Rais Magufuli kakosea, RPC Mbeya hana kosa; nilishatoa ushauri Mbeya barabara iwe double Uyole hadi Mbalizi

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Raisi Magufuli anasema RPC Mbeya afukuzwe kazi. Raisi Magufuli anaweza kutuambia kosa la RPC kwa ajali hii ya Mbeya ni nini hasa? Au ni ile kawaida ya kutoa kauli za kisiasa kwa jambo ambalo sio la siasa?

Kama kuna mtu wa kukukuza kazi basi ni Meneja wa Tanroads wa Mbeya, Mkuu wa Mkoa pamoja na Mkurugenzi wa jiji.

Kazi ya Traffic Polisi ni kusimamia usalama wa barabarani kulingana na miundo mbinu iliyopo, sio ku-design miundo mbinu ili ajali zisitokee. Hapo ndipo utaona Raisi Magufuli anahitaji ushauri kabla ya kutoa matamko ya kisiasa kwa matukio nchini yasiyo ya kisiasa.

Tuangalie tukio la ajali. Hizi kauli za lori kufeli breki ni za kiasiasa na uongo. Ukweli ni kwamba wakati lori likishuka huu mteremko, kuna Hiace ailijaribu ku-overtake coaster na ikakutana na hili lori likishuka. Hapo ndipo kimbembe kilipoanza katika harakati za kukwepa na kukwepana, na kusababbisha ajali yote. Hakuna dereva wa lori la mzigo mwenye akili atashuka huu mteremko kwa kasi. Ni mteremko mkali ambao kila dereva wa lori anajua anapaswa kushuka kwa low gear zikisaidiana na breki, kwa hiyo suala la kusema lori likikuwa likienda kasi ni za kutunga.

Sasa Meneja wa Tanroads Mbeya, Mkurgenzi wa Jiji na Mkuu wa Mkoa wote wanajua hili ni eneo la hatari sana, kwanza kila wakati wanapita njia hii kwenda Songwe airport. Hawaoni kuwa angalau hata walipaswa kuweka climbing lane kwenye hili eneo baada ya ajali nyingi sana na watu wengi kufa katika sehemu hii? Si mara ya kwanza, nadhani mtakumbuka huko nyuma gari ya mbunge ilipata ajali hapa na kuungua na watu kadhaa kufa, sababu zikiwa zile zile ku-overtake sehemu hii.

Na pia Mbeya kwa sasa hii barabara ya Tanzam kuanzia eneo la Uyole ni tatizo. Ina msongamano mkubwa wa magari unaoweka hatarini waenda kwa miguu na magari. Nilishaweka post humu ndani kwamba hili ni tatizo linakua kila siku. Siku nyingi sana niliweka post humu JF na kuuliza kama Tanroads hawalioni hili tatizo, ukizingatia Mbeya ni jiji, na nikatoa pendekezo barabara double (dual carriageway) ijengwe kuanzia Uyole hadi Mbalizi. Kama ushauri huu ungefuatwa vifo vingi sana eneo la mteremko wa Mbalizi vingeepushwa.

Ushauri nilioweka hapo nyuma;

Mbeya msilale, shurutisheni serikali iwatengee fedha za kupanua barabara ya Tanzam eneo la Mwanjelwa hadi Mbalizi

Kwa msisitizo, kama Raisi Magufuli anataka kutumbua watu kutokana na hii ajali basi wanaopaswa kuwajibishwa ni Meneja wa Tanroads, Mkurugenzi wa Jiji na Mkuu wa Mkoa. RPC mnamwonea tu.
 
Shida kubwa ni madereva wala sio barabara. Barabara madereva wengi wanazijua hasa hao wa malori na mabasi sasa kinachowafanya washuke mbio au kuovateki kwenye sehemu mbaya ni nini kama sio bangi? Au hao madereva waliohusika na hio ajali ni wageni wa hio njia?

Kwa akili za madereva wengi hata uwawekee dual carriageway bado watasababisha ajali tu! Na wa kuweza kukomesha hizi akili za bangi ni wasimamia sheria tu.
 
