MANG'ONYI
JF-Expert Member
- Jun 14, 2013
- 384
- 310
Mh Rais Magufuli, watanzania tumeona dhamira yako safi iliyoambatana na hatua thabiti kwa vitendo kupambana na mchwa wanaoitafuna Nchi hii bila huruma.
Cha kusikitisha hadi sasa kuna mijitu bado haijasikia wala kuelewa kile unachokisimamia cha kuitafuta Tanzania yenye Neema.
Leo nakutajia mchwa mbaya kabisa ndani ya serikali yako ambaye ni Mhandisi, mwizi anayevaa suti na tai bwana Sprian Luhemeja Afisa mtendaji mkuu wa DAWASCO.
Hili jipu lina kiburi, dharau na utendaji mbovu lakini linajilinda kwa kutoa rushwa ili liendelee kubaki madarakani pamoja na kuutaka ukatibu mkuu ama uwaziri kwa kijipendekeza kwa wakubwa au hata kuununua. Kuhani wake ni Prof. Maghembe.
Turudi kwenye ufisadi wake:
Kuna kazi pale Serengeti ameipa kampuni ya mtindasi ambaye ni mtu wake wa karibu kwa gharama ya Tshs milioni 420 ambazo hizi fedha walizigawana yeye Luhemeja na Mtindasi. Ikumbukwe mtindasi pia ni mfanyakazi wa DAWASCO hivyo mchakato wa zabuni umekiukwa.
Katapila za Dawasco ni nzima lakini Shirika linakodisha mengine kutoka nje kwa laki Nane (8) na linafanya kazi kwa masaa mawili au matatu ili hela iendelee kuingia kw Luhemeja.
Amekomba mamilioni ya fedha za SACCOSS ya wafanyakazi ambayo kila mfanyakazi anachangia 60 000/- kila mwezi.
Pesa za OPEX zikitumwa vituoni kuna kijana anaitwa Costa anaenda kukusanya 3ml/- na mkurugenzi anapelekewa Milioni moja.
Kuna mtu anaitwa konyaki ambaye ni mkurugenzi wa rasilimali watu (CHRO) amefanya ufisadi wa shilingi milioni 20 akiwa mamlaka ya maji moshi na amekuwa hafiki kazini muda mwingi anafanya mambo yake nje ya dar lakini mkurugenzi Luhemeja amelifumbia macho. Huyu Konyaki baada ya kushirikiana na Luhemeja kupiga sana hela wakiwa wote moshi na ishu kubumburuka luhemeja alipopata utendaji mkuu DAwasco akamfanyia mpango akamhamishia dar kuja kumficha.
Luhemeja Analea wafanyakazi ambao wanafahamika wazi ni wezi wa maji kwa sababu wanagawana kinachopatikana mfano Costa ni mwizi wa maji na baadhi ya kesi zake ziko mahakamani lakini ameajiriwa kwa utashi wa Boss Luhemeja ili kukamilisha ishu zake za Migao ya fedha.
Hii ni part one. Zingine zaja...
Mheshmiwa Rais, Tunakuomba uichunguze DAWASCO tumechoka kwa kweli. Anzia kwa Luhemeja uje kwa waziri wa maji na bodi ya DAWASCO kuna uchafu wa kutisha. Serikali inaibiwa mno.
Hapa kumejaa chuki tu, Luhemeja ni mchapa kazi na ana maono ya wapi shirika linatakiwa kwenda, kaulize moshi ameacha legacy, kama ameziba mirija ya wizi wenu poleni.