Mzalendo2015
JF-Expert Member
- Aug 14, 2012
- 6,697
- 9,048
Rais John Joseph Pombe Magufuli ameonekana ni mwungwana, mpole na mwenye moyo wa huruma sana. Tumeona juhudi zake za kutaka DPP na DCI waangalie utaratibu wa kuwasamehe WATUHUMIWA WA UFISADI kama tu wataomba msamaha na kurudisha fedha waliyokwiba au kutakatisha. Hili ni jambo jema.
Hii siyo mara ya kwanza kwa Rais Magufuli kutoa msamha. Alianza na Babu Seya aliekuwa amefungwa kifungo cha maisha kwa kumtoa gerezani. Tatizo linakuja pale inapoonekana hii misamaha imelengwa zaidi kwa kikundi fulani cha aidha wana-CCM au watu waliokuwa ndani ya mfumo wa chama Twawala.
Kuna kesi nyingi sana za Viongozi wa upinzani hasa Wabunge na Wanachama ambao aidha wana kuesi zinazoendelea Mahakamani au wamefungwa gerezani kwasababu tu ni wanachama wa vyama vingine nje ya CCM. Kwa Serikali yoyote yenye kusimamia Utawala bora yenye Rais anayeheshimu Katiba ya nchi haiwezi kuwa na DOUBLE STANDARDS katika kuhudumia raia wake kwa misingi ya itikadi ya vyama, dini au jinsia.
Hivi kesi za Viongozi na Wbunge wa Upinzani nyingi zikiwa za kubambikiwa hasa CHADEMA na CUF zinangoja nini kwa Rais kutoa msamaha na kumwelekeza DPP na DCI kuzifutiliwa mbali Mahakamani? iInasikitisha sana kiongozi wa nchi anapoendesha nchi kwa misingi ya kibaguzi na upendeleo kama ilivokuwa kwa Makaburu wa Afrika ya Kusini.
Hii siyo mara ya kwanza kwa Rais Magufuli kutoa msamha. Alianza na Babu Seya aliekuwa amefungwa kifungo cha maisha kwa kumtoa gerezani. Tatizo linakuja pale inapoonekana hii misamaha imelengwa zaidi kwa kikundi fulani cha aidha wana-CCM au watu waliokuwa ndani ya mfumo wa chama Twawala.
Kuna kesi nyingi sana za Viongozi wa upinzani hasa Wabunge na Wanachama ambao aidha wana kuesi zinazoendelea Mahakamani au wamefungwa gerezani kwasababu tu ni wanachama wa vyama vingine nje ya CCM. Kwa Serikali yoyote yenye kusimamia Utawala bora yenye Rais anayeheshimu Katiba ya nchi haiwezi kuwa na DOUBLE STANDARDS katika kuhudumia raia wake kwa misingi ya itikadi ya vyama, dini au jinsia.
Hivi kesi za Viongozi na Wbunge wa Upinzani nyingi zikiwa za kubambikiwa hasa CHADEMA na CUF zinangoja nini kwa Rais kutoa msamaha na kumwelekeza DPP na DCI kuzifutiliwa mbali Mahakamani? iInasikitisha sana kiongozi wa nchi anapoendesha nchi kwa misingi ya kibaguzi na upendeleo kama ilivokuwa kwa Makaburu wa Afrika ya Kusini.