sacred wall
JF-Expert Member
- Aug 9, 2017
- 804
- 1,318
Bwana Magufuli, kama kweli wazungu hao unaowaita mabeberu wakitaka kukuondoa/kutuondoa kweli wanashindwa? Kwahiyo zuia na dawa zote za MSD maana ni mali za mabeberu! ARVs, TB meds, simu yako, computer yako, etc etc.Hayo ni maagizo aliyoyatoa leo huko Dodoma ndani ya uwanja wa Jamuhuri Dodoma kwenye mkutano wa CWT.
Asema marufuku kwa vikundi vya watu kugawa barakao na ukikutwa ukamatwe ujibu ulikozitoa pamoja na hayo kama vipi shona ya kwako na unaweza chukua sidiria ya upande mmoja na kuifanya barakoa
Nukuu
Ukitaka kuvaa barakoa kashone yako, mbona ni rahisi tu, barakoa mbona imekaa kama titi moja la Mtu mmoja hivi limekatwa upande mmoja, weka huku kama... aaah samahani Mh.Waziri nimesema hapa, nilikuwa nachomekea tu kidogo”
Juzi nilikuwa nasikiliza taarifa ya habari kuna group linaitwa Magufuli Forum wala silijui, ila sishangai Mtu kujiita Magufuli hata akijiita fisi ni hiyari yake, lakini walikuwa wanagawa barakoa wala hazijulikani zinatoka wapi, tutaumia kwa kukosa maarifa
Njia nyingine ambayo inaweza kutumika ni kuletewa vifaa vya corona vyenye corona, anapokuletea Mtu barakoa hujui ameitoa wapi kataa, mwambie kavae wewe na Mke wako na Watoto wako nyumbani, tutaumizwa
Mfano kama target ni wewe si watafanya kama ya Qssem Soleiman wa Iran? na dunia haitajua artillery ilitokea wapi! Hivyo usiwe na hofu hata kidogo na hawa watu. Ni development partners!