Rais na Waziri anayehusika na NSSF toeni muongozo wazee wastaafu walipwe pensheni zao za mwezi wa kwanza

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Jan 26, 2013
18,670
22,261
Kuna wazee wastaafu ambao wameondolewa kwenye orodha ya wanaolipwa pensheni ya kila mwezi wakidhaniwa tayari wamefariki! Maafisa wa NSSF wanadai wamewaondoa ili pensheni zao zisichukuliwe na wajanja wao wakiwa tayari wamefariki!

Dhana hii inatokana na wazee hao kutohakikiwa, NSSF iliwajibika kuwapelekea taarifa kama wafanyavyo kwenye malipo lakini haikufanya hivyo kwa sababu wazijuazo wao.

Wengi wa wazee hawa malipo yao yapo kwenye wastani wa shs.250,000/=, Baada ya kujitokeza kwenye ofisi za NSSF wakiwa hao, wameambiwa watalipwa mwisho wa mwezi wa pili!

Wakati wazee hawa hawana ajira nyingine. Mwezi huu tumekuwa tukiwasikia walioko kwenye ajira wakilalamika haki ya kifedha kuwa ngumu kutokana na majukumu ya mwisho na mwanzo wa mwaka, sasa hawa wenye kipato kinacholingana na hela ya matumizi ya mwanafunzi wa sekondari ataishije mpaka mwisho wa mwezi wa pili!

Nilipowahoji NSSF kuhusu taarifa ya kujihakiki walisema ziko kwenye baadhi ya magazeti, japo hawakuweza kusema ni vipi mzee anayelipwa shs.250,000/= anaweza kununua magazeti yote kila siku ili akutane na tangazo la uhakiki wakati NSSF wanazo namba za simu za wazee hao! Ni wazi NSSF wamelichukulia swala la malipo haya ya wastaafu kuwa ni dogo sana na halina maana.

Waheshimiwa, kuna wazee walikuwa wana nauli ya kuwafikisha NSSF makao makuu wakijua watalipwa huko, lakini walijikuta hawana nauli ya kurudi makwao hivyo ikabidi wasaidiwe.

Ni tumaini langu viongozi wa juu mtaona umuhimu wa kulipwa mafao yao ya mwezi wa kwanza kwani chanzo cha tatizo ni NSSF kutojipanga.
 
Very sad indeed! Inauma sana kwa kweli. Kama suala la pension kwa waliokuwa wafanyakazi sio haki yao tena basi sheria zibadilishwe ili ijulikane wazi wazi. Hii itasaidia wananchi kujiandaa kivyao kwa ajili ya uzeeni badala ya pension kuonekana kama hisani ya serikali badala ya haki ya kisheria. WAJIBU WAO WALISHATEKELEZA, WAPENI HAKI YAO.
 
Mleta maada naomba kuuliza, ni NSSF au PSSSF?
Kama hii taarifa ni ya kweli, natarjia kusikia hao waliokula pesa za wastaafu kuwajibishwa Mara moja kwa mujibu wa Sheria. Unaanzaje kuleta uhuni kwa wazazi wako? Pumbavu kabisa. Mh. Rais Niteue Mara moja nisafishe hayo mafisi huko kwenye mifuko kimbilio la wzee wetu.
 
.... very sad indeed! Inauma sana kwa kweli. Kama suala la pension kwa waliokuwa wafanyakazi sio haki yao tena basi sheria zibadilishwe ili ijulikane wazi wazi. Hii itasaidia wananchi kujiandaa kivyao kwa ajili ya uzeeni badala ya pension kuonekana kama hisani ya serikali badala ya haki ya kisheria. WAJIBU WAO WALISHATEKELEZA, WAPENI HAKI YAO.
Zinatolewa kwa kuviziana! Ili kuondoa kuviziana NSSF ingeweka utaratibu wawe wanalipwa kwenye ofisi zao na ambaye hatafika kuchukua pensheni yake, atakuwa amekwisha fariki.
 
Zinatolewa kwa kuviziana! Ili kuondoa kuviziana NSSF ingeweka utaratibu wawe wanalipwa kwenye ofisi zao na ambaye hatafika kuchukua pensheni yake, atakuwa amekwisha fariki.
Kwa nini wasiwekewe kwenye akaunti zao?
 
