogratius Ndejembi mkoani Dodoma, wakati wa hafla ya uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 1995 toleo la 2023.
Makabidhiano ya magari pamoja na vitendea kazi hivyo ni sehemu ya jitihada za Serikali katika kuhakikisha kunakuwa na usimamizi bora wa ardhi, huku sera hiyo mpya ikitarajiwa kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya ardhi.
Magari na vitendea kazi hivyo yamekabidhiwa kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Deogratius Ndejembi mkoani Dodoma, wakati wa hafla ya uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 1995 toleo la 2023.
Makabidhiano ya magari pamoja na vitendea kazi hivyo ni sehemu ya jitihada za Serikali katika kuhakikisha kunakuwa na usimamizi bora wa ardhi, huku sera hiyo mpya ikitarajiwa kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya ardhi.