Rais Magufuli, tunaomba Umteue Saada Mkuya Salum kwa Manufaa Makubwa ya Taifa

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,895
Naomba nianze kwa kusema kwamba Nchi ya Tanzania haina Udini.

images (9).jpeg



Salaam wakuu,

Rais Magufuli, katika teuzi zako usimsahau jicho la Vijana Saada Mkuya Salum Mwasisi wa Uchumi wa kati

Saada Mkuya Salum aliwahi kuwa Waziri wa fedha. Kuna kipindi alikuwa anahutubia Bunge akasema atahakikisha kufikia 2020 Tanzania inafika Uchumi wa kati. Ndo maana aliposikia Tanzania imetajwa kwenye orodha ya Nchi ya Uchumi wa kati, machozi ya furaha yalimtoka sababu malengo yake yametimia.

Ukiacha Mambo ya Siasa, Saada ni Hazina ya Taifa. Hawa wakina Mpango wanaenda kusitaafu na akili imeshaanza kuzeheka. Hivyo Vijana wangetamani kuona Saada anakuzwa kwa vizazi vijavyo akasaidie taifa.

Ni mfano kwa Wakina Mama. Wanawake waanze kusoma Masomo ya Sayansi na Hesabu wawe kama Saada. Hao Wazee Wizara ya fedha wamwchoka, wapo analogy. Tuleteeni huyu binti Shupavu.

Ni mnyenyekevu, hana doa japo aliongoza Idara nyeti ya fedha. Hajadokoa hata tone.

Tunaamini Rais Magufuli upo kwaajili ya watanzania wote na una hofu ya Mungu. Tunaomba itusaidie kutuletea Saada Mukuya ili Watanzania tufaidi matunda ya Kizazi chetu. Wapo wengi ila Saada ana Uzoefu na Mambo ya fedha.


Huyu Mama ndo aliweka Mkakati wa Wakala ya Serikali Mtandao. Zamani fedha zilikuwa zinakaa na Wahasibu, sasa hivi unalipa online au banki kitu ambacho kiliondoa Ufisadi.

Ni kufuatia mapengo kadhaa katika CV yake Iliyopo kwenye tovuti ya Bunge la Tanzania.

Waziri Mkuya kuna kipindi aliongea na Mwandishi wa Mtanzania na kudema elimu yake wala haina mashaka, kwani alisoma kidato cha tano na sita katika Shule ya Sekondari Lumumba mjini Zanzibar.

Baada ya hapo, alijiunga na masomo ya diploma ya Biashara katika Chuo cha Stamford cha Malaysia, ambapo pia alichukua diploma nyingine ya biashara nchini Uingereza.

Alisema mbali na masomo hayo, pia amesoma shahada ya pili ya biashara katika Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) na kuhitimu mwaka 2009.

“Nimehitimu Shahada ya Uzamili ya Utawala na Biashara (MBA) ya Chuo Kikuu cha WATT kilichopo Edinburgh, Scotland.

“Kwa sasa nachukua Shahada ya Uzamivu (PhD) ya Utawala wa Biashara Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, tawi la Dar es Salaam,” alisema Mkuya mwaka 2014.

Alipokuwa Waziri wa Fedha alifanya mambo Makubwa. Huyu si mtu wa kubezwa au kumuacha achukuliwe na Wakenya kwa Mambo ya Ushauri wa Kifedha. Hata sisi anatufaa.

04 May 2012 Rais Mstaafu Jakaya Kikwete kwa kuona Umuhimu wake katika kuinua uchumi, alimteua Saada Mkuya Salum kuwa mbunge na baadaye akampa Uwaziri.

Huyu Mtoto bado anahitajika. Kumbuka ndiye alifanya mpango wa kuhakikisha fedha zinapatikana za kumuingiza Pombe Magufuli Ikulu. Bila kujali nchi ilikuwa kwenye Ukata.

Tujikumbushe


images (8).jpeg
 
Jiwe huyu huyu? Hapo umeshaharibu jiwe hapangiwi kama unaweza nenda kanywe naye chai basi.
 
