Rais Magufuli ajiandikisha kwenye daftari la mpiga kura kitongoji cha Sokoine. Asema amehamia Ikulu ya Chamwino, Dodoma

ESCORT 1

JF-Expert Member
Dec 7, 2015
1,267
2,519
Rais Magufuli amejitokeza katika kitongoji cha Sokoine jijini Dodoma kwa ajili ya kujiandikisha kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Baada ya kujiandikisha, amewaambia wakazi wa eneo hilo kuwa kwa sasa yeye ni mwenzao na ameshahamia rasmi kwenye Ikulu ya Chamwino. Hivyo yeye ni mwenzao.

Amewaambia wananchi kuwa amehamia Ikulu ya Chamwino ingawa bado haijakamilika rasmi.


Chanzo: Chanel Ten
 
Rais Magufuli na mke wake mama Janeth leo wamejiandikisha katika uchaguzi wa serikali za mitaa pale mtaani kwake Chamwino katika kitongoji cha Sokoine mjini Dodoma.

Rais Magufuli ambaye amefika mtaani kwake akitokea ziarani Mpanda imemlazimu kupanga foleni baada ya kuwakuta jirani zake wakiwa katika mstari wakiendelea kujiandikisha.

Bado siku 2 hima hima watanzania tukajiandikishe

Source Channel ten tv
Maendeleo hayana vyama!
 
Niko nae tayari kashasaini ila yule muhudumu alikuwa anajishtukia sana hadi kalamu kidogo ashindwe kuishika
 
Na ww lini utahamia huko

Ova
 
Afadhali f Afadhali foleni Dar na misafara ya viongozi zipungue!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…