Rais Magufuli alisomaje chuo kikuu?

Rais Magufuli alisomaje chuo kikuu?

Ukusanyaji wa mikopo utakuwaje rahisi wakati ajira za mliowakopesha mmezikalia?
Kiongozi acha akili za kimagumashi. Ni wangapi ambao wamemaliza CHUO, wafanya biashara wazuri na wengine wameajiriwa ila hawalipi mikopo yao. Pia unasema ajira zimekaliwa unataka kusema miaka yote hiyo ajira zimekaliwa. Kuwa na logic kidogo. Watanzania wengi hatupendi kulipa mikopo shida iko hapo. Wengine wanashughuli za maana tu lakini hawalipi.
 
Fedha za kusomesha wanafunzi chuo kikuu zilikuwa zinatolewa na wafadhili mpaka mwanzoni mwa miaka ya 2000! Wafadhili walipojitoa kutusomesha ndio yakaanza haya mambo ya mikopo...
Kuweka record sawa, mikopo imeanza kutolewa mwaka 1994 ila kwa mfumo wa unapewa kila kitu na wengine hata ada ya chuo hujui ni shilingi ngapi maana wewe ni kusoma tu unachojua ni stationery allowance pamoja na food and accomodation allowance mpaka pale bodi ya mkopo ilipoanzishwa 2004 ndipo huu utaratibu wa sasa ukaanzishwa ambapo pamoja na kwamba unapewa mkopo lakini gharama ya course yako unapewa na unachangia kiasi kadhaa kulingana na asilimia ulizopewa. Na ndio maana wanapotusaka wanufaika wa mikopo husema wale wote ambao wamesoma elimu ya juu kuanzia mwaka 1994 na kuendelea
 
Hakuna shida sisi kulipa mikopo ya elimu, shida ni sera ya kuzuia watumishi wa umma kujiendeleza kimasomo kwa kukata mishahara yao au kusoma pale tu serikali inapoona iinauhitaji wa kuendeleza elimu ya mtumishi na ina budget kwa ajili ya hilo, hii si haki, mbona wao walisoma wakiwa makazini bila mashariti yoyote magumu, kama kukatwa mishahara?????
 
Wakuu

Nimeangalia CV ya Rais nimeona amesema chuo degree ya kwanza mwaka 1985 -1988.

Je, alipataje elimu yake ?
Je, alisomeshwa na nani?
Je, kama alisomeshwa na serikali amelipa pesa ya serikali iliyomsomesha?
Je, kama hakulipa kwanini anawakazia wanafunzi waliokuwa chini ya bodi walipe madeni?
Kama hakulipa maana bodi ilikuwa aijaundwa kwanini hataki wenzake wasome bure?
Kwanini imekuwa ngumu sana kwa mtu aliyepewa elimu bure yeye kuwanyima wenzie elimu?
Basi hata hizo za kurudisha wapeni basi wadogo zetu masikini ziwasadie.

Ukweli mchungu ni kuwa hakuna viongozi wowote waliojilipia ada ya chuo kikuu.
Magufuli
Lowassa
Kikwete
Ndalichako .

Na wengine mulisoma bure udsm na wala hamkudaiwa pesa baada ya masomo yenu.

Nyerere kawapa elimu bure na Mungu anawaona .

Magufuli toa elimu bure mpaka chuo kikuu au jiuzulu.
Hakuna bure siku hizi,peleka stress zako mbele
 
Nafikiri hakuna mtu mnafiki hapa duniani kama mwanasiasa, kwanza ana mipango mingi ambayo yote anakuwa hajui hata namna ya kuitekeleza.

Hakuna mtu anayesahau kile anachakisema kwa muda mfupi kama mwanasiasa. Na ni bahati mbaya sana kuwa kwa nchi za kiafrika hawa wanasiasa wanajua kuwa watu wao nao ni wasahaulifu sana hivyo hawana cha kupoteza hata kama watatoa ahadi elfu mbili.

Mungu tu nafikiri ndiye mkweli hapa duniani naye sasa hatumuoni oooh! sijui sie maskini kimbilio letu litakuwa wapi.

