Rais Samia achana na kuikumbatia CCM, fanya kazi zenye Maslahi mapana kwa Watanzania

Hahahahah majibu yatakuwa kama hivi:
Ufisadi vs Huduma bora. 5-0
Rushwa vs Haki. 7-1
Uwazi vs Kuminywa. 2-1

Hapo ndipo atakapokumbukwa yule ambaye anadhihakiwa na kukiri kuwa jamaa ndiye aliiweza nchi!
Mzee baba hii nchi ngumu sana, kuiongoza inahitaji zaidi ya kudemka
 
Kwa kikwete pia mlikuwa mnasema huu upumbavu ila alivyokuja magufuli mkaanza kutoa milio ya kila aina mkarudi kumkumbuka tena kikwete. Ndio maana mkapa aliwaita wapumbavu na malofa maana hamjui mnachosimamia
Inashangaza kwa kweli hii mijitu.

Hawan elimu wala uelewa wa mambo. Hivi ni mchumi gani anaejitambua angweza pendekeza salary increment baada ya hali tuliyopitia world wide? Kupunguza hats hiyo 1% ya PAYEE ni move ya kijasiri sana mama ameifanya. Tatizo sijui ni wajinga hawa, au hawako kwenye access ya information. Yaani yanajisemea tu haya majitu hakuna yajualo.

Besides Mheshimiwa rais mama Samia Suluhu Hassan ametoa mpaka ahadi kwamba next year salary zinapanda. Labda hajui wala hawezi tafsiri ile statement ya mama juu ya next years'may day.

Huyu jamaa ni bure kabisa na no hasara kwa Chadema
 
Kuongoza watu ni kazi ngumu sana mtu familia watu watano tu inakutoa jasho sembuse milion 60 tumwombee tu mama amalize muda wake vizuri ..haiwezi kubadilika ashakuwa rais huwezi kutengue hiyo
Kuongoza familia ni kazi kubwa kuliko nchi
 
Unajua wewe una akili nusu kabisa,hivi kwa akili yako rais anafanya kazi kwa kufuata matakwa yako?
Tena alivyo mwehu eti anamtaka rais aje aombe msamaha kwa makosa aliyoyafanya magufuli.

Anashindwa hata kuelewa kwamba rais si mtu ni taasisi
 
Si rahisi kwake kubadili mfumo uliomweka madarakani ambao upo kupitia uchaguzi mkuu haramu.
 
Mkuu tuache kwanza tusheherekee.

Nipo nimechinja jogoo kusheherekea kundolewa ile 'compound interest rate" ya 6% ya loan board aliyeanzisha Rais wenu "madhubuti" maana Deni lilikuwa haliishi linajizalisha tena utafikiri magugu maji na tumaini la kupanda daraja mwaka huu.

Adumu madarakani kwa miaka mingi Madame President.
Haya yote huyu mpumbavu hayaoni.

Sijui anataka mama amfanyie nini.

Watu wengine wakiitwa majina ya ajabu wanstahili kabisa.

Binaadam matatizo sana, yote aliyoyafanya mama in less than 50 days hayaoni huyu mpumbavu. Jana nimekaa na mwalim ambae amemshukuru Mungu kwa kuondolewa hii retention fee ila huku kuna wapumbavu wanasema mama hujafanya chochote
 
Ni minyoosho tu, mi ningetoa hoja tu kama uhuru mnaotaka ndio huu wa kuropoka upumbavu basi ntawafurahisha😂
Kuna watu wapo wapo tu hawajui hata nini wanataka. They are used to cruelty and harassment.

lkgjlxkstlb41.jpg
 
Hakika mimi uwa nasema ukweli bila sisi kama nchi kuacha kuishi ya Uongo uongo hakuna maendelea ambayo tutakuja kupata.

Mama Samia alionekana ni mtu atakaye kuja kufanya mageuzi makubwa lakini nasikitika hakuna kitu chochote mpaka sasa ambacho amefanya.

Kwanza alitoa ahadi ya ukaguzi maalumu BOT ambapo pesa zilichotwa kinyemela mpaka sasa kimya.

Aliagiza kufunguliwa kwa vyombo vyote vya habari mpaka sasa kimya.

Ameleta tume ya walimu wameikataa na yeye kakubali.

Unamtoa mwizi hazina unampeleka viwanda na biashara kwa kuogopa nini?

