Bilionea Asigwa
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 16,587
- 28,750
Rais wangu Magufuli, hakika hii nchi kama una nia ya kweli ya kuirekebisha, soon itakutia uchizi, awamu na nne ilitotangulia imefanya madudu ya kutisha ukiamua kuyafuatilia kwa makini unaweza geuka chizi siku za hivi karibuni.
NSSF imeripotiwa na gazeti la Mwananchi imeitia serikali harasa ya zaidi ya Trillioni 1.33 katika miradi yake miwili tu ya Kigamboni(sio daraja) na Arumeru kati ya mingi iliyonayo , mradi wa Ujenzi wa mji mpya wa Kigamboni zaidi ya Tshs Billioni 179 zimepigwa na wajanja wachache, ardhi imenunuliwa kwa Tshs Millioni 800 kwa hekari badala ya Tshs millioni 39, huko Arumeru ardhi imenunuliwa kwa Billioni 1.8 kwa hekari badala ya Tshs laki 5 ikizidi sana Millioni 1.
Barrick Gold Mine kwa miaka minne tu nyaraka zinaonyesha imeingiza zaidi ya Tshs Trillioni 1.79 huku kwetu inadai kuwa haijawahi kuingiza hata senti moja kwa kuwa ilikuwa inapata hasara kubwa(ilikua ikijiendesha kwa hasara), cha ajabu mtangulizi wako alikua kila siku akiisifia kwenye majukwaa.
Leo tunakwenda mahakamani tunaishia kulipwa billioni 89.
Wamarekani wanasitisha misaada yao kwa ishu ya uchaguzi wa Zanzibar, Mchina na Mjapani walivyoonekana kuanza kujisogeza sogeza, leo msemaji wa MCC anadai kuwa serikali iende "kuzungumza nao vizuri" na ukienda na "hoja nzuri" na "za kuridhisha" ,wanaachia mpunga, wao "hawana shida", wanapoulizwa vipi kuhusu ile ishu ya Zanzibar mliyodai ndio sababu ya kusitisha msaada wanakataa kuiongelea kabisa, wanaipotezea kimya kimya, wanadai ajenda andaa tu wewe hawakuchagulii na wako tayari kurejesha hizi hela "ukizungumza nao tu vizuri".
Bandari kumeoza, zinaibwa mpaka meli, makontena zaidi ya 11,000 yanayeyuka mchana mchana, na mengine ya flow meters.
Huko bungeni napo wabunge wanakula rushwa utadhani mtu anatafuna karanga mbichi, wabunge wetu tuliowatuma watutetee wana mpango wa kuivunja EWURA kisa inawabana bana kwenye ishu zao za kukwepa kodi kwenye biashara zao za mafuta.
Ishu za madawa ya kulevya nazo zimepamba moto, kinara wa dawa za kulevya Shikuba kakamatwa kaweka gerezani, inadaiwa anaishi kama mfalme huko magarezani, "mfungwa anakula mpaka kuku" ?? nani kazipeleka kuku rosti huko gerezani??
mpaka mkuu wa magereza anaogopa, kamati ya bunge ilivyoenda kumtembelea akaomba aongezewe ulinzi la sivyo Shikuba aondolewe mana kamzidi uwezo.
Hebu angalia timu yako iliyoko hapo ikulu upya, iko upande wako kweli??.
Sio wao waliokuwa wanufaika wakubwa wa haya mambo??
Mukulu aisee, hii nchi hii ukiamua kuifumua sana, soon itakutia uchizi.
NSSF imeripotiwa na gazeti la Mwananchi imeitia serikali harasa ya zaidi ya Trillioni 1.33 katika miradi yake miwili tu ya Kigamboni(sio daraja) na Arumeru kati ya mingi iliyonayo , mradi wa Ujenzi wa mji mpya wa Kigamboni zaidi ya Tshs Billioni 179 zimepigwa na wajanja wachache, ardhi imenunuliwa kwa Tshs Millioni 800 kwa hekari badala ya Tshs millioni 39, huko Arumeru ardhi imenunuliwa kwa Billioni 1.8 kwa hekari badala ya Tshs laki 5 ikizidi sana Millioni 1.
Barrick Gold Mine kwa miaka minne tu nyaraka zinaonyesha imeingiza zaidi ya Tshs Trillioni 1.79 huku kwetu inadai kuwa haijawahi kuingiza hata senti moja kwa kuwa ilikuwa inapata hasara kubwa(ilikua ikijiendesha kwa hasara), cha ajabu mtangulizi wako alikua kila siku akiisifia kwenye majukwaa.
Leo tunakwenda mahakamani tunaishia kulipwa billioni 89.
Wamarekani wanasitisha misaada yao kwa ishu ya uchaguzi wa Zanzibar, Mchina na Mjapani walivyoonekana kuanza kujisogeza sogeza, leo msemaji wa MCC anadai kuwa serikali iende "kuzungumza nao vizuri" na ukienda na "hoja nzuri" na "za kuridhisha" ,wanaachia mpunga, wao "hawana shida", wanapoulizwa vipi kuhusu ile ishu ya Zanzibar mliyodai ndio sababu ya kusitisha msaada wanakataa kuiongelea kabisa, wanaipotezea kimya kimya, wanadai ajenda andaa tu wewe hawakuchagulii na wako tayari kurejesha hizi hela "ukizungumza nao tu vizuri".
Bandari kumeoza, zinaibwa mpaka meli, makontena zaidi ya 11,000 yanayeyuka mchana mchana, na mengine ya flow meters.
Huko bungeni napo wabunge wanakula rushwa utadhani mtu anatafuna karanga mbichi, wabunge wetu tuliowatuma watutetee wana mpango wa kuivunja EWURA kisa inawabana bana kwenye ishu zao za kukwepa kodi kwenye biashara zao za mafuta.
Ishu za madawa ya kulevya nazo zimepamba moto, kinara wa dawa za kulevya Shikuba kakamatwa kaweka gerezani, inadaiwa anaishi kama mfalme huko magarezani, "mfungwa anakula mpaka kuku" ?? nani kazipeleka kuku rosti huko gerezani??
mpaka mkuu wa magereza anaogopa, kamati ya bunge ilivyoenda kumtembelea akaomba aongezewe ulinzi la sivyo Shikuba aondolewe mana kamzidi uwezo.
Hebu angalia timu yako iliyoko hapo ikulu upya, iko upande wako kweli??.
Sio wao waliokuwa wanufaika wakubwa wa haya mambo??
Mukulu aisee, hii nchi hii ukiamua kuifumua sana, soon itakutia uchizi.