Jemadari gani anaogopa mapambano. rais mzima unalialia kwamba mniombee. Wewe una majeshi, una bunduki zote, una usalama wa taifa halafu unalialia eti tukuombee.
hajui kazi ya uraisi. Anayejua kazi ya uraisi hutamka maneno haya: UWEZO WA KUMPIGA TUNAO, SABABU YA KUMPIGA TUNAYO, NA NIA YA KUMPIGA TUNAYO, TUNATAKA DUNIA ITUELEWE HIVYO.
Sasa Rais wako badala ya kutamka maneno kama hayo analialia, mniombee. Alah. Je sisi ambao hatuna silaha kama yeye tukipambana na mafisadi au wauza madawa si tulie kabisaaa. yeye ana silaha sisi hatuna silaha.
mwambieni aache uoga anaaibisha. Urais ni ukakamavu. Uombewe usiombewe, uchukiwe usichukiwe wewe unapambana na silaha.
Labda kama alikabidhiwa na wananchi dhaifu, yaani wale waliompa kura.