Mleta maada naomba kuuliza, ni NSSF au PSSSF?
Kama hii taarifa ni ya kweli, natarjia kusikia hao waliokula pesa za wastaafu kuwajibishwa Mara moja kwa mujibu wa Sheria. Unaanzaje kuleta uhuni kwa wazazi wako? Pumbavu kabisa. Mh. Rais Niteue Mara moja nisafishe hayo mafisi huko kwenye mifuko kimbilio la wzee wetu.
Kichwa kinaonesha NSSF tofauti na PSSSF.
 
Miongoni mwa watu wanaoteseka vibaya ni wastaafu, Sijui hela zao ndio zinakwapuliwa kujenga chattle? I have a friend of mine who retired from government services 14 months ago, still he hasn't received any penny; just loitering in offices begging. Huu ni uuaji, wizi, unyang'anyi na ukosefu wa roho ya utu. Mwenyezi Mungu wapige kiboko wote wanaowasababishia mateso ya kinyama hao wastaafu.
 
Kuna Uzi mmoja humu nilichangia kuwa tatizo yaweza kuwa hali mbaya ya kifedha ya mifuko. Kanuni (formula) ya mifuko ili iwe endelevu wanatumia makusanyo ya wanachama + faida ya uwekezaji kulipa wastaafu. Sasa hivi hakuna ajira mpya Na kwà upande mwingine waliokuwa wanachangia ndiyo hao wanazeeka Na kuondoka. Kwa upande Wa pili miradi mingi waliyowekeza Nssf, biashara zinakufa. Kwa hiyo mashirika ya hifadhi yanatafuta upenyo Wa kupumulia. Twafa! The consequences of unemployment not only affects the younger!
 
Hivi kweli unafikiri ni rahisi kiasi gani kupiga simu kwa kila mstaafu Tanzania yote? Na je hizo namba walizoacha unahakika bado kwa wote zina exist?

Acheni lawama.

Serikali siku zote mambo yake hufanya kwa taarifa kwa njia ya vyombo vya habari, si simu.

Kama hawakufanya uhakiki wanapewaje pesa? Ni sahihi kabisa kupewa mwezi unaofuata.
 
Mleta maada naomba kuuliza, ni NSSF au PSSSF?
Kama hii taarifa ni ya kweli, natarjia kusikia hao waliokula pesa za wastaafu kuwajibishwa Mara moja kwa mujibu wa Sheria. Unaanzaje kuleta uhuni kwa wazazi wako? Pumbavu kabisa. Mh. Rais Niteue Mara moja nisafishe hayo mafisi huko kwenye mifuko kimbilio la wzee wetu.

Hebu tuliza mzuka.

Pesa hazijaliwa ila ni kuwa hawakufanya uhakiki kuthibitisha uwepo wao, naaamini kama wapo basi fedha zao watalipwa mwezi ujao.
 
Hivi kweli unafikiri ni rahisi kiasi gani kupiga simu kwa kila mstaafu Tanzania yote? Na je hizo namba walizoacha unahakika bado kwa wote zina exist?

Acheni lawama.

Serikali siku zote mambo yake hufanya kwa taarifa kwa njia ya vyombo vya habari, si simu.

Kama hawakufanya uhakiki wanapewaje pesa? Ni sahihi kabisa kupewa mwezi unaofuata.
Namba walizonazo ndizo zinazotumika kila mwezi kwa ajili ya malipo, kama hauna namba sijui utajulishwaje kuhusu malipo yako!
Ukijuacho wewe usiwapangie wengine.
 
Hebu tuliza mzuka.

Pesa hazijaliwa ila ni kuwa hawakufanya uhakiki kuthibitisha uwepo wao, naaamini kama wapo basi fedha zao watalipwa mwezi ujao.
Hao wazee pensheni shs. Laki mbili umwambie mwezi ujao! Hao walioko kazini shs Milioni moja ukimwambia mwezi huu haulipwi utalipwa mwezi ujao, sijui kama atakuelewa. Hata hivyo shs laki mbili fikiria anazitumiaje, kinachomsaidia hana gharama za nauli kila siku kwenda na kurudi, hana gharama za chakula chake kazini, mihangaiko ya starehe hana, ila lazima alipie maji na umeme.
 
