Rais Magufuli; Kuongoza kizazi hiki lazima uwe dikteta tu, bila hivyo nchi itakushinda

Mtoa mada nakupongeza kwa dhati kabisa, kwani kwa asilimia kubwa upo sahihi kabisa. Nchi hii watu wengi wanataka mambo makubwa na ya kifahari huku wakiwa wamekaa tu bila hata kujishughulisha kwa namna yoyote ile. Ni watu wenye kuilalamikia serikali kwa kila jambo bila aibu. Ni kizazi kilichokosa uvumilivu na kisichojituma. Ili kubadili hali na mtazamo wa watu wa nchi hii ili wawe wachapakazi ilikuwa ni kumweka madarakani RAIS ambaye ni KOMANDOO, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na viongozi wote wa ngazi mbalimbali wawe ni wanajeshi na nchi iongozwe kijeshi japo kwa miaka michache tu. Kwa kufanya hivyo bila shaka nchi ingeweza kupiga hatua za maendeleo siku hadi siku. MHESHIMIWA RAIS MAGUFULI, MUNGU AKUONGOZE, AKULINDE, AKUTIE NGUVU, AKUPE HEKIMA, BUSARA NA UJASIRI ili uweze kuliokoa taifa hili katika janga la umaskini, uvivu, ufisadi, wizi, uzembe, ubinafsi nk.
Mwaka huu lazima wasome namba kwa herufi kubwa.
 
Kama mkatoliki na unatoka kanda ya ziwa then sitokushangaa mleta mada! Yangu ni hayo tu
 
Nani wa kulaumiwa?kizazi kipya kimezaliwa na kulelewa na kizazi cha akina Nyerere,Kizazi cha Abed Amani Karume,Mwinyi,Mkapa,na Kikwete.Mtoto umleavyo ndio akuavyo.Uholazi crime rate inapungua wanafunga magereza lakini Tanzania ndio tunapanua maabusi na jela.Acha kupotosha umma.
 
Naililia nchi yangu Tanzania , kila nikitafakari machozi yananitoka nakosa majibu nabaki kujiuliza tutafika kweli? Magufuli kazi unayo sana kuongoza kizazi hiki cha ****** pole sana!

Limekuwa taifa la ajabu ajabu sana, viongozi wake (UKAWA & CCM)wamekuwa wanafiki, wazandiki, waongo hawaaminiki tena katika jamii. Wameruhusu kiburi na jeuri kuwavika kama mkufu shingoni mwao. Wana mawazo na mapenzi machafu mioyoni mwao. Kila kiongozi amekuwa muongo tu, kauli na videndo haviendani, ni wasaliti wa kwanza wa kauli zao wenyewe. Walimtangaza mchafu nchi nzima watanzania wakaamini hivyo gafla wakageuka tena kumtangaza msafi nchi nzima watanzania wakaamini tena hivyo bila kuwaoji kauli zao zile za mwanzo walizozisaliti wenyewe. Nchi imekuwa ya wanafiki sana hii. Tumekuwa jamii ya watu wa ajabu sana, tumebaki kuangalia mambo juu juu tu, na kutoa majibu mepesi kwa maswali magumu , jamii iliyojaa wapuuzi na wanafiki wengi.

Kila kukicha upendo unapungua baina ya watanzania, visasi, dhuluma, wizi, ubakaji, ufedhuli, majivuno, matabaka, ukada na umasikini unazidi kutumaliza. Ee Mungu wetu tusaidia kizazi hiki cha ******. Tumebaki kuabudu watu weupe na vitu vyao na uchafu wao wote. Tumekubali kuporwa utu wetu na kufanywa vivuli vya wazungu kiasi cha kupoteza hata utamaduni wetu.