Ole wao wale watakatawala katika enzi ambazo watu wao watakuwa wanajitambua na kujua wajibu na nafasi yao kwa kiongozi waliyemuweka madarakani kwa mikono yao wenyewe na akifika huko anawatisha na kuwanyima kile anachotakiwa kuwafanyia.

Huwezi ukamsaidia mtu kupanda juu na akifanikiwa tu anakugeukia na kukuona wewe si kitu na hata kama usingemsaidia angepanda mwenyewe.

Haya yanatokea Afrika tu.
 
mimi sikupata mkopo lakini kama ningekuwa nimekopeshwa nisingelipa huo mkopo kwanini nilipe niyekopeshwa wakatiwale waliochukua kwa nguvu hela za mboga,vijisenti zile za harusi na nyingine nyingi tu wala hawaulizwi na hili sio uchochezi ila ni halihalisi
 
Wakati yeye anasoma yaani kuanzia waliosoma 1993 kwenda nyuma ilikuwa unasoma bure alafu unatakiwa kufanya kazi serikalini kwa muda wa miaka 5 lakini kwa waliosoma kuanzia 1994 na kuendelea ndio utaratibu wa mikopo ulipoanzishwa na lengo lilikuwa kupata idadi kubwa ya wanafunzi kwa kigezo kwamba wanaporudisha walengwa wa mikopo zinapatikana za kulipia wengine. Kutokana na kutokuwepo utaratibu mzuri wa ukusanyaji madeni ndipo 2004 bodi ya mikopo ilipoanzishwa japokuwa bado changamoto ya ukusanyaji madeni haukuwa mzuri mpaka ilipofika 2009 angalau makusanyo yalianza kukusanywa japo kwa kasi ndogo

Kwahiyo Rais na kundi lake na wazee wetu wote wao sheria hahiwataki kulipa mikopo
Hiyo moral authority haimfanyi ashindwe kusomesha wenzie
 
Zamani wasomaji walikuwa wachache so ilikuwa ni rahisi kuwasomesha. Now wasomaji wamekuwa wengi so inakuwa ni mzigo mkubwa kwa taifa... Hili suala lingekuwa rahisi Zaidi kama ukusanyaji wa mikopo kwa wakopaji waliomaliza lingekuwa effective...
zamani walikuwa wachache kweli pamoja na hilo vitega uchumi vilikuwa vichache pia. Inakuwaje kwa sasa pamoja na migodi, gesi nk vipo ila hata uo mkopo wenyewe unakosekana
 
Fedha za kusomesha wanafunzi chuo kikuu zilikuwa zinatolewa na wafadhili mpaka mwanzoni mwa miaka ya 2000! Wafadhili walipojitoa kutusomesha ndio yakaanza haya mambo ya mikopo...
Sasa hivi wafadhili mnawatukana wana uwezo wa kuzitoa ndio maana tumepoteza 1.6 trions za MCC
 
Zamani wasomaji walikuwa wachache so ilikuwa ni rahisi kuwasomesha. Now wasomaji wamekuwa wengi so inakuwa ni mzigo mkubwa kwa taifa... Hili suala lingekuwa rahisi Zaidi kama ukusanyaji wa mikopo kwa wakopaji waliomaliza lingekuwa effective...
Swali gumu majibu mepesi
 
mimi sikupata mkopo lakini kama ningekuwa nimekopeshwa nisingelipa huo mkopo kwanini nilipe niyekopeshwa wakatiwale waliochukua kwa nguvu hela za mboga,vijisenti zile za harusi na nyingine nyingi tu wala hawaulizwi na hili sio uchochezi ila ni halihalisi
Daaah hii nchi ngumu kweli alafu mtu anakwambia niombee..
 