Kuna wazee wastaafu ambao wameondolewa kwenye orodha ya wanaolipwa pensheni ya kila mwezi wakidhaniwa tayari wamefariki! Maafisa wa NSSF wanadai wamewaondoa ili pensheni zao zisichukuliwe na wajanja wao wakiwa tayari wamefariki!

Dhana hii inatokana na wazee hao kutohakikiwa, NSSF iliwajibika kuwapelekea taarifa kama wafanyavyo kwenye malipo lakini haikufanya hivyo kwa sababu wazijuazo wao.

Wengi wa wazee hawa malipo yao yapo kwenye wastani wa shs.250,000/=, Baada ya kujitokeza kwenye ofisi za NSSF wakiwa hao, wameambiwa watalipwa mwisho wa mwezi wa pili!

Wakati wazee hawa hawana ajira nyingine. Mwezi huu tumekuwa tukiwasikia walioko kwenye ajira wakilalamika haki ya kifedha kuwa ngumu kutokana na majukumu ya mwisho na mwanzo wa mwaka, sasa hawa wenye kipato kinacholingana na hela ya matumizi ya mwanafunzi wa sekondari ataishije mpaka mwisho wa mwezi wa pili!

Nilipowahoji NSSF kuhusu taarifa ya kujihakiki walisema ziko kwenye baadhi ya magazeti, japo hawakuweza kusema ni vipi mzee anayelipwa shs.250,000/= anaweza kununua magazeti yote kila siku ili akutane na tangazo la uhakiki wakati NSSF wanazo namba za simu za wazee hao! Ni wazi NSSF wamelichukulia swala la malipo haya ya wastaafu kuwa ni dogo sana na halina maana.

Waheshimiwa, kuna wazee walikuwa wana nauli ya kuwafikisha NSSF makao makuu wakijua watalipwa huko, lakini walijikuta hawana nauli ya kurudi makwao

Kuna wazee wastaafu ambao wameondolewa kwenye orodha ya wanaolipwa pensheni ya kila mwezi wakidhaniwa tayari wamefariki! Maafisa wa NSSF wanadai wamewaondoa ili pensheni zao zisichukuliwe na wajanja wao wakiwa tayari wamefariki!

Dhana hii inatokana na wazee hao kutohakikiwa, NSSF iliwajibika kuwapelekea taarifa kama wafanyavyo kwenye malipo lakini haikufanya hivyo kwa sababu wazijuazo wao.

Wengi wa wazee hawa malipo yao yapo kwenye wastani wa shs.250,000/=, Baada ya kujitokeza kwenye ofisi za NSSF wakiwa hao, wameambiwa watalipwa mwisho wa mwezi wa pili!

Wakati wazee hawa hawana ajira nyingine. Mwezi huu tumekuwa tukiwasikia walioko kwenye ajira wakilalamika haki ya kifedha kuwa ngumu kutokana na majukumu ya mwisho na mwanzo wa mwaka, sasa hawa wenye kipato kinacholingana na hela ya matumizi ya mwanafunzi wa sekondari ataishije mpaka mwisho wa mwezi wa pili!

Nilipowahoji NSSF kuhusu taarifa ya kujihakiki walisema ziko kwenye baadhi ya magazeti, japo hawakuweza kusema ni vipi mzee anayelipwa shs.250,000/= anaweza kununua magazeti yote kila siku ili akutane na tangazo la uhakiki wakati NSSF wanazo namba za simu za wazee hao! Ni wazi NSSF wamelichukulia swala la malipo haya ya wastaafu kuwa ni dogo sana na halina maana.

Waheshimiwa, kuna wazee walikuwa wana nauli ya kuwafikisha NSSF makao makuu wakijua watalipwa huko, lakini walijikuta hawana nauli ya kurudi makwao hivyo ikabidi wasaidiwe.