Tumekuwa na vijana na wasomi wa hovyohovyo, kushinda kwenye mitandao kuanzia asubuh mpaka jioni kuangalia vipicha vya uchi uchi na ngono( ponograph), Kutukanana na kupost vipicha vya kipuuzi kwenye mitandao. Vinguo vyao wanavyovaa vya ajabu visizo hata maadili. Wanapenda vimagazeti na vijarida vya ngono ngono tu. Mada za mapenzi na mambo ya kipuuzi yanapewa kipaumbele kuliko hata mambo ya kitaifa. Kwenda kulima na kufanya kazi hawataki, viwanda vitakuja kwa muujiza gani?

Magufuli Rais wangu pole sana kuongoza jamii ya mashoga na wasagaji, wavuta bange na madawa ya kulevya. Mandanguro kila kona yamejaa madada poa na makaka poa wanashindania wateja na bahati mbaya wateja wao wengi ni viongozi wetu hawahawa wanaopiga marufuku mchana usiku ndio wateja wao. Taifa lawanafiki sana hili.

Makanisa na misikitini kwetu kama kimbilio na msaada kwa matatizo haya lakini huko ndiko kuna balaa. Hii ya makanisa niache nitaleta mada yake baadae maana inahitaji hekima ya Mungu sana kuijadili. Tumekuwa na uelewa finyu hata katika masuala ya msingi yanayohusu taifa letu, uelewa finyu unatufanya turubuniwe kirahisi au tuelekeze nguvu zetu kwenye mambo ambayo yanaonekana katika nyuso zetu kama ndio utatuzi wa matatizo yetu kumbe ni upuuzi.

Tuna wasomi wengi lakini wameshindwa kujiamini na kujisimamia. Wamekuwa ndio chanzo cha matatizo yetu. Wameshindwa kabisa kujitambua, kudadisi, kujituma, kuwa wabunifu, kupenda kazi, kuwa na mwenendo na maadili mema kama mfano kwa jamii. Wakulima , wafugaji na wavuvi wetu wataendelea kuwa maskini kwa sababu vijana wao baada ya kupata elimu yao ya vyeti wanakimbilia mjini, kutafuta kazi ya viyoyozi na kuvaa Suti. Hawataki kusikia tena habari ya kilimo wala ufungaji, kutwa nzima mitaondaoni na handfone masikioni. Bahati mbaya ajira zenyewe zimeota mbawa. Kizazi hiki kimekuwa kizazi cha hovyo sana kuwahi tokea.

Tanzania yangu jamani umerogwa na nani? Ngoja nishie hapo maana kadiri ninavyoandika machozi yananitoka. Magufuli Rais wangu pole sana. Naomba Mungu akujalie hekima uvumilivu na busara.

Boniphace .M. Pesambili.
MKUU UTAKOSANA NA WATU WE NGOJA WAJE WA UKANDA UCHWARA WATAKAVYOKUSHAMBULIA KWAMBA UNATAKA UKUU WA MKOA,ILA MKUU UMENIKUNA WEWE KWELI UNAITAKIA NCHI YETU MEMA,JPM WALA SI DIKTETA KAMA WALE WASIOITAKIA NCHI YETU MEMA,YEYE AMEKOSANA NA WATU KAFUNGA MIRIJAA ILIOKUA INAWANYONYA WANANCHI AMEJARIBU KURUDISHA MADILI NA UZALENDO KWA WATUMISHI NA WANANCHI KWA UJUMLA LEO HII ANAITWA DIKTETA,KAMA NI IVO BASI UDIKTETA UNAFAIDA SANA
 
