Rais Magufuli amteua Charles Kichere kuwa Kamishina Mkuu TRA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo March 25 2017 amemteua Charles Edward Kichere kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Kabla ya Uteuzi huo Charles Edward Kichere alikuwa Naibu Kamishna Mkuu wa TRA. Charles Edward Kichere anachukua nafasi ya Alphayo Kidata ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu, Ikulu.

Nafikiri nimepitwa kitu fulani hapa, yule Katibu Mkuu wa Ikulu aliyekuwepo zamani kaenda wapi?? Nakumbuka alikuwa mjamaa fulani kutoka Iringa....
 
Hivyo vyeo vya nchi si elewi kuna Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu na Katibu Mkuu Ikulu tupeni tofauti ya majukumu yao.

Katibu Mkuu Kiongozi ni msimamizi wa Utumishi wa Umma. Kwa hiyo anasimamia sekta ya utumishi wa umma yote nafikiri. Katibu Mkuu wa Ikulu, yeye anashughulika na Ikulu peke yake, kama walivyo Makatibu Wakuu wa Wizara nyingine.
 
CPA siyo tija. Kuna watu wana CPA ni Mabogus kichwani hamna kitu. Kina chotakiwa ni utendaji wa kazi na sifa husika. Amekwambia hana CPA?

Ebu lete CV yake mkuu.
Watu wamecremisha CPA utafikiri nini.....mfano mbona Bashite anapiga kazi na hizo CPA hajui kama ni kiazi mbatata gani?
 
Hapana. Si kila mtu akiwezeshwa anaweza. Kuna wengine hawawezi na hawapaswi kufikiriwa kuwezeshwa. Mfano ni Daudi Bashite. A total failure inside out, left-right and centre.



Elewa makontena hayajapotea. Huo ni wizi umetokea kushirikisha TRA, wafanyabiashara na wanasiasa. Mpaka sasa ni nani kafungwa kwa "kupotea" haya makontena?



Unapoleta mtu kutoka nje unatakiwa ulete mtu competent mwenye uelewa wa kodi na administration. Unapomtoa mtu ambaye hata hajawahi kuwa Director/Mkurugenzi na kumpa ukamishna, tena mtu aliyetoka Tanroads (agency chini ya wizara ya JPM kabla hajawa Rais), hapo kuna harufu ya upendeleo.



Uelewa wako ni mdogo. Haya makusanyo "yanaongezeka" kwa muda mfupi kutokana na hizo sera mbovu za uchumi. Unapoongeza kodi utapata makusanyo makubwa kwa muda mfupi.

Baada ya muda mrefu watu watafunga biashara na Serikali itakosa mapato na watu watakosa kazi. Baadhi ya wafanyabiashara wameanza kufunga biashara.

Hapo hujaongelea faini kutokana na ukwepaji kodi wa miaka ya nyuma.



Ni one man show. TISS na security organs zinapokea orders za mkuu tu. Wakipewa orders waende Clouds hao wanaenda. Wakipewa order wamtolee Nape bastola hao wanatoa. Kweli TISS ipo kazini.



Kazi yake ni ukusanyaji wa kodi. Ukiwa msimamizi yapaswa uwe na uelewa na unachosimamia. Leo hii wewe huwezi kuwa mganga mkuu bila kuwa daktari.



Basic taxation hata wewe unaweza kusoma hiyo haitoshi kuwa Kamishna. Kama kufanya kazi mwaka kunakupa experience ya kuwa kamishna basi waondoe madaraja ya kupanda kutoka chini kufika juu. Ili mtu aingie hapo na CPA yake akae mwaka apewe ukamishna.



Nakubali hakuna mwisho wa kujifunza lakini hupaswi kuwa Kamishna halafu ndo usome Acts zinasemaje. Soma kwanza halafu ndo uwe kamishna.( Unajua CV yake )



TISS wanapaswa kumshauri atengeneze mfumo ambao watu hawawazi kuiba hiyo Tshs 10m in the first place. Kuna watanzania zaidi ya milioni 40. Huwezi kufuatilia kila mtu.