Haya mambo 4 yanaonyesha kama taifa hatuna kiongozi mwenye msimamo.

Kutokana na picha hii naomba kutoa ushauri kwa mambo yafuatayo

1: Mama aombe msamaha taifa Kwa uharibifu ambao Magufuli aliufanya then.

2: Ahachane na baadhi ya elephant project kama ununzi wa ndege kwa cash uku mishahara ikikushinda kuongeza.

3: Rais aanzishe haraka mchakato wa katiba mpya lasivyo atakwama pakubwa.

4: Rais aongelee swala la Bandari ya bagamoyo ambayo inaonekana ni mradi wa kifisadi kama inawezekana initial contract iwekwe wazi ili Watanzania tuone yaliyomo.

5: Janga la covid19 nalo umepiga kimya mi nasema atakaye ichezea corona itaondoka na yeye.


Nimesikitishwa na Hotuba ya Rais leo kuongelea swala la wafanyakazi wa umma na kuacha wafanyakazi wa sector binafisi ambao ndio wengi zaidi mfano wafanyakazi wa sector binafsi

Wamekuwa hawaunganishwi na mfuko wa taifa ya bima ya afya kwa lazima.

Wamekuwa hawaunganiswi na mfumo wa pension kwa lazima hivyo waajiri wanakiuka sheria za kazi.

Wamekuwa wanafanya kazi muda mrefu kwa malipo yaleyale yaani mtu analipwa laki 3 kwa mwezi halafu anafanya kazi kwa masaa 12 mpaka 18 kwa siku

Tena kwa masikitiko malimbikizo ya mishahara yanakuwa makubwa mtu unakuta anadai kwa miezi 2 au 3 nyuma na kwa kulinganisha maisha ya sasa yalivyo magumu je tunawatetea.

Mikataba ya wafanyakazi wa sector binafsi imekuwa haipo wanaopewa ni chini ya 5% ya watu wote wanaofanya kazi sector binafsi hii inafanya watu wafukuzwe hovyo bila kupewa stahiki zao

Wakati yote haya yanafanyika Nchi ina Rais , Makamu, Mawaziri,Wabunge,Wakuu wa mikoa,Wakuu wa wilaya, wakurugenzi, Idara ya usalama wa taifa, polisi, Takukuru, Tume za wafanyakazi na vyama vya wafanyakazi.

Nchi sasa inaonekana kama mtu anaongozewa na amewekwa Kama rubber stamp.

Usumbufu kwa wachimbaji wadogo umerudi kwa haraka sana why?

Vituo vya Mafuta baadhi hawatumii EFD tena why?

Ongezeko la madawa ya kulevya kwanini yameongezeka kwa haraka why?

Tunaongelea siku 50 tu za utawala wako mambo yamebadilika hivi je ndani ya miaka 5 hali itakuwaje?


Bila kifanya mageuzi makubwa ya kikatiba na kimfumo hakuna pahali mama samia ataenda.

Inawezekana anafanya either kwa kutokuwa na taarifa au anafanya makusudi.

Nchii hii kwanza mkubali ni yetu sote then tukiri tulikosea hapo nyuma kama nchi then hatujachelewa tuanze upya tusimike mifumo imara other wise kila rais atakuja na kuondoka maendeleo ya kweli hakuna.

Jiulize gharama za pesa zilizotumika leo kuwapeleka mwanza Rais, Makamo, waziri mkuu, Mawaziri wote, Wakuu wa mikoa kwenda kupiga polojo halafu kwenda kushusha kodi kutoka 9% kwenda 8%.

Mama samia akiendelea kukumbatia watu waovu ndani ya ccm atakwama pakubwa sana

Tunataka report ya CAG ya ukaguzi maalumu pale BOT.

Ukishindwa utakuwa Rais dhaifu zaidi kuwai kuongoza taifa hili mambo bado usilale.

Achana na kuikumbatia ccm Fanya kazi zenye Maslahi mapana kwa Watanzania.
Hizo bange ulizovuta usirudie tena kuvuta.

Unapoandika jambo humu ni vizuri kuweka ushahidi ili at least usionekane kilaza.

1.Unasema Rais aombe msamaha? Labda nikuulize wewe unataka aombaje??? Wakati alitangaza msiba wa JPM aliongeje kuhusu kushikamana kama Taifa na kutoangalia nyuma ?? Wewe ulitafsiri vipi ile kauli???