Mtoa mada nakupongeza kwa dhati kabisa, kwani kwa asilimia kubwa upo sahihi kabisa. Nchi hii watu wengi wanataka mambo makubwa na ya kifahari huku wakiwa wamekaa tu bila hata kujishughulisha kwa namna yoyote ile. Ni watu wenye kuilalamikia serikali kwa kila jambo bila aibu. Ni kizazi kilichokosa uvumilivu na kisichojituma. Ili kubadili hali na mtazamo wa watu wa nchi hii ili wawe wachapakazi ilikuwa ni kumweka madarakani RAIS ambaye ni KOMANDOO, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na viongozi wote wa ngazi mbalimbali wawe ni wanajeshi na nchi iongozwe kijeshi japo kwa miaka michache tu. Kwa kufanya hivyo bila shaka nchi ingeweza kupiga hatua za maendeleo siku hadi siku. MHESHIMIWA RAIS MAGUFULI, MUNGU AKUONGOZE, AKULINDE, AKUTIE NGUVU, AKUPE HEKIMA, BUSARA NA UJASIRI ili uweze kuliokoa taifa hili katika janga la umaskini, uvivu, ufisadi, wizi, uzembe, ubinafsi nk.
NIMEIPENDA
 
Nani wa kulaumiwa?kizazi kipya kimezaliwa na kulelewa na kizazi cha akina Nyerere,Kizazi cha Abed Amani Karume,Mwinyi,Mkapa,na Kikwete.Mtoto umleavyo ndio akuavyo.Uholazi crime rate inapungua wanafunga magereza lakini Tanzania ndio tunapanua maabusi na jela.Acha kupotosha umma.
KWAHIYO UNATAKA TUFUNGE MAGEREZA ILI MUENDELEA KUTWIBIA,MPAKA MAFISAD WATAKAPOKWISHA NDO TUTAFUNGA MAGEREZA
 
Pamoja na kuandika mambo mengi mazuri ambayo ndio udhaifu wa nchi na wananchi wake, Lakini ningekuona wa maana kumshauri bw. mkubwa akawa na taasisi imara zenye nguvu za kujitegemea e.g. Katiba nzuri, Takukuru huru. Kwa sababu Maghufuli ni mwanaadamu kipindi chake kitaisha na atapita
NI KWELI MKUU ILO NALO NINENO LA KULIANGALIA KWA MAKINI ANAWEZA AKAJA MTAWALA MWINGINE AKAANZA KULA BATA TUTARUDI TENA KWENYE ULIMWENGU WA UFISADI
 
Bado hajabana vizur mi naona huku mitaani watu wanalewa asubuhi, watu wanaombaomba il hali wananguvu bana tengeneza katiba itakayoongoza miaka ming hata ukitoka madalakani lazima ifuatwe tutakushukuru sana hebu tunaomba uludishe madili yetu ya zamani halafu kama hawa wadada wanaovaa nusu uchi suluwali zimebana na vipedo (skin tite)kwa nn wasizibitiwe na vijana wanao lewa asubuhi viloba?jamani tunaomba rais wetu maguful kama unaingiaga hum hebu jaribu kusoma huuu uzi kwa kweli nchi yetu hii inahuzunisha sana.
 
Mtoa mada nakupongeza kwa dhati kabisa, kwani kwa asilimia kubwa upo sahihi kabisa. Nchi hii watu wengi wanataka mambo makubwa na ya kifahari huku wakiwa wamekaa tu bila hata kujishughulisha kwa namna yoyote ile. Ni watu wenye kuilalamikia serikali kwa kila jambo bila aibu. Ni kizazi kilichokosa uvumilivu na kisichojituma. Ili kubadili hali na mtazamo wa watu wa nchi hii ili wawe wachapakazi ilikuwa ni kumweka madarakani RAIS ambaye ni KOMANDOO, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na viongozi wote wa ngazi mbalimbali wawe ni wanajeshi na nchi iongozwe kijeshi japo kwa miaka michache tu. Kwa kufanya hivyo bila shaka nchi ingeweza kupiga hatua za maendeleo siku hadi siku. MHESHIMIWA RAIS MAGUFULI, MUNGU AKUONGOZE, AKULINDE, AKUTIE NGUVU, AKUPE HEKIMA, BUSARA NA UJASIRI ili uweze kuliokoa taifa hili katika janga la umaskini, uvivu, ufisadi, wizi, uzembe, ubinafsi nk.
Ni kweli mkuu maana nchi hii ilikuwa imefika pabaya sana, ofisi za serikali ziligeuzwa mali binafsi kila aliyekuwa akipata nafasi hiyo aliona kama kiamba chake binafsi bila kujali maslahi ya nchi yetu.
 