Jenga mfumo ambao watu hawaibi. Lipa watu vizuri. Fanya watu wapende kazi yao. Si kejeli na matusi.

Tuna fikra tofauti sana. Wewe unawaza TISS kukamata watu, mimi nawaza TISS kusaidia kujenga mfumo ambao mtu haibi in the first place.



Mchechu alikuwa CEO wa CBA kabla. Hakuwa head of department. CEO.
 
TRA kwa sasa na kwa kiwango kilichofikia ni kuweka mtu ambaye ni businesse mind... alikuja Dr.Mpango hakukaa.....akaja Kidata naye hakukaa... Hawa Watu sio wafanya biashara in nature.. Na ndio maana wanashindwa kuongeza mapato.... TRA bila Kuwa na Watu ambao biashara iko kwenye damu... Mtafukuza mara kwa mara...
wachagga wameifilisi sana TRA ona sasa mpaka leo aliekuwa mkurugenzi mchaga Hans Kitilya yuko gerezani kwa wizi
 
Mamlaka ya ukusanyaji kodi TRA ni taasisi nyeti sana kwa maendeleo ya taifa.. Nadhani inatakiwa kuwa na uongozi ambao ni stable ili upange na kutekeleza jukumu lake kwa utaratibu na weledi wa hali ya juu.. Hii kubadilisha uongozi wa juu kila mara kwa maoni yangu, hayaleti tija na wala hayampi nafasi alieteuliwa kupanga mikakati yake ya kuhakikisha kodi inakusanywa kwenye mifumo inayoeleweka..

Alfayo Kidata amejifunza mfumo na sasa ni mshauri mkuu wa Rais kama katibu mkuu ikulu. Nafasi ya kamishna mkuu ni ya kisera kwa hiyo hakuna athari kwenye utendaji kwani tra ina wataalamu wa kodi kwenye kila idara. Wanatakiwa tu kutopindisha sheria ya kodi. Kama rais ataendelea kuwapandisha vyeo watumishi walioko halitaharibika jambo na walioko chini watakuwa na kitu kinachoitwa 'job satisfaction' kwani 'succession planning' ni nzuri.
 
Hili ndilo jukumu lake yale mengine awaachie basi hata mawaziri wapate kiki daahh
 
Hongera sana mheshimiwa Rais Magufuli kwa uteuzi mzuri na hakika Kichere ni mtu safi na anaweza.

Bavichaa mmebaki watu wa kupandikiza mbegu za udini katika jamii....kwa kuangalia teuzi anazofanya Mheshimiwa Rais Magufuli. Hakika nawahakikishia watanzania tuko sambamba na Rais wetu na hamtashinda.

Awamu ya nne mlikuwa mnaangalia teuzi kwa miwsni ya kidini kwakuwa Rais alikuwa ni muislamu. Sasa awamu ya tano mmeona mtumie ukabila eti 'ukanda uleule'. Kwa taarifa yenu hata wateule wote wawe wazanaki watanzania tunachohitaji ni maendeleo na sio kitu kingine.

Viva Rais Magufuli na serikali yako kwa ujumla.
Umejenga hoja papo hapo ukabomoa. Kukosolewa hakukwepeki hasa katika nchi yenye watu takribani milioni 45. Mambo ya uteuzi unachanganya na bavicha ni ujuha.
 
Hongera sana mheshimiwa Rais Magufuli kwa uteuzi mzuri na hakika Kichere ni mtu safi na anaweza.

Bavichaa mmebaki watu wa kupandikiza mbegu za udini katika jamii....kwa kuangalia teuzi anazofanya Mheshimiwa Rais Magufuli. Hakika nawahakikishia watanzania tuko sambamba na Rais wetu na hamtashinda.

Awamu ya nne mlikuwa mnaangalia teuzi kwa miwsni ya kidini kwakuwa Rais alikuwa ni muislamu. Sasa awamu ya tano mmeona mtumie ukabila eti 'ukanda uleule'. Kwa taarifa yenu hata wateule wote wawe wazanaki watanzania tunachohitaji ni maendeleo na sio kitu kingine.

Viva Rais Magufuli na serikali yako kwa ujumla.
Hopeless
 
Back
Top Bottom