Nafikiri vyote viwili ni tatizo madereva fulani na attitude zao na viongozi wanaosimamia sheria. Hawatumii mamlaka yao ipasavyo.

Kila mtu akifanya kazi yake inavyotakiwa ajali zitapungua.
 
Ukweli ni kuwa madereva ndio wanamakosa zaid huwezi Ku overtake sehemu ambayo unaifahamu kuwa sio salama.
 
Shida kubwa ni madereva wala sio barabara. Barabara madereva wengi wanazijua hasa hao wa malori na mabasi sasa kinachowafanya washuke mbio au kuovateki kwenye sehemu mbaya ni nini kama sio bangi? Au hao madereva waliohusika na hio ajali ni wageni wa hio njia?

Kwa akili za madereva wengi hata uwawekee dual carriageway bado watasababisha ajali tu! Na wa kuweza kukomesha hizi akili za bangi ni wasimamia sheria tu.
Kweli mkuu, lakini kupeleka lawama kirahisi rahisi kwa dereva wa lori eti halikuwa na breki ni kutaka kufanya hatujui tatizo ni nini. Hiace ndiyo ilikuwa inaovertake Coaster na hii sehemu kama sio kuiwekea dual carriageway basi angalau walipaswa waweke climbing lane.

Hivi unakumbuka tatizo la ajali barabara kati ya Dar na Morogoro zilivyomalizwa kwa kuweka climbimg lanes? Sasa Tanroads wasichojua ni nini?
 
Kweli mkuu, lakini kupeleka lawama kirahisi rahisi kwa dereva wa lori eti halikuwa na breki ni kutaka kufanya hatujui tatizo ni nini. Hiace ndiyo ilikuwa inaovertake Coaster na hii sehemu kama sio kuiwekea dual carriageway basi angalau walipaswa waweke climbing lane.

Hivi unakumbuka tatizo la ajali barabara kati ya Dar na Morogoro zilivyomalizwa kwa kuweka climbimg lanes? Sasa Tanroads wasichojua ni nini?
With or without climbing lanes.....kama akili za madereva hazitabadilika ajali zitazidi kuongezeka. SA wana barabara nzuri sana, three-lane highways lakini kuna fatal accidents nyingi sana. Unafikiri kwa nini?

South Africa's road death toll a 'national crisis'
 
With or without climbing lanes.....kama akili za madereva hazitabadilika ajali zitazidi kuongezeka. SA wana barabara nzuri sana, three-lane highways lakini kuna fatal accidents nyingi sana. Unafikiri kwa nini?

South Africa's road death toll a 'national crisis'
Hivi Mkuu hukumbuki ajali zilivyokuwa zinatokea kila mwezi barabara ya Morogoro eneo baada ya Chalinze? Baada ya kuweka climbing lanes hujaona tofauti?
 
Mkulu kayaongea jana
Imekuwaje leo ndio uibuke kuja kumlilia humu?

Mmejadili au mlifikiri anatania!!

Wameshajiuzuru au bado wanasubiri kupunguziwa nyota?

Ungekuwa siriasi na sio kujitetea kikazi.. ungeambatanisha na picha hata video na maelezo ya risechi ya hizo ajali tatu zilizotokea
 
Mkulu kayaongea jana
Imekuwaje leo ndio uibuke kuja kumlilia humu?

Mmejadili au mlifikiri anatania!!

Wameshajiuzuru au bado wanasubiri kupunguziwa nyota?

Ungekuwa siriasi na sio kujitetea kikazi.. ungeambatanisha na picha hata video na maelezo ya risechi ya hizo ajali tatu zilizotokea

Hueleweki. Angalia hapa niliyoyasema mwanzoni mwa mwaka kabla ya huyo Mkulu

Mbeya msilale, shurutisheni serikali iwatengee fedha za kupanua barabara ya Tanzam eneo la Mwanjelwa hadi Mbalizi
 
Mi naona jamaa alikuwa ana mpango wa kuharibu CV ya Mwigulu tu coz since day 1 baraza linatajwa everyone expected yule jamaa apewe wizara yake coz ndio field yake na field ambayo alionyesha anaimudu sana.
But tofauti na matarajio ya watu wengi akapelekwa Kilimo, mara kidogo Mambo ya ndani, unategemea nini, muhasibu unampa kazi ya mwanasheria unategemea ataderiver nini