Magufuli tunakuunga mkono baba, watu walizoea vya bwerere. Fe fikiria mtu hajasoma lakini ana wadhifa serikalini, waliosoma walionekana wajinga. Wajanja wanabangaiza tu na kujipatia mishahara serikalini huku wakichekewa na kuambiwa fursa kwa kila Mkwere/Mtanzania, for what wakati haujasoma kihivyo? Pale Ikulu ilikuwa ni sehemu ya dili, watu wanahonga pesa wapatiwe kuongoza almashauri ili waiibie serikali na yule jamaa mtalii alijuwa lakini alikuwa anacheka tu. Kwa sasa vihiyo wanatumbuliwa eti wanalia na kumkejeli rais kuwa ni dikteta, really? Yaani hujasoma na hauna ujuzi wowote ule unataka ulipwe tu na serikali? To hell.
Lazima tumuunge mkono katika kurudisha heshima ya nchi yetu. Kuhakikisha rasilimali na maliasili za taifa letu zinalindwa, kutunzwa, na kutumiwa katika namna bora, endelevu na kwa maslahi ya watanzania wote.
 
Pamoja na kuandika mambo mengi mazuri ambayo ndio udhaifu wa nchi na wananchi wake, Lakini ningekuona wa maana kumshauri bw. mkubwa akawa na taasisi imara zenye nguvu za kujitegemea e.g. Katiba nzuri, Takukuru huru. Kwa sababu Maghufuli ni mwanaadamu kipindi chake kitaisha na atapita
Ni kweli usiopingika kwamba lazima tuwe na taasisi zenye nguvu na huru kwa mfano taasisi kama TAKUKURU ina madaraka ya kuchunguza vitendo vya rushwa na kukamata wahalifu. Lakini uwezo wake wa kupeleka watuhumiwa mahakamani unaishia kwa makosa madogo madogo tu. Kwa makosa makubwa TAKUKURU haina uwezo wa kupeleka watuhumiwa mahakamani bila kibali cha mkurungenzi wa mashtaka.

Mkurungezi wa mashitaka ambaye ndiye huamua kama kesi ipelekwe mahakamani au isipelekwe. Kwa hiyo mwendesha mashitaka ana uwezo wa kusimamisha mashitaka ya haina yoyote yanayoendelea mahakamani, aliyofungua yeye au mamlaka nyingine yoyote ikiwemo TAKUKURU. Mkurungezi wa mashtaka atafanya kama anavyoona yeye na hatalazimika kufuata maagizo au maelekezo kwa mtu yeyote isipokuwa Rais.

Kwa masharti haya TAKUKURU inakosa meno kwa ajili ya kuwachukulia vigogo wakubwa wanaongoza katika taasisi zao kwa rushwa kubwa. Kwa hiyo ufanisi unakuwa mdogo sana wa TAKUKURU. Wakati mwingine TAKUKURU inapeleka kesi mahakamani lakini mahakama inatupilia mbali kesi hizo zinazopelekwa mahakamani na Mkurungezi wa mashtaka kwa kukosa ushaidi wa kutosha.

Kwa hali kama hii ndio maana tumekuwa na kilio kikubwa cha kupata katiba mpya itakayoipatia TAKUKURU meno na kuimarisha misingi na mifumo imara ya taasisi za umma.
 
Ni kweli usiopingika kwamba lazima tuwe na taasisi zenye nguvu na huru kwa mfano taasisi kama TAKUKURU ina madaraka ya kuchunguza vitendo vya rushwa na kukamata wahalifu. Lakini uwezo wake wa kupeleka watuhumiwa mahakamani unaishia kwa makosa madogo madogo tu. Kwa makosa makubwa TAKUKURU haina uwezo wa kupeleka watuhumiwa mahakamani bila kibali cha mkurungenzi wa mashtaka.

