Rais Magufuli: Tetemeko halijaletwa na Serikali, watu wafanye kazi

Mfuko wa TAIFA wa maafa hauna senti yaani uhuru Na Museveni wanarespond haraka kuliko serikali.
Unaahirisha ziara alafu unajifungia Ikulu wiki nzima ......sibora angeenda Zambia akamuombe waachee kupitisha copper Durban Wakati Tazara iPo..
Rais akienda mahala Ni Tofauti Na Waziri Mkuu Au Makamu ...rais Ni rais na marais wanaongea Na marais mambo ya kuongea Na mtu ambaye Hana uamuzi wa mwisho hawapendi
Hahaha uwii I hate ccm with all my strength f*****
 
hoja nyingine ni kuwa aliomba japo robo ya roho ya JK na SHEIN kwa nyakati tofauti je yeye ana roho ya aina gani??siku zote mwanaume unavyoonekana ukiwa na wenzio maneno na matendo yako vinakisi mbali sana ...

well, hata hilo suala la upole wa Shein Magufuli did not mean what he said. Kasema anaomba japo robo ya roho ya Shein halafu hapo hapo akamkandia kwamba ni mpole sana inabidi akaze ili nchi ya Zanzibar ipige hatua. Which means hafagilii upole.
Okay, sasa kwa nini anajifanya kusema anaomba awe japo na robo ya roho ya Shein? Sio unafiki huo?

He doesn't mean what he says, anajifanya kusema "...mkweli ni mpenzi wa Mungu." Anachofanya ni psychological projection, kama ambavyo wana saikolojia wanasema unaweza kukuta mtu shoga akiwa hadharani analaani ushoga. Yani anajitetea kabla hajashambuliwa kwa sababu anajua ana madhambi, Rais anajijua anasema uongo kwa hiyo anatanguliza "mpenzi wa Mungu" bull crap.

Kwanza from a protocol standpoint amemkosea heshima Shein kwa kum potray mbele ya Wazanzibari kwamba anawalostisha watu wake. Especially baada ya kuutetea sana Muungano that day, kiasi cha kusema mtu yeyote anaemsumbua huko Zanzibar amwambie yeye atammaliza within five minutes. Okay, kama unautetea Muungano namna hiyo kwa nini huheshimu himaya ya Rais wa Zanzibar unam rubbish mbele za watu wake namna ile?

Ndio maana kama umefuatilia, wiki hii iliyopita Shein amerudi majukwaani Pemba ku clean up the mess ya Magufuli. Magufuli alimshambulia viciously mgombea ambae Pemba nzima wanaamini alishinda uchaguzi wa Rais, amemsifia Jecha ambae watu wote kule wanajua ndio alikuwa the symbol of the stolen vote, amempigia chapuo Waziri Mbarawa ambae alishindwa uchaguzi wa ubunge, amewananga Wazanzibar kwamba hawajui chema na kibaya kwa kumkataa Waziri ambae yeye amempa wizara tatu na ubunge wa bure. Hotuba zake ni fully studded with uchochezi. Shein amerudi majukwaani kusahaulisha kauli za Magu.

Magufuli ni kama Donald Trump, he does not have the temperament befitting a president, Rais mwenyewe ndio mchochezi wa kwanza.
 
Kwa kweli sina milioni saba ya kulipa... Ila Mkuu ana maneno mazito! Anasema waathirika wasikae tu huko wanangoja hela za serikali kwa sbb wanasikia zimechangwa,waanze kujisaidia kwanza wao na serikali itawasaidia pale waliposhindwa.

Mkuu anasema mtu ukuta umedondoka, anataka asubiri serikali ndio imtengenezee! Watu wajue tetemeko ni janga la asili halijaletwa na CCM. Waanze kwa kujenga wenyewe kuta zilizodondoka sio wasubiri serikali, sababu maisha yanendelea na watu wanatakiwa wafanye kazi kwa kujenga nyumba zao na sio kila kitu serikali itafanya.

Na wale wanasiasa wanaotaka kutumia janga hili kujinufaisha kisiasa mkuu anasema waache mara moja.

Na kasema wote wanaotumia janga hili kukusanya misaada kwa njia ya kitapeli, basi wakamatwe mara moja.

=======

Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amepokea taarifa ya maafa yaliyosababishwa na tetemoko la ardhi lililotokea katika Mkoa wa Kagera na mikoa jirani ya Mwanza, Geita na Mara kutoka kwa Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, Ikulu DSM.

