Rais Magufuli avuruga wengi

Hata hivyo namna ya kumsimamisha haikuwa nzuri. Mh raisi anapaswa kuwaheshimu walio chini yake. JPJM amemhukumu Kabwe mbele ya hadhira na katika namna dhalili isiyofaa kwa binadamu yeyote.

Anyway, tulimtaka wenyewe sasa tumvumilie!
Alianza mwenyewe kujidhalilisha kwa kuiba mali za umma. Wenje alishawahi kulia sana bungeni lkn iyo iyo sheria haikufutilia wala kuchunguza tuhuma zinazomkabili leo sheria inaonekana sana kwa kuwa amemkuta. She ria inalinda sana wezi.big up Mr prezidaa
 
At least you are there brother thanks. Mie nilisema wapigwe risasi hadharani tu kusiwe kabisa na mafisadi.
 
Kwa bahati mbaya sana Mheshimiwa John Pombe Magufuli amekuja na kauli mbiu ya kutumbua majipu. Lakini binafsi naona hakuangalia mbali. Aliona mwisho wa pua yake tu. Hili ni kosa la kwa.nza kwa kiongozi mkubwa kama yeye, kutokuona mbali. Kosa la pili ni namna anavyotumbua jipu. Hatumbui kitaaluma namna majipu yanavyotakiwa utumbuliwa. Nitaeleza moja baada jingine.
Angalianza kujiuliza ni kwa nini majipu yapo. Majipu msingi wake ni upungufu wa kinga mwilini. Kinga ikipungua ukitumbua jipu hili huota jipu jingine mahala pengine. Mchezo hujirudia rudia hadi jipu linaota kwenye ini, mahala pabaya zaidi. Daktari makini hatibu dalili, hutibu kisababishi cha ugonjwa. Daktari makini hawezi kutibu kichwa kwa sababu kichwa ni kiashiria tu kuwa mwili unatatizo mahali. Atachunguza kitabibu. Akigundua kwa mgonjwa ana malaria atatibu malaria akiwa makini zaidi atamshauri mgonjwa kufyeka majani yote kuzunguka nyumba yake, kufukia vidimbwi vyote wanamozalia mbu na kutumia chandarua kwa kulala ndani ya chandarua mwaka mzima. Magufuli hafanyi hivyo anampa mgonjwa dawa ya kutuliza maumivu ya kichwa kwa kumpa panadol mbili mara tatu kutwa maumivu yakizidi anaongeza dozi tatu mara nne kutwa, lakini masikini DKT Magufuli mgonjwa wake Tanzania haponi na hakuna dalili kuwa atapona sababu anatibu dalili. Masikini Magufuli apate wa sikio ili asikie kuwa tatizo siyo majipu ni kinga imepungua ili ampe mgonjwa wake vyakula vinavyopandisha CD4? Shida ya Tanzania na watanzania ni maadili. Tatizo la maadili linaanzia kwa wanasiasa kujilimbizia mali kwa kutumia nafasi zao za kisiasa. Tanzama viongozi wa kisiasa wanavyojilimbizia mishahara mikubwa. Viongozi wa kisiasa kuanzia raisi, mkamu wa rais, waziri mkuu mawaziri manaibu mawaziri, wabunge nk nk mishahara yao na marupurupu yao yalivyo makubwa upita hata wanataaluma wa hali ya juu. Kansa hii ndiyo ndiyo iliyotufikisha hapa tulipo. Kiini cha jipu ni fikira kuw ukiwa na nafasi fulani ya kiutumishi sharti uitumie wewe mwenyewe kwanza kabla hujawagawia wengine. Jipu hili lipo katika kila ubongo wa Mtanzania kwa sasa. Hizo zingine ni dalili tu.
Nani aliyesema mtumishi aliyeko kwenye taasisi za fedha alipwe zaidi kuliko daktari aliyeko hospitali au mhandisi anayejenga barabara au daraja ati kwa sababu anatunza fedha? Nani aliyesema mtumishi aliyeko TRA ana umuhimu kuliko mtumishi aliyeko kilimo.
Tunajua hata wabunge Bungeni hupitisha miswada kwa kuangalia masilahi ama ya vikundi ama binafsi. Tatizo linaanzia katika akili za watanzania wote kwa pamoja wala siyo mmoja mmoja.
Kosa la pili ni kutumbua jipu bila hata kufuata kanuni za utumbuaji. Jipu linapaswa kwanza lionyeshe mdomo wake, pili lisubiriwe hadi liive ndipo litumbuliwe. Unapokamua jibu sharti usaha wote utoke pamoja na kiini chake. Ukitumua jipu bila kumalizia kutoa kiini, jipu linarudia tena palepale. Magufuli anachanja juujuu nakutoa amu kidogo huku akiacha kiini cha jipu. You are sorry my dear man hujatumbua jipu bado.
Fuata taratibu za kuwaondoa watu kazini. Usikurupuke wewe ni Rais, una haraka gani?
 