Mkurungezi wa mashitaka ambaye ndiye huamua kama kesi ipelekwe mahakamani au isipelekwe. Kwa hiyo mwendesha mashitaka ana uwezo wa kusimamisha mashitaka ya haina yoyote yanayoendelea mahakamani, aliyofungua yeye au mamlaka nyingine yoyote ikiwemo TAKUKURU. Mkurungezi wa mashtaka atafanya kama anavyoona yeye na hatalazimika kufuata maagizo au maelekezo kwa mtu yeyote isipokuwa Rais.

Kwa masharti haya TAKUKURU inakosa meno kwa ajili ya kuwachukulia vigogo wakubwa wanaongoza katika taasisi zao kwa rushwa kubwa. Kwa hiyo ufanisi unakuwa mdogo sana wa TAKUKURU. Wakati mwingine TAKUKURU inapeleka kesi mahakamani lakini mahakama inatupilia mbali kesi hizo zinazopelekwa mahakamani na Mkurungezi wa mashtaka kwa kukosa ushaidi wa kutosha.

Kwa hali kama hii ndio maana tumekuwa na kilio kikubwa cha kupata katiba mpya itakayoipatia TAKUKURU meno na kuimarisha misingi na mifumo imara ya taasisi za umma.
Bahati mbaya kwa nchi yangu ni kuwa wengine wamekuwa washabiki hawataki hata Rais kushauriwa vinginevyo
 
Ni kweli usiopingika kwamba lazima tuwe na taasisi zenye nguvu na huru kwa mfano taasisi kama TAKUKURU ina madaraka ya kuchunguza vitendo vya rushwa na kukamata wahalifu. Lakini uwezo wake wa kupeleka watuhumiwa mahakamani unaishia kwa makosa madogo madogo tu. Kwa makosa makubwa TAKUKURU haina uwezo wa kupeleka watuhumiwa mahakamani bila kibali cha mkurungenzi wa mashtaka.

Mkurungezi wa mashitaka ambaye ndiye huamua kama kesi ipelekwe mahakamani au isipelekwe. Kwa hiyo mwendesha mashitaka ana uwezo wa kusimamisha mashitaka ya haina yoyote yanayoendelea mahakamani, aliyofungua yeye au mamlaka nyingine yoyote ikiwemo TAKUKURU. Mkurungezi wa mashtaka atafanya kama anavyoona yeye na hatalazimika kufuata maagizo au maelekezo kwa mtu yeyote isipokuwa Rais.

Kwa masharti haya TAKUKURU inakosa meno kwa ajili ya kuwachukulia vigogo wakubwa wanaongoza katika taasisi zao kwa rushwa kubwa. Kwa hiyo ufanisi unakuwa mdogo sana wa TAKUKURU. Wakati mwingine TAKUKURU inapeleka kesi mahakamani lakini mahakama inatupilia mbali kesi hizo zinazopelekwa mahakamani na Mkurungezi wa mashtaka kwa kukosa ushaidi wa kutosha.

Kwa hali kama hii ndio maana tumekuwa na kilio kikubwa cha kupata katiba mpya itakayoipatia TAKUKURU meno na kuimarisha misingi na mifumo imara ya taasisi za umma.
Taasisi hii ilifaa iwe huru bila kuingiliana na mhimili mwingine wa serikali bila hivyo rushwa haitaisha kabisa. Rais atabaki kupiga kelele tu basi.

Lakini kuna taasisi kama hii inajiita ya maadili ya umma kazi yao nini maana mi naona kama haina umuhimu wowote katika taifa hili, labda ni kitengo cha ulaji tu. Maana wao ndio wangeshughulika na hawa watumishi wanaovunja maadili yao na kukalia rushwa na wizi tu.
 
Taasisi hii ilifaa iwe huru bila kuingiliana na mhimili mwingine wa serikali bila hivyo rushwa haitaisha kabisa. Rais atabaki kupiga kelele tu basi.

