Hasa laaana za mzee Wariyoba zinamla pole pole.Kama kuna Mtu ambaye ndiyo ameleta Nuksi nzima katika Kikosi cha Taifa Stars na Maandalizi yake Kiujumla basi ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda. Makonda anapaswa Kujiuliza ni kwanini kila Jambo analolisimamia tena huku akijigamba kabisa huwa linakuja Kutofanikiwa baadae na anazidi tu Kudharaulika huku walio nae karibu wakiwa wanaendelea tu Kumsanifu. Namshauri Makonda awatafute upesi wale Watu wote aliowakosea tokea alipoteuliwa kuwa Mjumbe wa lile Bunge la Katiba, Ukuu wake wa Wilaya ya Kinondoni na huu Ukuu wake wa Mkoa kwani yawezekana akawa amebeba Laana za Wabaya wake wengi ambazo ndizo zinamgharimu na Kumuumiza. Na hii si dalili njema Kwake na yawezekana pia akaja kuwa na mwisho mbaya japo kwa Kiburi chake na Jeuri yake ya Pesa za Kidhuluma anazozipata sasa akawa hajajigundua.