Mleta uzi, jaribu kutafsiri mambo kulingana na wakati. Enzi hizo hakukua na bodi ya mikopo na chuo kikuu kilikua 1 tu nchi nzima, miaka ya 80 mwishoni mwishoni pale ndio kikaja kingine hicho cha SUA, vingine vyote kama kina IFM, CBE, Nyegezi (sasa SAUT) DSA (sasa TIA), Mzumbe nk vilikua vinatoa Advance diploma and hence serikali ilikua inaweza kuwagharamia hao waliobahatika (angalia nimetumia neon waliobahatika na sio waliofaulu kwasababu maalumu, wazee wenzangu wanajua) kuwasomesha kokote ulimwenguni kwasababu walikua wachache. Sidhani kama UD ilikua inaweza kubeba walau wanafunzi 7000, sidhani. Sasa leo cchuo kimoja kina wanafunzi zaidi ya hao na vipo vyuo zaidi ya 40, do you think serikali inaweza kuwamudu kweli wote hao? Tuweni wakweli. Wakati ukuta.
Tukumbuke pia Enzi za mwalimu Nyerere nchi ilikua ikifuata mfumo wa Kijamaa yaani wa hiki ni chetu sote na ndio maana hata wazazi wetu walikua wanazaa watoto hadi 15, mtoto akiumwa serikali itampa huduma zote za afya, leo ni tofauti. Nchi ni ya "Kibepari" tunafata mfumo wa Hiki ni changu na sio chetu.
 
Hiyo moral authority haimfanyi ashindwe kusomesha wenzie
Tujenge utamaduni wa kuwajenga watoto wetu kwamba jukumu la kumsomesha mtoto ni la mzazi mwenyewe hivyo tutakuwa na kizazi ambacho tayari kimejiandaa kisaikolojia kuliko hivi sasa kila siku tunawaza bure na kila awamu inakuja na mkakati wake yaani maisha yanakuwa mashakani kila siku yaani huyu elimu bure akiingia mwingine lazima tulipe. (kwa mapato gani ya serikali mpaka tusome bure, na huu mkopo sema wengi wameutafsiri vibaya hasa wale ambao hawajaanza kulipa na vichwani siasa ndio kila kitu katika mfumo wa maisha).

Kwa mfano walivyoanza kukusanya walikuwa wanamwomba mwajiri aonyeshe ushirikiano kwa kuwataja wanafunzi waliosoma kipindi cha kuanzia 1994 kisha bodi inaleta deni ofisini kila mtu aliangalie na kukubali kama ni kweli na yupo tayari kisha unaandaliwa utaratibu wa kulipa na wengi walikuwa wanalipa kati ya 30,000 mpaka 50,000 haijalishi unadaiwa shilingi ngapi, uzembe wa serikali kwa miaka iliyopita na wanufaika wenyewe kukimbiakimbia wakidhani watalipishwa laki kadhaa ndio umetufikisha hapa mpaka Bodi ikaweka kiwango cha marejesho kisipungue 8% ya mshahara wa mnufaika
 
Tujenge utamaduni wa kuwajenga watoto wetu kwamba jukumu la kumsomesha mtoto ni la mzazi mwenyewe hivyo tutakuwa na kizazi ambacho tayari kimejiandaa kisaikolojia kuliko hivi sasa kila siku tunawaza bure na kila awamu inakuja na mkakati wake yaani maisha yanakuwa mashakani kila siku yaani huyu elimu bure akiingia mwingine lazima tulipe. (kwa mapato gani ya serikali mpaka tusome bure, na huu mkopo sema wengi wameutafsiri vibaya hasa wale ambao hawajaanza kulipa na vichwani siasa ndio kila kitu katika mfumo wa maisha).

Kwa mfano walivyoanza kukusanya walikuwa wanamwomba mwajiri aonyeshe ushirikiano kwa kuwataja wanafunzi waliosoma kipindi cha kuanzia 1994 kisha bodi inaleta deni ofisini kila mtu aliangalie na kukubali kama ni kweli na yupo tayari kisha unaandaliwa utaratibu wa kulipa na wengi walikuwa wanalipa kati ya 30,000 mpaka 50,000 haijalishi unadaiwa shilingi ngapi, uzembe wa serikali kwa miaka iliyopita na wanufaika wenyewe kukimbiakimbia wakidhani watalipishwa laki kadhaa ndio umetufikisha hapa mpaka Bodi ikaweka kiwango cha marejesho kisipungue 8% ya mshahara wa mnufaika
Unapoongea angalia maisha ya watanzania 80% ni bora mtu umpe elimu iliyo bora hivyo vingine atatfuta mwenyewe...
 
Back
Top Bottom