Kwa hiyo hizo lawama alizomrushia mzee wa skafu sio na hata ivyo hayo matatizo aliyoyaorodhesha yapo miaka nenda rudi

Ngoja tusubiri Kangi amalize ajali barabarani, sijui atakuwa anazibeba gari mkononi

Let's see
 
Hivi Mkuu hukumbuki ajali zilivyokuwa zinatokea kila mwezi barabara ya Morogoro eneo baada ya Chalinze? Baada ya kuweka climbing lanes hujaona tofauti?
Takwimu zinaonesha ajali nyingi ni sababu ya madereva na sio miundo mbinu. Aidha kuovateki kwenye kona,kwenye mlima au mwendokasi uliopitiliza. Barabara ya Morogoro ajali zimepungua kwasababu hamna kipande kirefu unaweza kukimbia bila kukutana na kizuizi aidha tochi au matuta. Unaweza kukimbia usiku tu napo kunakuwa na magari machache. Hio safari sasa hivi inachukua hadi masaa manne ila ni bora ukawie ufike.
 
Takwimu zinaonesha ajali nyingi ni sababu ya madereva na sio miundo mbinu. Aidha kuovateki kwenye kona,kwenye mlima au mwendokasi uliopitiliza. Barabara ya Morogoro ajali zimepungua kwasababu hamna kipande kirefu unaweza kukimbia bila kukutana na kizuizi aidha tochi au matuta. Unaweza kukimbia usiku tu napo kunakuwa na magari machache. Hio safari sasa hivi inachukua hadi masaa manne ila ni bora ukawie ufike.
Sehemu nyingi za milima ajali zilipokuwa zinatokea barabara ya Morogoro hazina tochi. Tochi zipo maeneo ya makazi ya watu, kwa hiyo conclusion yako sio ya kweli.
 
Nakumbuka hili eneo,nilipita mwezi wa 5 mwishoni,lori lilikuwa limetoka kuanguka na watu ndio kwanza wameanza kujazana...
 
Siasa kwenye maswala tasiyo ya siasa ajali nyingi zinasababishwa na miundombinu ila wakulaumiwa ni dereva na polosi kwanini ajali mbeya issue siyo RPC wa RTO badala ya kukaa na kujiuliza na kufanya utafiti ila kwa vile Jiwe kajiita mtumbua majipu acha tu tuendelee hivyo hivyo tu
 
Mkulu kayaongea jana
Imekuwaje leo ndio uibuke kuja kumlilia humu?

Mmejadili au mlifikiri anatania!!

Wameshajiuzuru au bado wanasubiri kupunguziwa nyota?

Ungekuwa siriasi na sio kujitetea kikazi.. ungeambatanisha na picha hata video na maelezo ya risechi ya hizo ajali tatu zilizotokea
Kama huvuti bangi basi mlevi wa gongo
 
Raisi Magufuli anasema RPC Mbeya afukuzwe kazi. Raisi Magufuli anaweza kutuambia kosa la RPC kwa ajali hii ya Mbeya ni nini hasa? Au ni ile kawaida ya kutoa kauli za kisiasa kwa jambo ambalo sio la siasa?

Kama kuna mtu wa kukukuza kazi basi ni Meneja wa Tanroads wa Mbeya, Mkuu wa Mkoa pamoja na Mkurugenzi wa jiji.

Kazi ya Traffic Polisi ni kusimamia usalama wa barabarani kulingana na miundo mbinu iliyopo, sio ku-design miundo mbinu ili ajali zisitokee. Hapo ndipo utaona Raisi Magufuli anahitaji ushauri kabla ya kutoa matamko ya kisiasa kwa matukio nchini yasiyo ya kisiasa.