Uwezo wake ni wakawaida sana

Aliupata uwaziri kibahati baada ya kifo cha Mgimwa

Pia ni kati ya watu hatari waliopenya na kushika wizara nyeti kabisa
 
Naomba nianze kwa kusema kwamba Nchi ya Tanzania haina Udini.View attachment 1630231

Salaam wakuu,

Rais Magufuli, katika teuzi zako usimsahau jicho la Vijana Saada Mkuya Salum Mwasisi wa Uchumi wa kati

Saada Mkuya Salum aliwahi kuwa Waziri wa fedha. Kuna kipindi alikuwa anahutubia Bunge akasema atahakikisha kufikia 2020 Tanzania inafika Uchumi wa kati. Ndo maana aliposikia Tanzania imetajwa kwenye orodha ya Nchi ya Uchumi wa kati, machozi ya furaha yalimtoka sababu malengo yake yametimia.

Ukiacha Mambo ya Siasa, Saada ni Hazina ya Taifa. Hawa wakina Mpango wanaenda kusitaafu na akili imeshaanza kuzeheka. Hivyo Vijana wangetamani kuona Saada anakuzwa kwa vizazi vijavyo akasaidie taifa.

Ni mfano kwa Wakina Mama. Wanawake waanze kusoma Masomo ya Sayansi na Hesabu wawe kama Saada. Hao Wazee Wizara ya fedha wamwchoka, wapo analogy. Tuleteeni huyu binti Shupavu.

Ni mnyenyekevu, hana doa japo aliongoza Idara nyeti ya fedha. Hajadokoa hata tone.

Tunaamini Rais Magufuli upo kwaajili ya watanzania wote na una hofu ya Mungu. Tunaomba itusaidie kutuletea Saada Mukuya ili Watanzania tufaidi matunda ya Kizazi chetu. Wapo wengi ila Saada ana Uzoefu na Mambo ya fedha.


Huyu Mama ndo aliweka Mkakati wa Wakala ya Serikali Mtandao. Zamani fedha zilikuwa zinakaa na Wahasibu, sasa hivi unalipa online au banki kitu ambacho kiliondoa Ufisadi.

Ni kufuatia mapengo kadhaa katika CV yake Iliyopo kwenye tovuti ya Bunge la Tanzania.

Waziri Mkuya kuna kipindi aliongea na Mwandishi wa Mtanzania na kudema elimu yake wala haina mashaka, kwani alisoma kidato cha tano na sita katika Shule ya Sekondari Lumumba mjini Zanzibar.

Baada ya hapo, alijiunga na masomo ya diploma ya Biashara katika Chuo cha Stamford cha Malaysia, ambapo pia alichukua diploma nyingine ya biashara nchini Uingereza.

Alisema mbali na masomo hayo, pia amesoma shahada ya pili ya biashara katika Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) na kuhitimu mwaka 2009.

“Nimehitimu Shahada ya Uzamili ya Utawala na Biashara (MBA) ya Chuo Kikuu cha WATT kilichopo Edinburgh, Scotland.

“Kwa sasa nachukua Shahada ya Uzamivu (PhD) ya Utawala wa Biashara Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, tawi la Dar es Salaam,” alisema Mkuya mwaka 2014.

Alipokuwa Waziri wa Fedha alifanya mambo Makubwa. Huyu si mtu wa kubezwa au kumuacha achukuliwe na Wakenya kwa Mambo ya Ushauri wa Kifedha. Hata sisi anatufaa.

04 May 2012 Rais Mstaafu Jakaya Kikwete kwa kuona Umuhimu wake katika kuinua uchumi, alimteua Saada Mkuya Salum kuwa mbunge na baadaye akampa Uwaziri.

Huyu Mtoto bado anahitajika.

Tujikumbushe


View attachment 1630232

Kama we mwanae au mpambe ujue we ni nuksi ushamwalibia Rais hapangiwi kama alikuwa kwenye list kesha chomolewa kwa upambe wako nuksi aendelee kutumikia wapiga kura wa jimbo lake
 
Back
Top Bottom