Rais mstaafu wa Tanzania Kikwete ateuliwa na AU kuwa mwakilishi maalum wa pembe ya Afrika na bahari ya Shamu

Rais mstaafu wa Tanzania Kikwete ateuliwa na AU kuwa mwakilishi maalum wa pembe ya Afrika na bahari ya Shamu

Retired

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2016
Posts
50,136
Reaction score
96,161
Umoja wa Afrika (AU) umetangaza kumteua Rais mstaafu wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, kuwa Mwakilishi Maalum wa AU kwa Ukanda wa Pembe ya Afrika na Bahari ya Shamu.

Mwenyekiti wa Tume ya AU, Mahmoud Ali Youssouf, amesema Kikwete ataongoza juhudi za kushughulikia changamoto za kisiasa, amani na usalama katika eneo hilo.

Majukumu yake yanahusisha kuendeleza diplomasia ya kuzuia migogoro, kurahisisha mazungumzo jumuishi, kujenga imani miongoni mwa wadau na kuimarisha ushirikiano wa kikanda.

Kikwete atashirikiana kwa karibu na IGAD, Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Jumuiya ya Nchi za Kiarabu, Umoja wa Mataifa na washirika wengine ili kuhakikisha hatua za pamoja zinakuwa na ufanisi.

AU imesisitiza kuwa uzoefu na uongozi wa Kikwete utachangia pakubwa kuimarisha amani, uthabiti na ustawi katika Pembe ya Afrika na Bahari ya Shamu, eneo lenye umuhimu wa kimkakati kwa biashara ya kimataifa na usalama wa bara zima.

20260325_212009.jpg
 
Umoja wa Afrika (AU) umetangaza kumteua Rais mstaafu wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, kuwa Mwakilishi Maalum wa AU kwa Ukanda wa Pembe ya Afrika na Bahari ya Shamu.

Mwenyekiti wa Tume ya AU, Mahmoud Ali Youssouf, amesema Kikwete ataongoza juhudi za kushughulikia changamoto za kisiasa, amani na usalama katika eneo hilo.

Majukumu yake yanahusisha kuendeleza diplomasia ya kuzuia migogoro, kurahisisha mazungumzo jumuishi, kujenga imani miongoni mwa wadau na kuimarisha ushirikiano wa kikanda.

Kikwete atashirikiana kwa karibu na IGAD, Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Jumuiya ya Nchi za Kiarabu, Umoja wa Mataifa na washirika wengine ili kuhakikisha hatua za pamoja zinakuwa na ufanisi.

AU imesisitiza kuwa uzoefu na uongozi wa Kikwete utachangia pakubwa kuimarisha amani, uthabiti na ustawi katika Pembe ya Afrika na Bahari ya Shamu, eneo lenye umuhimu wa kimkakati kwa biashara ya kimataifa na usalama wa bara zima.

View attachment 3562761
Aliye nacho huongezewa, asiye nacho hata kidogo alichonacho, hunyang'anywa.

Pongezi kwake mheshimiwa JK.
 
Chama dola kongwe kina mbinu za kujisafisha kabla pigia mstari neno kabla, wakati na baada ya 29 October 2026 kwa kupeleka makada wao Jumuiya za Kikanda

Hawa wote ni lazima Samia aandike barua ya kuwakingia kifua kuwa serikali yake haramu inawapendekeza na kuwaruhusu watumike katika taasi za kikanda na kimataifa

TOKA MAKTABA:

WE NEED TO TELL OUR STORIES OF COURAGE AND RESILIENT

October 22 2025
Windhoek, Namibia

Ambassador Liberata Mulamula’s Remarks | “She Stands for Peace” 3rd Edition Launch | #UNSCR1325at25


View: https://m.youtube.com/watch?v=c2QFpOli4Yg
Ambassador Liberata Mulamula, African Union (AU) Special Envoy on Women, Peace and Security (WPS), delivers inspiring closing remarks at the launch of She Stands for Peace 3rd Edition during the 25th Anniversary celebrations of UN Security Council Resolution 1325 in Windhoek, Namibia.

Balozi Liberata Mulamula, Mjumbe Maalum wa Umoja wa Afrika (AU) kuhusu Wanawake, Amani na Usalama (WPS). aliyeteuliwa mnamo Agosti 2025, ni Mjumbe Maalum wa Umoja wa Afrika (AU) kuhusu Wanawake, Amani na Usalama (WPS). Akiwa mwanadiplomasia mzoefu wa Tanzania na Waziri wa Mambo ya Nje wa zamani, anaongoza juhudi za AU za kuendeleza ushiriki wa wanawake katika ujenzi wa amani na utatuzi wa migogoro kote Afrika, akizingatia uwajibikaji, uongozi wa vizazi mbalimbali, na kuimarisha Ajenda ya Wanawake, Amani na Usalama..

Majukumu na Vipaumbele Muhimu:
  • Kuendeleza Ajenda ya WPS: Kukuza ushiriki kamili na wenye maana wa wanawake katika kuzuia migogoro, mazungumzo ya amani, na urejeshaji wa migogoro baada ya migogoro.
  • Uwajibikaji na Athari: Kusonga mbele zaidi ya ujumuishaji wa mfano hadi kupima ushawishi wa wanawake katika michakato ya amani, haswa kupitia " Azimio la Windhoek+25 ".
  • Maeneo Muhimu ya Kuzingatia: Kuimarisha Mfumo wa Matokeo ya Bara (CRF) ili kufuatilia ahadi za Nchi Wanachama, kuimarisha ufadhili wa mipango ya amani inayoongozwa na wanawake, na kushughulikia vitisho vinavyoibuka vya usalama kama vile mabadiliko ya hali ya hewa na kuhama kwa watu.
  • Ushirikiano: Kufanya kazi na Nchi Wanachama wa AU, Jumuiya za Kiuchumi za Kikanda (RECs), na asasi za kiraia ili kukuza sauti za wanawake katika michakato ya amani.
Usuli na Uzoefu:
  • Kazi ya Kidiplomasia: Zaidi ya miaka 35 ya uzoefu katika diplomasia, utawala, na utatuzi wa migogoro.
  • Nafasi Muhimu: Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Katibu Mtendaji wa zamani wa Mkutano wa Kimataifa kuhusu Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR).
  • Utambuzi: Mwanzilishi katika Mtandao wa Viongozi Wanawake wa Afrika (AWLN) .
Balozi Mulamula analenga kutoa matokeo yanayoonekana, akilenga kutafsiri sera kuwa maboresho halisi kwa wanawake katika jamii zilizoathiriwa na migogoro
 
Huyu ndio anachochea migogoro hapa nchini anateuliwa kwenda kushugulikia migogoro hiki ni kituo kingine
 
JK ni CIA viongozi wengi afrika ni agents wa Mabeberu hata la MO29 Jk alijua litapita tu
 
Back
Top Bottom