Al Zagawi
JF-Expert Member
- Mar 17, 2009
- 2,461
- 1,448
Wadau,
Majuzi hapa wakati wa-Japan wanakumbuka wenzao walipoteza hali, mali na nafsi katika tsunami ya mwaka uliopita Mh Rais Mkapa alikuwa ni katika wageni waalikwa ambao walikaribishwa jukwaani na kutoa hotuba. Balozi wa Japan hapa nchini alikuwa ni mwenyeji katika hafla hiyo pamoja na wageni wengine kadhaa.
Kilichonishangaza ni kuwa Raisi Mkapa alipokaribishwa jukwaani, alitoa hotuba yake kwa ki-ingereza(sijui kama ni english phobia au laa) wakati mwenyeji wa shughuli, balozi wa Japan, alitoa hotuba yake kwa Kiswahili.
Ni kwa mantiki hiyo nauliza swali hili je, mh sana Ben Mkapa ana nini na kiswahili chetu, hakipendi au ni vipi?
Nauliza nikiwa na kumbukumbu kuwa wakati fulani akiwa madarakani, alikwenda Addis Ababa kuhudhuria mkutano wa AU. Wakati huo AU ilikuwa imetoka kupitisha azimio la kuruhusu hotuba za wakulu kutolewa kwa kiswahili, mh Mkapa alichagua kutumia kingereza lakini Joachim Chissano akatumia kiswahili kwa muda wa kutosha na baadae ki-reno.
Hivi kuna aibu gani ya Rais Mmachinga, Mndengereko, Mchaga, n.k. akatumia kiswahili katika kutoa hotuba huko ughaibuni? Hivi pasi na juhudi za makusudi za wakiwemo watawala(usiseme viongozi maana hakuna njia wanayotuongoza kuipita), hiki kiswahili kitakuwa kweli.
Kuna lugha inaitwa Fursi...inaongewa na taifa moja tu duniani, Iran na bado Ahmadinejad anatamba nayo mpaka UN.
Hivi, ni kweli kuwa tumethubutu, tumeweza na tunasonga mbele au ni porojo za alinacha kama kawaida yetu.
Majuzi hapa wakati wa-Japan wanakumbuka wenzao walipoteza hali, mali na nafsi katika tsunami ya mwaka uliopita Mh Rais Mkapa alikuwa ni katika wageni waalikwa ambao walikaribishwa jukwaani na kutoa hotuba. Balozi wa Japan hapa nchini alikuwa ni mwenyeji katika hafla hiyo pamoja na wageni wengine kadhaa.
Kilichonishangaza ni kuwa Raisi Mkapa alipokaribishwa jukwaani, alitoa hotuba yake kwa ki-ingereza(sijui kama ni english phobia au laa) wakati mwenyeji wa shughuli, balozi wa Japan, alitoa hotuba yake kwa Kiswahili.
Ni kwa mantiki hiyo nauliza swali hili je, mh sana Ben Mkapa ana nini na kiswahili chetu, hakipendi au ni vipi?
Nauliza nikiwa na kumbukumbu kuwa wakati fulani akiwa madarakani, alikwenda Addis Ababa kuhudhuria mkutano wa AU. Wakati huo AU ilikuwa imetoka kupitisha azimio la kuruhusu hotuba za wakulu kutolewa kwa kiswahili, mh Mkapa alichagua kutumia kingereza lakini Joachim Chissano akatumia kiswahili kwa muda wa kutosha na baadae ki-reno.
Hivi kuna aibu gani ya Rais Mmachinga, Mndengereko, Mchaga, n.k. akatumia kiswahili katika kutoa hotuba huko ughaibuni? Hivi pasi na juhudi za makusudi za wakiwemo watawala(usiseme viongozi maana hakuna njia wanayotuongoza kuipita), hiki kiswahili kitakuwa kweli.
Kuna lugha inaitwa Fursi...inaongewa na taifa moja tu duniani, Iran na bado Ahmadinejad anatamba nayo mpaka UN.
Hivi, ni kweli kuwa tumethubutu, tumeweza na tunasonga mbele au ni porojo za alinacha kama kawaida yetu.