Umeangalia upande mmoja wa riba. (Hakimu mzuri mtenda haki hufanya maamuzi kwa kuangalia pande zote 2)
Riba, VAT kwa miamala ya simu na bank, mfumuko wa bei za bidhaa na kushuka sana kwa bei ya mavuno shambani.
(Hivi ni vinamuumiza mtu wa hali ya chini vinahitaji marekebisho)..
Usimamizi wa kodi stahiki kwa makampuni na wafanyabiashara wakubwa, uongozi wa serikali thabiti km kwenye halmashauri kwa wakubwa na wadogo, kuzuiwa kwa mitandao ya madawa ya kulevya kwa kukamatwa wahusika wakubwa, kupungua kwa mianya ya rushwa na kubana matumizi kwa baadhi ya shughuli km safari za nje( haya ni baadhi yanamuumiza mwenye kipato cha juu tofauti na alivyozoea awamu zilizopita)
Elimu bure kwa waliokuwa hawana fedha kusomesha watoto wao, usimamizi, uwajibikaji na ufuatiliaji kwa madaktari na walimu, umakini ktk hospitali, ununuzi wa vitanda na huduma kwa wagonjwa na wajawazito, kuondolewa kwa ushuru na tozo ndogo ndogo kwa wafanyabiashara wadogo wa mbogamboga na mama ntilie (haya ni baadhi ya kutetea wanyonge)
Riba ikiwa kubwa hata mwenye kipato cha juu pia kina muumiza na kinamuathiri pamoja na serikali yenyewe.