Magufuli%20tetemeko1.JPG

Rais Magufuli akipokea taarifa pamoja na misaada iliyochangwa na nchi jirani

Pamoja na kupokea taarifa hiyo Rais Magufuli amepokea mchango wa fedha taslimu kiasi cha Dola za Kimarekani laki mbili (USD-200,000/-) sawa na takribani Shilingi za Kitanzania Milioni Mia nne na therathini na saba (Tshs-437,000,000/-) kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni na pia amepokea taarifa ya mchango wa mabati, blanketi na magodoro vyenye thamani ya Shilingi za Kitanzania milioni 115 kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta kwa ajili ya kuwasaidia waathirika wa tetemeko la ardhi Mkoani Kagera.

Katika taarifa yake Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa amesema tetemeko hilo limesababisha vifo vya watu 17, majeruhi 440, nyumba 2063 zimeanguka, nyumba 14,081 zipo katika hali hatarishi na nyumba 9,471 zimepata uharibifu mdogo, huku watu 126,315 wakihitaji misaada mbalimbali.

Mhe. Waziri Mkuu ameongeza kuwa Serikali imechukua hatua mbalimbali zikiwemo kupeleka chakula, huduma za matibabu na hifadhi za dharura kwa waathirika na pia inaratibu ukusanyaji wa michango kutoka sehemu mbalimbali ambapo mpaka sasa kiasi cha Shilingi za Kitanzania Bilioni tatu nukta sita (Tshs Bilioni 3.6) zimepatikana.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa ya maafa na michango kwa ajili ya waathirika wa maafa hayo, Rais Magufuli amewashukuru wote waliojitoa kusaidia waathirika wakiwemo Marais Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda, Mhe. Uhuru Kenyatta wa Kenya na Paul Kagame wa Rwanda ambao wamempigia simu za kumpa pole na tayari wametoa misaada yao, na pia nchi mbalimbali, mashirika, wafanyabiashara, watumishi wa umma na watu binafsi na amesema michango hiyo ina umuhimu mkubwa katika kukabiliana na athari za maafa haya.

Dkt. Magufuli ametoa wito kwa Watanzania na wote walioguswa na maafa haya kuendelea kutoa misaada kwa waathirika kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera, huku akionya na kuvitaka vyombo vya dola kuwafuatilia watu wanaotaka kutumia maafa haya kukusanya michango kwa lengo la kujinufaisha.

Rais Magufuli amebainisha kuwa Serikali itahakikisha inarekebisha miundombinu iliyoharibika zikiwemo shule, vituo vya matibabu, barabara na huduma nyingine za kijamii na pia ametaka wananchi waliokumbwa na madhara ya tetemeko hususani nyumba zilizobomoka, wajipange kurekebisha nyumba zao kwa kuwa Serikali pekee yake haitaweza kujenga nyumba zote zilizobomoka.

Aidha, Rais Magufuli amewasihi Watanzania kuwapuuza watu wanaotaka kutumia maafa haya kueneza uchonganishi na chuki dhidi ya Serikali na ameweka wazi kuwa mpaka sasa hakuna teknolojia ya kutabiri kutokea kwa tetemeko la ardhi na kwamba tetemeko hili halikuletwa na Serikali.

Dkt. Magufuli amesema hata mataifa makubwa yenye maendeleo makubwa ya uchumi na teknolojia yanakumbwa na tetemeko la ardhi na kusababisha vifo vya idadi kubwa ya wananchi na uharibifu mkubwa wa mali.

"Nilikuwa najaribu kuangalia kwa mfano nchi kama China kwenye mwaka 2014 watu 617 walipoteza maisha, Mwaka 2013 walipoteza watu 193, Mwaka 2010 walipoteza watu 2,998 Mwaka 2008 China ilipoteza watu 98,712.

Ukijaribu kuangalia Japan, nchi ambayo imeendelea na ina utaalamu wa hali ya juu sana, kwenye mwaka 2016 tarehe 14 mwezi wa nne ilipoteza watu 6, baada ya siku mbili tarehe 16 mwezi wa nne 2016 tetemeko likatokea tena na likaua watu 35, mwaka 2012 likaua watu 3, mwaka 2011 likaua watu 15,904 mwaka 2008 likaua watu 12, mwaka 2007 likaua watu 11, mwaka 2004 likaua watu 40, mwaka 1923 liliua watu 142,800 na hiyo ni Japan. Amesisitiza Rais Magufuli.

Shughuli ya kupokea taarifa ya Waziri Mkuu na michango kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi lililotokea Mkoani Kagera na Mikoa jirani imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Augustine Mahiga, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt Suzan Kolimba, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Balozi wa Uganda nchini Tanzania Mhe. Dorothy Hyuha na Naibu Balozi wa Kenya nchini Tanzania Mhe. Boniface Muhia.


Chanzo: IPP Media

Huu ni ufinyu wa mawazo yake, kila mtu ana mapungufu ila huyu amepungukiwa zaidi, anadhani wanaotoa mpaka dola 400, 000 wana hela sana ama? Utu na ubinadamu kwanza! bwana.... Anaboa huyu jamaa sasa.
 