Ni tumaini langu viongozi wa juu mtaona umuhimu wa kulipwa mafao yao ya mwezi wa kwanza kwani chanzo cha tatizo ni NSSF kutojipanga.
Wakubwa kunatatizo kwani? Mimi mwenyewe kuna mtu wangu wa karibu kapata changamoto hii lakini kikubwa alicho elezewa na NSSF ni kwamba Zoezi la uhakiki wa wastaafu linafanyika kila mwaka ili kuweka sawa taarifa za wastaafu na kuondokana na kulipa pensheni hewa kwa wastaafu hewa yaani wasije walipa wasiohusika na jamaa kaongeza kuwa
baadhi ya wastaafu wamesimishiwa pensheni zao za mwezi, kutokana na kutoshiriki katika zoezi la uhakiki na mfuko huo Mkongwe.
 
Mleta maada naomba kuuliza, ni NSSF au PSSSF?
Kama hii taarifa ni ya kweli, natarjia kusikia hao waliokula pesa za wastaafu kuwajibishwa Mara moja kwa mujibu wa Sheria. Unaanzaje kuleta uhuni kwa wazazi wako? Pumbavu kabisa. Mh. Rais Niteue Mara moja nisafishe hayo mafisi huko kwenye mifuko kimbilio la wzee wetu.
Inaonekana mjibu hoja hii unaishi kwenye ivory tower yako,unataka kuniambia hujui yanayotokea kwa wastaafu wa nchi yetu?hujui kilichotokea kwa wastaafu wa iliyokuwa EAC?na kwa taarifa yako ni serikali kuu ndio iliyoiba fedha za watumishi wale!wapi wakashitakiwe?
 
Wakubwa kunatatizo kwani? Mimi mwenyewe kuna mtu wangu wa karibu kapata changamoto hii lakini kikubwa alicho elezewa na NSSF ni kwamba Zoezi la uhakiki wa wastaafu linafanyika kila mwaka ili kuweka sawa taarifa za wastaafu na kuondokana na kulipa pensheni hewa kwa wastaafu hewa yaani wasije walipa wasiohusika na jamaa kaongeza kuwa
baadhi ya wastaafu wamesimishiwa pensheni zao za mwezi, kutokana na kutoshiriki katika zoezi la uhakiki na mfuko huo Mkongwe.
Ni sawa linafanyika kila mwaka, lakini miaka yote walikuwa wanatoa taarifa kupitia namba za wastaafu walizonazo kama wafanyavyo kila mwezi kwenye malipo. NSSF ndio wanajua tarehe za uhakiki si jukumu la wastaafu kuuliza kila mara.
Sasa huyo mstaafu yupo hai kwanini wasimlipe pesa yake ambayo wameishikilia isichukuliwe kwenye akaunti yake ya benki! Kama ni rahisi hivyo mtu kuchukua pesa kwenye akaunti yako, basi hakuna sababu kuweka pesa benki, amini usiamini kuna zaidi ya hicho wanachosema NSSF.
Kitendo walichowafanyia wazee wastaafu ni kitendo cha kikatili ukichukulia udogo wa pensheni zenyewe na wazee ha hawawezi kuajiriwa ili wapate pesa za kujikimu.
 
Kwa wasiojua, NSSF hulipa pensheni za wastaafu kupitia akaunti za wastaafu za benki, kila malipo yanapofanyika hupelekwa ujumbe mfupi kwa mstaafu. Dhana ya watu wabaya kuchukua pesa kwenye akaunti ya mstaafu, ni dhana kuwa akaunti zote za benki haziko salama.
 
Kwa wasiojua, NSSF hulipa pensheni za wastaafu kupitia akaunti za wastaafu za benki, kila malipo yanapofanyika hupelekwa ujumbe mfupi kwa mstaafu. Dhana ya watu wabaya kuchukua pesa kwenye akaunti ya mstaafu, ni dhana kuwa akaunti zote za benki haziko salama.
Hii naielewa sasa mzee wangu alikuwa anangojea pensheni yake ya mwezi huu (anangoja sms ya muamala) akaona kimya ikabidi awaendee NSSF, wakamwambia kuwa mfuko umeweka utaratibu wa kuwapokea wanaoenda kuhakikiwa yaani wastaafu ambao pensheni zao zimestopishwa na kuwa pensheni hizo zitarudishwa mwezi wa pili ambapo watalipwa na za mwezi wa kwanza.
 
Back
Top Bottom