Rais Magufuli: Vijiji vilivyobakia kupata umeme Tanzania bara ni vijiji 3000 tu

mulwanaka

JF-Expert Member
Feb 19, 2017
5,262
12,835
"Katika kipindi Cha awamu ya tano Mimi pamoja na nyinyi wakati tukitekeleza ilani ya Chama chetu Cha Mapinduzi tulijiwekea mipango yetu na mipango hiyo ilitakiwa itekelezwe katika kipindi Cha miaka mitano, Mipango mingi Sana tumeitekeleza. Tuna mpango wa kuweka umeme katika kila Kijiji nchini, vijiji vilivyopokea umeme wa Rea Ni vijiji 9114 bado vijiji 3000 kila Kijiji lazima kiwe na umeme na huu ni mpango ambao bado hatujaukamilisha."
 
Husikiagi viwanda viwanda!!! Ila usihoji viwanda vya nini na vipo wapi. Sasa sijui kwa umeme maana nyaya mi zimepita batini kwangu ila umeme nauskia kwenye bomba
 
Rais Magufuli ameweka rekodi ya kupeleka umeme kila kijiji Tanzania

Hii haijawahi kutokea kwa Africa
Ahsante Magufuli kwa kuwatumikia Watanzania
Wewe unaota ndoto zinazosababishwa na uelewa mdogo. Nenda Ghana ti hapo ukaone umeme ulivyosambaa vijijini. Na ulisambaa tangu miaka zaidi ya 30 iliyopita. Watu hawaongelei kwa sababu wanaona ni kitu cha kawaida.

Nenda Mali, nchi maskini na sehemu kubwa ni jangwa, ukaone jinsi flyovers (siyo madaraja), zinavyoonekana ni kitu cha kawaida (Tanzania inaonekana ni muujiza).

Ukiwa mjinga na maskini, unaweza kupewa baiskeli, ukaamini hakuna chombo kizuri kusafiria zaidi ya baiskeli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
"Katika kipindi Cha awamu ya tano Mimi pamoja na nyinyi wakati tukitekeleza ilani ya Chama chetu Cha Mapinduzi tulijiwekea mipango yetu na mipango hiyo ilitakiwa itekelezwe katika kipindi Cha miaka mitano, Mipango mingi Sana tumeitekeleza. Tuna mpango wa kuweka umeme katika kila Kijiji nchini, vijiji vilivyopokea umeme wa Rea Ni vijiji 9114 bado vijiji 3000 kila Kijiji lazima kiwe na umeme na huu ni mpango ambao bado hatujaukamilisha."
Vijiji vitatu ambavyo ni Kamwanga,Nyamikoma na Rwenge vilivyopo Mkoa wa Geita,wilaya ya Geita havina vyote kwa pamoja havina nishati ya umeme na havijawekwe kwenye mpango wa REA na ikumbukwe kuwa Rais na waziri wa nishati wanatokea na wamezaliwa mkoa wa Geita. Vijiji hivi havia barabara ,shule ya sekondari,Wala maji. Vijiji hivi vinazungukwa na mgodi mkubwa duniani wa kuzalisha dhahabu ,mgodi wa Geita gold mine.GGM. Tunaomba mh Rais kipindi Cha kampeni aweze kutembelea vijiji hivi na kujione mwenyewe na wako tayari kuichagua CCM . Mkuu wa mkoa wageita,mkuu wa Wilaya ya Geita hawajawahi kutembelea vijiji hivi vitatu tangu Uhuru. Hata mawasiliano ya simu Ni shida kuwasiliana na huduma za afya Ni shida,
 
Back
Top Bottom