Daudi Mchambuzi
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 62,190
- 128,264
Kina Lugumi, Mkapa, Muhongo,Kikwete ndiyo wanyonge pekee anaowazungumzia Magufuli.
Naiona ccm ikifa mwaka 2020!
!
Labda wanyonge wa Chato mkuu maana hata huku nilipo hakuna unafuu wowote ule.
Mkuu kwanza pokea LIKE kubwa sana...kutoka kwangu...Nimekuwa nikiumia sana na nchi yangu kwa mambo yanayoendelea !!
Rais Magufuli nipo hapa leo kuongelea mwenendo wa nchi yetu kwenye suala la kiuchumi!!!
Suala lako la kubana matumizi ni zuri lakini unalifanya liwe gumu kwa wananchi wako jinsi unavyochukua hatua!!
Hatua zako hazionekani kuwa za kisayansi kufanya utafiti kuwasaidia wananchi wa kawaida!!!
Riba ya Mabenki
Mh : Riba ya mabenki yetu ipo juu mno kiwango ni 24%-30% kwa mwanachi wa kawaida mfano ukikopa 10,000,000 atatakiwa alipe milioni 13,000,000 sasa hiyo liba ya milioni tatu ndio inawezekana ikawa faida kwenye biashara mtu anayoifanya lakini yote anairudisha kuilipa kama Riba !!
Wewe bado ujaliona hilo lakini Jirani yako Uhuru Kenyatta ameliona hilo kaamua kusaini mswada wa sheria kupunguza Riba ya mabenki kutoka 22%-24% na kuwa 10.5%-14.5 wewe bado hata swala la mabenki hakuna siku nimesikia ukiliongelea!!
Uwezi kujenga uchumi bila kuimulika sector ya mabank Tanzania!!
Sasa hivi kuna vijana wanaitimu Chuo kikuu walitakiwa kukuta Riba imeshushwa ili watumie vyeti vyao vya kuitimu kukopea pesa kwenye mabenki ni kitendo cha kuweka Sera wewe upo kimya !!!
Tatizo la Ajira litaisha vipi kama waitimu wa vyuo vikuu watamaliza vyuo bila kupata mikopo ya kujiajiri na kuajiri wenzao wa Form 4&6?
Tatizo la Ajira tunalitengeneza sisi wenyewe wala hatutakiwi kutafuta mchawi wachawi ni sisi wenyewe!!!
Mbona mswada wa mahakama ya mafisadi uliwaiswa kupelekwa bungeni ingawa hata hatuoni ukifanya kazi ??
Kwanini tusipeleke mswada wa kupunguza Riba tukaacha kuwakamua Watanzania na kuwavutia waitimu wa vyuo vikuu wajiajiri wenyewe?
Kila mwaka tunasikia mabank kama Crdb,Nmb wanatangaza faida ya billions of money, hiyo faida kwanini hata nusu yake isipunguziwe kwenye kushusha Riba ya mabenki ili kuwasadia waitimu wa vyuo vikuu na wawekezaji wa ndani!!
Bado Mimi sijaelewa Mtukufu Rais Magufuli wewe ni Rais wa wanyonge wapi??
Kweli nimeamini hawa jamaa wakifa uwa hawaendi mbuguni!!Mkuu kwanza pokea LIKE kubwa sana...kutoka kwangu...
Tatizo la serikali ya awamu hii hawapendi watu wenye mawazo mbadala kama haya....Wao wanataka kusifiwa tu hata penye hamna.....
Kama viongozi angekubali kupokea ushauri kama huu na wakaufanyia kazi, hakika tungepiga hatia kubwa sana kama taifa.......
Hata kutoa elfu kumi wanakata hela nyingi yani.Leo Ukimtumia bibi yako kijijini sh 200,000/ kwenye simu, ajiandae kukatwa sh 5,000/. Huyu ndo maskini ambaye anatakiwa rais kumfikiria
Kwanini we ongea bwana bora useme ukweli uende mbinguni kuliko kuishi duniani kinafiki!!Mods wakienda kunywa Chai ntaandika...
Nchi hii sasa hawapendi kusikia ukweli mkuu... Ni shida tupu juu ya ardhi hii... Vitisho kila mahali.Kwanini we ongea bwana bora useme ukweli uende mbinguni kuliko kuishi duniani kinafiki!!
Nimeanza kuelewa kwanini Ccm uchaguliwa na wajinga?Sijawahi jutia kura yangu.
Unataka niwe wapi?Bado upon uraiani we kiumbe?
Labda masikini wa fikra😀Yaani nashindwa kabisa kuelewa ni masikini wapi anamaanisha ?