Mulhat Mpunga
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 27,263
- 16,288
Mafisadi CCM hayajaisha, yapo na kila anayejaribu kulalamika anachukuliwa hatua.
Kuna mengine yalikimbilia upinzani.
Kuna Jengo la UVCCM kuna vyumba vya watu flani walipewa bure.
Hata Makao Makuu ya CCM kuna maeneo mengi na assets za chama zimeenda mikononi mwa mafisadi.
Sekretarieti: Nina orodha ya mali za CCM ambapo Wizara ya Ardhi wanajua mmiliki wa mali hizo ni CCM na madai tunatakiwa kulipia zaidi ya Bil 1.6; lakini zaidi ya 70% kuna vituo vya mafuta vya watu, kuna maduka ya watu n.k. Ninayo hiyo nyaraka, nitawashikia mahali pazuri.
Kama ni ujumbe, imekuwa SENT and DELIVERED.
Amewataka vijana waache kutumika; wasikubali kutumiwa na yeyote kwani wakati unaweka imani yako kwa huyu, kumbe anayekuja kushinda ni yule...