Lakini kuna taasisi kama hii inajiita ya maadili ya umma kazi yao nini maana mi naona kama haina umuhimu wowote katika taifa hili, labda ni kitengo cha ulaji tu. Maana wao ndio wangeshughulika na hawa watumishi wanaovunja maadili yao na kukalia rushwa na wizi tu.
Mkuu, Sekretarieti ya maadili iliundwa kwa mujibu wa ibara ya 132 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Kama ilivyo TAKUKURU, Sekretarieti ya maadili ya umma, ina jukumu la kuchunguza na kusimamia mwenendo wa maadili ya viongozi wa umma wakiwemo watendaji wakuu wa serikali na viongozi wa kuchaguliwa.

Taasisi hii pia iko chini ya ofisi ya Rais, kwa hiyo Sekretarieti ya maadili haina madaraka ya kuchukua hatua za kuadhibu viongozi wanaokiuka maadili ya viongozi wa umma. Badala yake Sekretarieti hupeleka mapendekezo yake kwa Rais na Spika wa Bunge au wakati mwingine kwa Rais peke yake kutegemeana na suala lilivyo. Kwa hiyo bado tunabaki pale pale kuwa ufanisi wa Sekretarieti ya maadili utendaji wake utategemea ridhaa na maoni ya Rais na Spika kuhusu malalamiko yatakayotolewa.
 
Lazima tumuunge mkono katika kurudisha heshima ya nchi yetu. Kuhakikisha rasilimali na maliasili za taifa letu zinalindwa, kutunzwa, na kutumiwa katika namna bora, endelevu na kwa maslahi ya watanzania wote.


Magufuli inabidi ampige ban Kikwete asionekane mtaani kwani anatia taifa letu haibu.
 
Tatizo NI hiki kizazi cha Viroba
Nakuambia nitatizo,
Kutwa siasa kazi hapana.
Siasa zenyewe hawajui kufuata mkumbo tu.
Tatizo lingine
Kuachia watu Elimu ndogo kuongoza Vyama vilivyo zungukwa na wenye Elimu kubwa pia NI tatizo.

Magu kaonyesha anaingia JF
Tunaomba aongeze kubana zaidi

Bila hivyo mambo yatakuwa mabaya

Wenye Elimu kubwa wanaoongozwa na wenye Elimu ndogo ni kwa sababu ya AKILI ndogo.
Afadhali mwenye AKILI kubwa na Elimu ndogo kuliko mwenye Elimu kubwa na AKILI ndogo.
 
kweli wewe hujielewi, unamshauri awe dikiteta harafu unamaliza kwa kusema Mungu amjalie hekima na busara, uliona wapi dikiteta anakuwa na hekima na busara? by the way hujui dikiteta ni MTU Wa aina gani na hufanya nini kwa nchi anayoiongoza maana ungejua usingeomba kiongozi wako awe dikiteta
 
Naililia nchi yangu Tanzania , kila nikitafakari machozi yananitoka nakosa majibu nabaki kujiuliza tutafika kweli? Magufuli kazi unayo sana kuongoza kizazi hiki cha ****** pole sana!

Boniphace .M. Pesambili.
Pesambili BM
Ni kweli unapenda "udikteta" au kiongozi wako awe "dikteta"?
Kama unapenda hayo, wewe ni hovyo kabisa. Tena unaleta fyokofyoko. Unajua mwisho wa madikteta?

Kama ambavyo wadau wengine wamekupa shule. Tanzania inahitaji taasisi imara, zile zinazotakiwa ziwe huru zionekane hivyo na sio kutumikia wanasiasa au kutumika kisiasa.

Kama unampenda mtumbua majipu, ungemshauri ajenge taasisi imara.

Wewe unajua ni chama gani kimetufikisha hapa tulipo? Ni hikohiko chama cha majipu ambacho mtumbua majipu anasema anakipenda kwa sababu kimempa urais.

