Rais Magufuli kuzindua miradi mitano Songwe

MIMI BABA YENU

JF-Expert Member
Mar 1, 2019
295
679
1570017044952.png

Jumla ya miradi mitano kuzinduliwa na kuwekewa mawe ya Msingi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli katika ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Songwe ambayo inatarajiwa kauanza oktoba nne mpaka oktoba tano mwaka huu.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Brigedia Jeneral Nicodemas Mwangela akiongea na vyombo vya habari alisema katika ziara hiyo ambayo ni ya kwanza toka aingie madarakani mwaka (2015) kuwa Rais atatembelea miradi mbalimbali kuanzia oktaba nne katika wilaya za Mbozi na Momba ambapo mradi wa maji, barabara,ujenzi wa hospitali ya mji wa Tunduma, kiwanda cha kahawa na mradi wa kutoa huduma kwa pamoja mpakani mwa Tanzania (Tunduma) na Zmbia (Nakonde).

Alisema akiwa wilayani Mbozi oktoba nne (4) mwaka huu Rais atatembelea na kuweka jiwe la Msingi katika mradi wa maji wa Mantengu Vwawa ambao unategemewa kutatua changamoto ya maji katika mji wa Vwawa na kuzindua kiwanda cha Kahawa cha GDM Mlowo.

Oktoba tano (5) Rais Dk John Magufuli akiwa na Rais wa Zambia Edgar Chagwa Lungu watazindua kituo cha kutoa huduma kwa pamoja mpakani mwa Tanzania (Tunduma) wilayani Momba na Zambia Nakonde.

Mwangela alisema pia Rais wa Jamhuri ya Muungano atamalizia ziara yake kwa kuweka jiwe la msingi katika Mradi wa ujenzi hospital ya mji wa Tunduma na katika Mradi wa wa ujenzi wa Barabara ya Mpemba -Isongole Wilayani Momba.

Aidha Mwangela aliwataka wananchi wote mkoani Songwe kujitokeza kwa wingi kumlaki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ndiye anayetekeleza miradi yote ya maendeleo kwa vitendo ikiwa ni pamoja na kuuanzisha mkoa wa Songwe.
 
Masahihisho,barabara inayowekewa jiwe la msingi ni ya Mpemba[Momba]-Isongole[Ileje]. MWANDISHI AMEPOTOSHA KWA KUSEMA MPEMBA-ISONGOLE WILAYANI MOMBA.
HE/SHE isa big lie,
 
Mh Rais nakujua wewe ni mzee wa maamuzi nakuomba utaona inafaa toa amri mara moja vifanyike vifuatavyo hapo Tunduma

1. Ijengwe bandari kavu kubwa.
itakayopitiwa na reli ya Tazara. Mizigo
yote ya Congo DRC, Zambia na Malawi
destination iwe hapo na clearing.
zifanyike hapo, Dar port ibakie kuwa.
transit port tu.
 
Mh Rais nakujua wewe ni mzee wa maamuzi nakuomba utaona inafaa toa amri mara moja vifanyike vifuatavyo hapo Tunduma

1. Ijengwe bandari kavu kubwa.
itakayopitiwa na reli ya Tazara. Mizigo
yote ya Congo DRC, Zambia na Malawi
destination iwe hapo na clearing.
zifanyike hapo, Dar port ibakie kuwa.
transit port tu.
Inajengwa bandari kavu kubwa Kwala nafikiri ICDs zote Dar ndio itakua bye bye, hata Tunduma ipo kwenye plan.
 
Bila Kubadili Maisha ya Raia ili yawe na unafuu ni bure kabisa! Endeleeni Kusifia Wazee wa Kusifu.
 
Bila Kubadili Maisha ya Raia ili yawe na unafuu ni bure kabisa! Endeleeni Kusifia Wazee wa Kusifu.
Maisha ya raia mpaka sasa ni safi ndiyo maana tunafanya kazi kwa bidii ifikapo 2025 tuwe level ya kati! Wale wenye self-hatred hawaoni hivyo! Akili zao zinawarudisha nyuma tu. Watu sasa wana umeme, maji, life expectant imeongezeka bado watu hawaoni hayo! Wanajaribu kubeza serikali kwa kutumia vigezo vya masikini ambao wapo kila nchi! Hakuna nchi duniani isiyokuwa na hao. Ila wewe nakuelewa sana - maana unamkubali Raisi Magufuli na utendaji wake na matokeo ya kazi zake, ila hutaki kusifia sasa hivi asije akapunguza kasi. Lakini watu wote tunaona maendeleo.
 
View attachment 1221596
Jumla ya miradi mitano kuzinduliwa na kuwekewa mawe ya Msingi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli katika ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Songwe ambayo inatarajiwa kauanza oktoba nne mpaka oktoba tano mwaka huu.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Brigedia Jeneral Nicodemas Mwangela akiongea na vyombo vya habari alisema katika ziara hiyo ambayo ni ya kwanza toka aingie madarakani mwaka (2015) kuwa Rais atatembelea miradi mbalimbali kuanzia oktaba nne katika wilaya za Mbozi na Momba ambapo mradi wa maji, barabara,ujenzi wa hospitali ya mji wa Tunduma, kiwanda cha kahawa na mradi wa kutoa huduma kwa pamoja mpakani mwa Tanzania (Tunduma) na Zmbia (Nakonde).

Alisema akiwa wilayani Mbozi oktoba nne (4) mwaka huu Rais atatembelea na kuweka jiwe la Msingi katika mradi wa maji wa Mantengu Vwawa ambao unategemewa kutatua changamoto ya maji katika mji wa Vwawa na kuzindua kiwanda cha Kahawa cha GDM Mlowo.

Oktoba tano (5) Rais Dk John Magufuli akiwa na Rais wa Zambia Edgar Chagwa Lungu watazindua kituo cha kutoa huduma kwa pamoja mpakani mwa Tanzania (Tunduma) wilayani Momba na Zambia Nakonde.

Mwangela alisema pia Rais wa Jamhuri ya Muungano atamalizia ziara yake kwa kuweka jiwe la msingi katika Mradi wa ujenzi hospital ya mji wa Tunduma na katika Mradi wa wa ujenzi wa Barabara ya Mpemba -Isongole Wilayani Momba.

Aidha Mwangela aliwataka wananchi wote mkoani Songwe kujitokeza kwa wingi kumlaki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ndiye anayetekeleza miradi yote ya maendeleo kwa vitendo ikiwa ni pamoja na kuuanzisha mkoa wa Songwe.


.....Aidha Mwangela aliwataka wananchi wote mkoani Songwe kujitokeza kwa wingi kumlaki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ndiye anayetekeleza miradi yote ya maendeleo kwa vitendo ikiwa ni pamoja na kuuanzisha mkoa wa Songwe. Awaache wananchi wafanye kazi, watakula wapi siku hiyo na bada ya hapo? Piga kazi Wananchi... au siyo bwana?
 
Back
Top Bottom