POLE KWA KUTOJUA, UMECHELEWA NDEGE. Ni jambazi la CK nyingi tangu Arusha, Mbeya ,Mwanza na sasa Dar es salaam pengine hilo la Dar ni sababu tu. Yupo kwenye ripoti ya CAG KTK ujenzi wa clinic mwanza na sunset hotel kule LECHELELE MWANZA.
 
Na bado kuna watu wanatatumbuliwa tu na utumbuaji majipu hauhitaj ganzi so mvumilie tu yakiwa yanawauma
Tufanye kazi kwa bidii
Tuache kuabudu pesa
Tufikirie zaid ya tunavyoona
Tujenge Tanzania yenye nguvu umoja na mshikamano
Tupunguze lawama za kila siku tuache kuish kimazoea
 
Naunga mkono hoja
 
Fisadi ni mtu mdaya sana hatumtetei tunachosema sheria zifuatwe unakumbuka yale ya Samaki tulilipa bei gani?
Hii michakato tuliilalamikia sana..kwenye serikali ya awamu ya nne..hahahah mbona kwenye mambo mengine hatutaki sheria zifuatwe.
 
Yaan bado watu mnatetea sheria kwenye ukweli acheni ujinga sheria nyingi ziliundwa kutetea wachache tuzipuuze ndio maana tunadai katiba ndio maana magu anapuuza kutetea wengi tumuunge mkono
tatizo la kila viporo limehasiri sana ubongo wako! hakuna unachofikiri zaidi ya kutapika tu.
 
Pole muhangaikaji tafuta njia mbadala wa kuendesha maisha ambazo ulizoea ndan ya miaka 30 ya utawala wa kidhalimu
 
Ushasema wapinzani kwahiyo sie lazima tutafute lolote lile la kupinga ili tuonekane tupo tofauti,maana hivyo ndio tunaamini tutachukua nchi.
Nchi iliharibika lazima rais afanye hivyo kwani ilioza
 
POLE KWA KUTOJUA, UMECHELEWA NDEGE. Ni jambazi la CK nyingi tangu Arusha, Mbeya ,Mwanza na sasa Dar es salaam pengine hilo la Dar ni sababu tu. Yupo kwenye ripoti ya CAG KTK ujenzi wa clinic mwanza na sunset hotel kule LECHELELE MWANZA.

Hoja yangu umeilewa lakini? Hoja yangu haina uhusiano wowote na ulichoandika hapa. "Jambazi la CK [sic] la siku nyingi" ni nani? Na hilo jambazi au mtu kuwa kwenye ripoti ya CAG kuna uhusiano gani na hoja yangu kuhusu umuhimu wa kuzifanya taasisi kama TAKUKURU kuwa na more autonomy? Vijana wa siku hizi hapa JF hamtaki kabisa kusoma hoja na kuzielewa. Kwa nini?
 
Aidha, ripoti iliyotolewa leo inaonesha kuwa, uchaguzi uliofanyika tarehe 25 Oktoba 2015 ulikuwa huru japo kulikuwa na wasiwasi wa kutokuwa na haki kutokana na madai ya kuibiwa kura.

Hii kali!
Hili hapo chini kulikuwa na uongo?

Polisi wavamia Kituo cha Haki za Binadamu, wabeba ...
www.jamiiforums.com/2015/.../polisi-wavamia-kituo-...
Translate this page
Oct 30, 2015 - Polisi wanaodaiwa kuwa na silaha za moto wamevamia na kuzingira ofisi ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), ... ni uwezekano wa kituo hicho kuwa na matokeo ya uchaguzi ambayo ... Breaking news: Wabunge wa CUF wamejiondoa katika Bunge la Tanzania katika kipindi cha 2015-2020.
 
Acheni ushabiki nyie kwani yeye Kabwe alipokabidhiwa ofisi hayo hakuyaona. Kwanza anashutumiwa tokea alipokuwa Mwanza. Wengi wape sisi wananchi tumeridhika labda nyie na kituo chenu.
 
Mkuu ukitaka kushindwa kufanya kazi, wasikilize watanzania, ukitumbua watasema, usipotumbua watasema!! Ndio maana namkubali Mkapa alipoita baadhi ya watz ambao ndio wengi kwa maoni yangu kuwa ni wapumbavu na malofa
Unamkubali eeh? Ila yule kijana wa Arusha hukubali mawazoyake!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…