2. Unasema mishahara imemshinda kuongeza?? Wewe una akili kweli?? Mtu kachukua nchi ana siku hata 100 hazifiki Leo unataka aongeze tu mishahara??? Unajua kakuta kiasi gani kwenye hazina ya Taifa???

3. Mtu ndo kwanza ana siku hata 100 hazifiki unasema tu eti aanzishe mchakato wa Katiba mpya. Unajua kuwa huo mchakato wenyewe unaitaji hela?? Atapata wapi hizo hela??? Utampa wewe???

4. Bandari ya Bagamoyo unataka aongelee kivipi?? Aongeleeje?? Kwani kuna nini juu ya Bandari ya Bagamoyo ambalo ni lazima Rais aliongelee?? Nchi hii haina wataalaamu kuwa kila kitu kiongelewe na kufanywa na Rais?

5. Kuhusu covid kwani hajasema ameunda timu ya wataalam?? Wewe unataka kipi cha zaidi mfano??? Unataka afanye maamuzi bila ushauri wa wataalamu??? Alafu mseme anakurupuka????

6 Kwa iyo unataka serikali iendelee kuingilia sekta binafsi kama alivyofanya magufuli na kupelekea kuiua kabisa??? Kazi ya serikali ni kuweka mazingira mazuri kwa sekta binafsi ili iweze kuperform vizuri na kutoa matokeo. Kama mna madai kuhusu mishahara, platforms za vyama vya wafanyakazi zipo , Kwa nini msiende???

7. Unasema usumbufu wa machinga umerudi, kwa iyo unataka miji yetu iendelee kuchafuka na kuwa ya hovyo Kwa kuruhusu hovyo wamachinga kufanya biashara popote pale hadi barabarani??? Kwanza Unajua kufanya biashara Kwa mfumo wa machinga maana yale ni kuwa Wigo wa kodi unapungua???

8. Unasema vituo vya mafuta havitoi risiti kwani kuna sehemu mama amesema visitoe risiti??? Wewe kwa nini hujadai hizo risiti??? Umekwenda kuripoti TRA kuhusu Hilo jambo??? Alafu kwa nini hujavitaja hivyo vituo humu kuweka ushahidi wako ili mamlaka zifuatilie????

9. Unadai kuwa madawa ya kulevya yameongezeka kutumika, labda utoe mifano na ushahidi, ni wapi na lini ??? Sio unaongea tu juu juu na unataka watu wakuamini??? Hili ni jukwaa la great thinkers Kwa nini unatoa allegations bila ushahidi???

Nafikiri kwa bange zako ni heri ungesema kuwa dhaifu ni Mbowe Kwa sababu kwa miaka Karibu 25 ya uhai wa Chama chenu hamjafanikiwa kuwa hata na ofisi ya kujenga wenyewe ya Makao Makuu alafu mnakalia kusema yasio na msingi tu!
 
Mie nashangaa kuona anaruhusu COVID-19 waendelee kulipwa kiharamu pesa chungu nzima za walipa kodi bila kutia neno. Hizo pesa hao COVID-19 watazitolea tundu lolote kwenye miili yao.
Lakini mkuu, si ni nyinyi ndio mnasema mhimili wa bunge usiingiliwe???

Nakuheshimu tu mkuu lakini ningekuuliza swali ungesema nimekutukana
 
Naomba kuuliza kwani alitoa hadi lini ripoti iwe imekamilika? Kuweni na subra..na kuhusu ndege mbona amekuta zimeshalipiwa tayari ..hana jinsi..kiufupi mama nitaanza kumpima mwakani cause atakuwa ndio anafanyia kazi bajeti na vipaumbele vyake..ila kwa sasa mwacheni ajipange kwanza kakutana na mamiradi mikubwa hela zinazokusanywa asilimia kubwa zinaenda huko..hapo labda atafute wafadhili kwa baadhi ya miradi kisha makusanyo ya kodi ndio aelekeze ndani kwenye uchumi
Yaani akili zao wanataka ile miradi isimame?? Ikishasimama tutakuwa tumepata faida au hasara??

Yaani bwawa la kuzalisha umeme wa maji kazi isimame, halafu ndio iweje sasa?

Hawa watu akili zao zimekaa kama mavi
 
Back
Top Bottom