Tuangalie tukio la ajali. Hizi kauli za lori kufeli breki ni za kiasiasa na uongo. Ukweli ni kwamba wakati lori likishuka huu mteremko, kuna Hiace ailijaribu ku-overtake coaster na ikakutana na hili lori likishuka. Hapo ndipo kimbembe kilipoanza katika harakati za kukwepa na kukwepana, na kusababbisha ajali yote. Hakuna dereva wa lori la mzigo mwenye akili atashuka huu mteremko kwa kasi. Ni mteremko mkali ambao kila dereva wa lori anajua anapaswa kushuka kwa low gear zikisaidiana na breki, kwa hiyo suala la kusema lori likikuwa likienda kasi ni za kutunga.

Sasa Meneja wa Tanroads Mbeya, Mkurgenzi wa Jiji na Mkuu wa Mkoa wote wanajua hili ni eneo la hatari sana, kwanza kila wakati wanapita njia hii kwenda Songwe airport. Hawaoni kuwa angalau hata walipaswa kuweka climbing lane kwenye hili eneo baada ya ajali nyingi sana na watu wengi kufa katika sehemu hii? Si mara ya kwanza, nadhani mtakumbuka huko nyuma gari ya mbunge ilipata ajali hapa na kuungua na watu kadhaa kufa, sababu zikiwa zile zile ku-overtake sehemu hii.

Na pia Mbeya kwa sasa hii barabara ya Tanzam kuanzia eneo la Uyole ni tatizo. Ina msongamano mkubwa wa magari unaoweka hatarini waenda kwa miguu na magari. Nilishaweka post humu ndani kwamba hili ni tatizo linakua kila siku. Siku nyingi sana niliweka post humu JF na kuuliza kama Tanroads hawalioni hili tatizo, ukizingatia Mbeya ni jiji, na nikatoa pendekezo barabara double (dual carriageway) ijengwe kuanzia Uyole hadi Mbalizi. Kama ushauri huu ungefuatwa vifo vingi sana eneo la mteremko wa Mbalizi vingeepushwa.

Ushauri nilioweka hapo nyuma;

Mbeya msilale, shurutisheni serikali iwatengee fedha za kupanua barabara ya Tanzam eneo la Mwanjelwa hadi Mbalizi

Kwa msisitizo, kama Raisi Magufuli anataka kutumbua watu kutokana na hii ajali basi wanaopaswa kuwajibishwa ni Meneja wa Tanroads, Mkurugenzi wa Jiji na Mkuu wa Mkoa. RPC mnamwonea tu.
Hapa nitatetea kidogo, kwa nini dereva atake kuovateki kwenye mteremko? Dereva ni mzembe na inawezekana hajui taratibu za udereva. Mpaka kafika hapo kuna uwezekano huko atokako polisi hawajafanya kazi yao kwa huyu dereva. Ajali nyingi ni za dereva mmoja kujaribu kuovateki eneo ambalo sio la kuovateki. Yawezekana uko sahihi kuwa rpc kwa kiasi fulani hausiki ila sio jambo la barabara.
 
Hapa nitatetea kidogo, kwa nini dereva atake kuovateki kwenye mteremko? Dereva ni mzembe na inawezekana hajui taratibu za udereva. Mpaka kafika hapo kuna uwezekano huko atokako polisi hawajafanya kazi yao kwa huyu dereva. Ajali nyingi ni za dereva mmoja kujaribu kuovateki eneo ambalo sio la kuovateki. Yawezekana uko sahihi kuwa rpc kwa kiasi fulani hausiki ila sio jambo la barabara.
Mkuu dereva aliyekuwa ana-overtake alikuwa anapanda huo mlima, na alikuwa ana-overtake Coaster sio lori. Alikutana na hilo lori.

Ukweli ni kwamba huu ni mlima mkali na kuna gari zinaenda taratibu mno. Inatia sana shauku ya kutaka kuzipita gari zinazoenda taratibu. Pia hata kukaa nyuma ya gari zinazopanda mlima taratibu sana kwa muda mrefu ni hatari, maana matokeo yalishatokea hapa gari kushindwa kupanda na kurudi nyuma na kugonga magari.

Ndio maana nikasema suluhisho ambalo huhitaji kuwa injinia kulifikiria ni climbing lane kwa gari zinazoelekea Mbeya
 
Back
Top Bottom