Rais Magufuli unahubiri kupinga ubeberu Afrika wakati wewe unataka kuwa beberu dhidi ya waganda?

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Rais Magufuli sidhani kama unatamani mafuta ya waganda yachimbwe kuliko waganda wenyewe! Hivi nikuulize swali? Wale wenye mitambo ya kuchenjulia makinikia kule Japan ambapo umezuia makontena kwenda huko wakaja hapa nchini kisha wakahubiri weee na wakamalizia kwa kusema "Mfukuze huyo mkuu wa bandari kwa kuwa anatukwamisha kwa kuzuia hayo makinikia kuchenjuliwa, You have to lose "Litre" and gain more" Utakubali? Utakubali kuwa wenye smelter waseme kuwa mkuu wa bandari anakukwamisha hivyo mfukuze kazi?

Narudia tena, sidhani kama hayo mafuta ya waganda una uchungu nayo kuliko waganda wenyewe. Wewe unataka waganda waingie hasara kwa vile tu bomba linalopitisha hayo mafuta halina hasara yoyote kwani utalipwa kwa pipa linalopita pale? Wao wapate hasara ili waharakishe wewe uingize hela kwenye bomba na mambo ya ulinzi?

Ukiona kamishina wa mapato wa Uganda amekataa hilo ujue anaona kabisa hakuna maslahi, yeye siyo mjinga hadi akatae nchi yake kuchimbwa mafuta! Ukiona naye Museven kakaa kimya pia siyo mjinga! Kuna vingi anaangalia. Hawawezi kujiingiza mkenge ili kumnufaisha Magufuli kisiasa!

Haya uliyohubiri juzi kwakweli ni Ubeberu asilimia 100. Naamini sasa Waganda wamekuelewa na wameelewa kwanini unatumia nguvu kubwa sana kunyamazisha wanaoelewa na kisha kukosoa.

Nimeshangazwa sana, Rais wa nchi tena jirani unahubiri waziwazi kuifanya nchi jirani yako kuingia mkenge wakati huku kwako unazuia tena kila siku kuwalaumu watangulizi wako kwa kuingia mkenge? Tafadhali sana mheshimiwa Rais usionyeshe waziwazi kuwa umejiwekea ubinafsi sehemu fulani ya mwili wako. Kwa kasi hii angalia sana Kagame asije kuku....Maana kwa jinsi anavyojikomba atakuwa ameshakuelewa.

Halafu kusema vile mbele ya mkuu mwenzako wa nchi wala haijakaa poa kabisa kabisa.
 
wanaojifany kupinga sana ubeberu ndio wangekuwa mabeberu makubwa kama wangekuwa na uwezo

ubeberu ni kujiona taifa lako ni bora kuliko mengine na kulazimisha mataifa mengine kufuata tamaduni zako na itikadi zako
Magufuli ana attitude za kibeberu kama Nyerere alivyokuwa, atttude zenyewe ni kama hizi za kulazmisha kwa nguvu zote Kiswahili eti ni lugha ya kimataifa wakati hata hapo Uganda hawaifahamu, Waziri wa Museven tu juzi kwenye mkutano alikuwa haelewi Kiswahili japo yeye ni kati ya watu wenye exposure kubwa huko Uganda, alipoenda Malawi kwenyewe alihitaji translator hawakielewi ila jamaa anavyolazimisha kuki impose sasa dah..!

Badala ya ku intergrate nchi yako na dunia, wananhi waelewe kinachoendelea duniani, wewe unawaambia eti wasijifunze lugha za kigeni,unalazimisha ku impose culture yako

Walitoa msaada kidogo hapo msumbiji wakati wa kimbunga, wakaanza kujigamba na kusema eti wana TanzaAid, wakati wao walipewa msaada wakati wa tetemeko, purely attitude za kibeberu
 
Katika utafiti wangu nimegundua kuwa watu wanaendeshwa na mihemuko ya kiitikadi, jambo linalowafanya kushindwa hata kuelewa ambacho amekisema mtu fulani badala yake kudhihaki na matusi. nimesikiliza kwa makini kauli ya Mhe Rais hakuna mahala alipo muagiza M7 kuwafukuza maafisa wake wa URA bali alitoa kama ushauri tena akisema "mzee sikufundishi kazi" lakini mnaojua kutafsiri mnageuza kauli. Huo ni ni unafiki na uchonganishi
 
Boss G Sam Ushauri wangu: Ningependa sana Mambo ya Kitaifa, Tuwe kitu kimoja, Mambo ya Ndani, ndio Tumchane Mh. Rais. Maana hilo Bomba likifanikiwa kujengwa, anayefaidika ni Wananchi na Taifa na si Mh. Rais iwapo ... Tushajua ... Mapungufu ya Mh. Rais.
 
