Tatizo hapa ni kuanzisha utitiri wa vyuo vikuu bila kufanya utafiti na kupima hali ya walipa kodi na watakojiunga uwezo wao. Tuliosoma zamani tulikuwa tunapewa vichere kuanzia certificates mpaka uni. Uchumi ulikuwa mzuri sawa, population ilikuwa low, kiwango cha ufaulu kiliwekwa juu ingawa si kwa mikoa yote mf. Ziwa Magharibi ulipaswa ufaulu mara mbili ya yule wa Dodoma na Singida ndo ufikiriwe kuchaguliwa. shule ilitoa mtoto mmoja au wawili kati ya 45.
Sekondari za serikali zilikuwa ndogo lakini zenye viwango na mwal. Nyerere aliomba walimu toka nchi mbali mbali kama marekani, Scandnavia, ueingereza, india na nchi nyingine kusaidia hivyo vifaa vya kufundishia na walimu haikuwa shida. Tulisoma bure, kula chakula cha 3star hotel na kucheza michezo yote ya hapa duniani na kushindana kimataifa. Tulikuwa tunapata nauli za kwenda nyumbani na kurudi, resurts zilikuwa zinatumwa kwenye posta hivyo huwezi kucheat. Mambo mengi ambayo tukiwaeleza hapa mtachukia hali. Tatizo Population imeongezeka, elimu imeshuka, utitiri vwa vyuo bila viwango, kila mtu kuona kwenda uni ndo kusoma, vyuo vya ufundi kudharauliwa, vyuo vya maendeleo na maarifa ya nyumbani kuwa dormant.
Kila mtu anataka kwenda Uni badala ya kuangalia vyuo ambavyo vinatoa ujuzi wa moja kwa moja kama Veta kunachangia kuleta shida. Uchumi umeshuka mazao tuliyotegemea kama kahawa na katani zimekufa sasa mnategemea nini. Bring back our country.