Hatimaye mkuu kazungumza japo kwa kuchelewa sana. Ila naomba niulize: hivi inawezekana kukawa na watu wanaoamini kuwa "tetemeko limeletwa na serikali" mpaka mkuu atake wananchi wafahamishwe kuhusu hilo?

Hahhahaha kuna wabongo wengine vichwa maji kweli ....kama vile kupatwa najua,huko mbeya kuna jamaa kajua serikali yake imeamua kupatwa najua mwaka huu 2016 ufanyikie mbeya na akawaanaponheza uongozi wa CCM .sembuse tukioo kama ilo.
 
Hatimaye mkuu kazungumza japo kwa kuchelewa sana. Ila naomba niulize: hivi inawezekana kukawa na watu wanaoamini kuwa "tetemeko limeletwa na serikali" mpaka mkuu atake wananchi wafahamishwe kuhusu hilo?
Inawezekana kabisa kuna watu inabidi waelimishwe kuhusu hilo. Si unajua mambo ya shule za kata yalivyo na matatizo? Kama mtu anaweza kuishukuru serikali kwa kuuchagua Mkoa wa Mbeya kuwa ndiyo sehemu ya kupatwa na Jua, itashindikanaje watu wa aina hiyo kuamini kuwa Serikali hiyo hiyo imechagua Bukoba kuwa sehemu ya kupatwa na tetemeko? Halafu hapo unaambiwa elimu imepanda kiwango. Je ilipokuwa chini hali ilikuwaje?
 
Anasema rafiki Wa kweli ni anayekusaidia wakati Wa shida.. Amewashukuru Kenyatta na Museven nadhani alikuwa akituma ujumbe kwa Kagame.. Haijakaa vizuri sana hiyo.. Nadhani hamjui teacher Wa visasi atakuja kujuta kwanini Safari ya kwanza alianzia kule.

Mnyarwanda zake husema it's a matter of time tu.. Kichapo lazima ule
 
Hotuba imerudiwa jpili channel 10. I am bit disappointed na miss-interpretation ya hotuba ya mkulu kwenye huu uzi. Kwa mwendo huu JF iaanza kua a mere political propaganda platform na sio great thinkers platform kama ilivyokua. Wengi tunakuja JF kupata breaking/update news bila kijali political ideology ya mtu. Kwa walioisikia hotuba yote ya mkulu, mengi kazungumza, but is just not right kutumia sentensi moja negatively katika 30mins speech. Moderators tunaomba kwa credibility ya JF habari iwe inakua scrutinised kabla haijawa posted.
 
Foreman in da building....Kama baba wakati mwingine ukali huifanya familia yake ikae vizuri japo si kwa zaidi ya asilimia15..
 
duuuh...kazi ipo..ukiangalia takwimu nyumba zilizoanguka na zilizo hatarishi ni zaidi ya 16,000.mpaka sasa zimepatikana bn3.5..ukisema ujenge nyumba kwa milion 20 kila moja utajenga nyumba 175 tu..bado kuna tatizo kubwa.
 
Wakati Mh Rais anapokea taarifa ya maafa ya tetemeko kutoka kwa Waziri Mkuu alisema yafuatayo:
- Waanga wa tetemeko waelezwe ukweli kuwa tetemeko halikusababishwa na Serikali wala CCM...Hivyo waache kukaa na kutegemea msaada wa kila kitu kutoka kwa serikali ni wakti sasa wajipange na kuanza kufanyaaa kazii. Hapa hakuna tatizo maana lazima watu wajisadie pale wanapoweza huku wakisubiri msaada mkubwa kutoka serikalini.
-Akaendelea kusema tetemeko hili lisitumike kama sehemu ya wana siasa kwenda kujitafutia umaarufu..Na hapa akasema kwa mafumbo kidogo kuwa kuna Kiongozi wa Wa chama kimoja cha Siasa ameenda huko akazunguka nyumba zoooote mwishowe hakutoa hata kitu..Na akaendelea kusema wanachi hawataki maneno matupu wanataka msaada. Hapa ndo nilipoona tatizo kidogo maana Kiongozi wa chama cha siasa alienda kule nadhani anajulikana ni nani na naamini watu wanapofikwa na matatizo hata kwenda kuwapa pole ya mdomo tu inawafariji mno kuliko hata kuwapelekea vitu.. Nikakaa nikajiuliza sana Mkuu wakati anazungumza kwa mafumbo marahisi hivyo ni kweli anadhani wanachi hawaelewi ni nani anamzunguzia? Nimefananisha dongo hilo na lile alilosema akiongea na NHC kuwa yeyote ambaye hajalipa kodi ya nyumba mtoeni nje na vitu vyake kama mlivyofanya kwa yule jamaa...Itakuwa hivi mpaka lini sasa?
 
Back
Top Bottom