Umoja wa Afrika (AU) umetangaza kumteua Rais mstaafu wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, kuwa Mwakilishi Maalum wa AU kwa Ukanda wa Pembe ya Afrika na Bahari ya Shamu.
Mwenyekiti wa Tume ya AU, Mahmoud Ali Youssouf, amesema Kikwete ataongoza juhudi za kushughulikia changamoto za kisiasa, amani na usalama katika eneo hilo.
Majukumu yake yanahusisha kuendeleza diplomasia ya kuzuia migogoro, kurahisisha mazungumzo jumuishi, kujenga imani miongoni mwa wadau na kuimarisha ushirikiano wa kikanda.
Kikwete atashirikiana kwa karibu na IGAD, Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Jumuiya ya Nchi za Kiarabu, Umoja wa Mataifa na washirika wengine ili kuhakikisha hatua za pamoja zinakuwa na ufanisi.
AU imesisitiza kuwa uzoefu na uongozi wa Kikwete utachangia pakubwa kuimarisha amani, uthabiti na ustawi katika Pembe ya Afrika na Bahari ya Shamu, eneo lenye umuhimu wa kimkakati kwa biashara ya kimataifa na usalama wa bara zima.
Mwenyekiti wa Tume ya AU, Mahmoud Ali Youssouf, amesema Kikwete ataongoza juhudi za kushughulikia changamoto za kisiasa, amani na usalama katika eneo hilo.
Majukumu yake yanahusisha kuendeleza diplomasia ya kuzuia migogoro, kurahisisha mazungumzo jumuishi, kujenga imani miongoni mwa wadau na kuimarisha ushirikiano wa kikanda.
Kikwete atashirikiana kwa karibu na IGAD, Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Jumuiya ya Nchi za Kiarabu, Umoja wa Mataifa na washirika wengine ili kuhakikisha hatua za pamoja zinakuwa na ufanisi.
AU imesisitiza kuwa uzoefu na uongozi wa Kikwete utachangia pakubwa kuimarisha amani, uthabiti na ustawi katika Pembe ya Afrika na Bahari ya Shamu, eneo lenye umuhimu wa kimkakati kwa biashara ya kimataifa na usalama wa bara zima.