GE2025 Rais nataka nikuombee kura hapa Jamii Forums. Lakini nami nina Maombi yangu kwako

GE2025 Rais nataka nikuombee kura hapa Jamii Forums. Lakini nami nina Maombi yangu kwako

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

baz kaiza

JF-Expert Member
Joined
Jan 27, 2015
Posts
11,479
Reaction score
12,092
Rais wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Amirijeshi mkuu.

Naomba nikuombee kura hapa Jamii Forums hii ni platform kubwa huwezi kuimbeza.

Ila na mimi nina Maombi yangu kwako Mama kama manne hivi maana ninachokiomba kiko ndani ya Uwezo wako.

Mama kama unakumbuka kuna kipindi mitandao yote Tanzania ilikuwa inaimba sifa nzuri za kwamba unaupiga mwingi na ni kweli hapo nyuma uliupiga mwingi sana kila mtu alikuwa anakusifia ulitenda mambo mazuri sana.

Nakuja kwako mama na maombi yangu,

La kwanza naomba utoe tamko la kijana wetu Polepole apatikane, kama kuna makosa mama tafadhali naomba asamehewa huyu ni kijana mwana CCM mwenzetu kuelekea kwenye uchaguzi ili sio jambo jema ndani ya CCM kuna kura utazipoteza kisa huyu kijana.

Ombi langu la pili naomba umwachilie Tundu Antiphas Mughwai Lissu bila masharti yoyote kupitia DPP, niliowataja wote ni wapiga kelele tu na kelele za chura hazimnyimi tembo kunywa maji.

Nimekuomba hayo kwasababu Wewe ni Amiri jeshi Mkuu na kesi za Chadema zote zifutwe mahakamani.

Kuelekea Oktoba 29 ukifanya haya mama utakuwa umeponya Taifa na hutakuwa na deni na mtu na Utakuwa na amani moyoni mwako na kura utavuna za kutosha Oktoba 29

Achana kusikiliza wanafiki na wapambe hao ni watu wabaya tufungulie mitandao ya kijamii yote ikiwepo na JF yetu maisha yaendelee.
 
Mpaka sasa bado una amini kuwa ana nguvu yoyote kwenye hicho kiti?
Kama hana nguvu ndo tunaka tujue nani nyuma ya aya maana polepole hajawahi kumsema vibaya Rais Samia yeye alikua ana tatizo na wahuni. Mama Samia bado anaweza kutoa neno Polepole akapatikana tunamuitaji sana Polepole
 
Mimi binafsi nampenda aana Rais Samia ila hii tabia ya watu kutekwa na kupotezwa naomba airekebishe, atambue kuna maisha baada ya haya.
Damu ya mnyama yeyote ni ya thamani mbele za Muumba.
Mfano Polepole aliendelea kumuheshimu Samia hakuwai kumvunjia heshima yoyote tatizo lake walikua wahuni sasa Je hao wahuni ndo wamefanya aya Polepole kupotea Mama Samia naomba utoe tamko Polepole apatikane
 
Back
Top Bottom