Kumbuka Magufuli kama alichaguliwa kwa kura za wadanganyika(wananchi) yeye ni mtumishi wa wananchi. Wakati anapita kuomba "kula" alikuwa anajitupa chini na kupiga push up na "kuomba" kwa unyenyekevu achaguliwe. Inakuwaje leo umpe high 5 ajigeuze " dikteta". Hilo halikubaliki.

Akiwatendea haki anaowaongoza basi kuongoza kwa ushawishi ni rahisi.

Hatutaki DOMOkrasi, tunataka DEMOkrasi.
Na ni taasisi imara tu ndio zitahakikisha kuwa nchi inaongozwa vizuri.

Je JPM atajenga Taasisi imara na huru? Hiyo ndiyo changamoto inayomkabili Baba. J.
Tuendelee kumwombea kuwa kiongozi bora na sio kuwa dikteta.
 
Pesambili BM
Ni kweli unapenda "udikteta" au kiongozi wako awe "dikteta"?
Kama unapenda hayo, wewe ni hovyo kabisa. Tena unaleta fyokofyoko. Unajua mwisho wa madikteta?

Kama ambavyo wadau wengine wamekupa shule. Tanzania inahitaji taasisi imara, zile zinazotakiwa ziwe huru zionekane hivyo na sio kutumikia wanasiasa au kutumika kisiasa.

Kama unampenda mtumbua majipu, ungemshauri ajenge taasisi imara.

Wewe unajua ni chama gani kimetufikisha hapa tulipo? Ni hikohiko chama cha majipu ambacho mtumbua majipu anasema anakipenda kwa sababu kimempa urais.

Kumbuka Magufuli kama alichaguliwa kwa kura za wadanganyika(wananchi) yeye ni mtumishi wa wananchi. Wakati anapita kuomba "kula" alikuwa anajitupa chini na kupiga push up na "kuomba" kwa unyenyekevu achaguliwe. Inakuwaje leo umpe high 5 ajigeuze " dikteta". Hilo halikubaliki.

Akiwatendea haki anaowaongoza basi kuongoza kwa ushawishi ni rahisi.

Hatutaki DOMOkrasi, tunataka DEMOkrasi.
Na ni taasisi imara tu ndio zitahakikisha kuwa nchi inaongozwa vizuri.

Je JPM atajenga Taasisi imara na huru? Hiyo ndiyo changamoto inayomkabili Baba. J.
Tuendelee kumwombea kuwa kiongozi bora na sio kuwa dikteta.
Ndugu yangu Nonda, Kwa kifupi hakuna nchi yoyote inayopenda dhana ya udikteta na tena nakubaliana na wewe kuwa utawala wa kisheria ni moja ya misingi imara ya demokrasia, lakini ni sheria hizo zinazotumika kwa tafsiri halisi ama hasi. Miongoni Mwa wanahabari, wanasiasa , wanataalum pamoja na viongozi wa dini walioji sana udhaifu wa serikali ya awamu ya 4 uliosababishwa na kutokuchukuliwa kwa uamuzi mgumu. Wakiwa na maana uamuzi mgumu ni ule unaolenga maslahi ya umma.

Mh Rais Magufuli aliamua kuchukua hatua ya uamuzi mgumu kupambana na rushwa, ufisadi na uzembe wa watumishi wa umma lakini wakamuita "dikteta uchwara" sio jina zuri hata kidogo kulitumia lakini kabatizwa hilo jina, nikaona kwa sababu kaitwa dikteta uchwara kwa hatua unazochukua basi heri dikteta anayedhibiti dhuluma, wizi, ufisadi, unyang'anya, uporaji wa Mali za umma, unafiki wa viongozi, uzandiki na wale wote watumishi waliokuwa wanatumia madaraka au ofisi za umma vibaya waliogeuka miungu watu. kwa kuendelea kubembelezana hatutafika kamwe ndugu yangu Nonda.
 
Back
Top Bottom