Katika utafiti wangu nimegundua kuwa watu wanaendeshwa na mihemuko ya kiitikadi, jambo linalowafanya kushindwa hata kuelewa ambacho amekisema mtu fulani badala yake kudhihaki na matusi. nimesikiliza kwa makini kauli ya Mhe Rais hakuna mahala alipo muagiza M7 kuwafukuza maafisa wake wa URA bali alitoa kama ushauri tena akisema "mzee sikufundishi kazi" lakini mnaojua kutafsiri mnageuza kauli. Huo ni ni unafiki na uchonganishi
Huo ujumbe eti sikufundishi kazi ilikuwa ni kautetezi tu kakupunguza makali ila alimaanisha hivyo hadi akatamani waamie Tanzania ili a deal nao. Rudia tena kusikiliza.
 
Boss G Sam Ushauri wangu: Ningependa sana Mambo ya Kitaifa, Tuwe kitu kimoja, Mambo ya Ndani, ndio Tumchane Mh. Rais. Maana hilo Bomba likifanikiwa kujengwa, anayefaidika ni Wananchi na Taifa na si Mh. Rais iwapo ... Tushajua ... Mapungufu ya Mh. Rais.
Hapana.. Huku kwetu tunawalaumu sana Ben na JK kwa kusaini mikataba ya hovyo. Basi kwa kuzingatia hilo tuwe na ubinadamu kwa wenzetu ili lawama zetu zikamilike. Unafiki ni kitu kibaya. Wao wamekataa kutokana na maslahi. Unataka baadaye mrithi wa Museven aje kutoa lawama kama nyie?
 
Katika utafiti wangu nimegundua kuwa watu wanaendeshwa na mihemuko ya kiitikadi, jambo linalowafanya kushindwa hata kuelewa ambacho amekisema mtu fulani badala yake kudhihaki na matusi. nimesikiliza kwa makini kauli ya Mhe Rais hakuna mahala alipo muagiza M7 kuwafukuza maafisa wake wa URA bali alitoa kama ushauri tena akisema "mzee sikufundishi kazi" lakini mnaojua kutafsiri mnageuza kauli. Huo ni ni unafiki na uchonganishi
Kulikuwa na haja gani kwa Kiongozi Mkuu wa Nchi kutamka vile tena mbele za watu wenye uelewa tofauti? Alishasema ashauriwi wala hapangiwi na mtu, yeye inakuaje kuwapangia/kuwashauri wengine?? Hapo ndipo penye ukakasi.
 
Mwenzako kazungumza vile kisiasa, anataka dunia ifaham ndani ya 4years kafukuza makamishna wanne, alafu anakatabia cha kujiona yeye yupo sahihi kwa kila jambo (anayempinga sio mzalendo)
 
Katika utafiti wangu nimegundua kuwa watu wanaendeshwa na mihemuko ya kiitikadi, jambo linalowafanya kushindwa hata kuelewa ambacho amekisema mtu fulani badala yake kudhihaki na matusi. nimesikiliza kwa makini kauli ya Mhe Rais hakuna mahala alipo muagiza M7 kuwafukuza maafisa wake wa URA bali alitoa kama ushauri tena akisema "mzee sikufundishi kazi" lakini mnaojua kutafsiri mnageuza kauli. Huo ni ni unafiki na uchonganishi
Ushauri ungebaki private ingependeza zaidi kuliko kuuleta public, unafikiri katuma picha gani kwa raia wa uganda dhidi ya rais wao? Kwamba M7 dhaifu awajibishi watumishi wazembe au?
 
Hivi inakuwaje mtu mzima kabisa unatoa maagizo kwa Rais wa nchi nyingine, tena maagizo yenyewe ni ya hovyo kabisa, naomba Rais museveni ampuuze tu
 
  • Thanks
Reactions: prs
Mambo yanayohusu nchi ya mwenzako lazima uwe mpole na kutumia busara zaidi... sababu hata yeye hapangiwi...



Cc: mahondaw
Tena mambo yenyewe ni yanayohusu rasilimali za nchi na maslahi yao,yani wafukuze watu ili waharakishe ujenzi wa bomba?wanahaki ya kusitisha na mradi wenyewe wa bomba kabisa kama maslahi yao hayajafikiwa.
 
Ushauri ungebaki private ingependeza zaidi kuliko kuuleta public, unafikiri katuma picha gani kwa raia wa uganda dhidi ya rais wao? Kwamba M7 dhaifu awajibishi watumishi wazembe au?
kama watamsikiliza kwa makini na kumuelewa hawawezi kuwa na dhana hiyo, MAANA YA JAMBO INATOKANA NA MTOA NENO NA SI MPOKEA NENO,
 
Boss G Sam Ushauri wangu: Ningependa sana Mambo ya Kitaifa, Tuwe kitu kimoja, Mambo ya Ndani, ndio Tumchane Mh. Rais. Maana hilo Bomba likifanikiwa kujengwa, anayefaidika ni Wananchi na Taifa na si Mh. Rais iwapo ... Tushajua ... Mapungufu ya Mh. Rais.

Ukitaka uwe na umoja wa kitaifa tenda haki. Unapoona mataifa mengine yana machafuko sio kwamba hawataki umoja wa kitaifa, bali ni kukosekana kwa haki kwa baadhi ya makundi. Unapoungana na mtu anayekukandamiza kwa sababu za itikadi hawezi kuona hatari ya kukundamiza, namna pekee ni kutokuunga naye kwa lolote ili ajirekebishe.
 
Back
Top Bottom