Rais Magufuli acha kumdhalilisha Kikwete

Rais Magufuli acha kumdhalilisha Kikwete

Naona mrija umekatika!una bahati mbaya mana umekatika mapema sana!pole!isijekuwa mmoja wa walioamrishwa kusalimisha hati za kusafiria!
 
Wanachama hamko satisfied!!!? Okay! Teh! Endeleeni kuisoma namba. Bila sheria mbovu ya viti maalumu, naamini nyie wanachama wengi mngelala njaa awamu hii!!!

Ngoja nikukumbushe kauli hizi za mheshimiwa rais, ili ujue chama sio kipaumbele kwake:
1. Chagua Magufuli kwa mabadiliko ya ukweli.
2. M4C ndugu zangu ni,"Magufuli for Change."
3. Nipeni kura wana Cuf, Chadema, Nccr, Udp niwatumikie.
4. Nipeni mimi kuzungusha mikono ya maendeleo, ninaweza kuzungusha hata mara 50.
5. Nimteue waziri wa maji halafu asilete maji, yeye ndiye atageuka maji.
6. Mafisadi watafute nchi ya kwenda (Tunajua mafisadi wana kadi ya chama).
7. Uchaguzi umeisha, rais ni JPJM Hapa kazi tu. Nk...
 
Mleta mada ni mwana-CCM Mzuri sana, na alikuwa anampigia debe Mh. Magufuli. Kutokana na maelezo yake ni kwamba, hafurahii utendaji kazi wa mheshimiwa Rais, na kwa maana hiyo inaonekana hawa ni miongoni mwa waliokuwa wamebweteka na kudekezwa na uongozi uliopita. Inaonekana wazi kabisa, kutokana na utendaji wa Mhe. Huyu mleta mada ana wasiwasi kuathiriwa kwa maslahi yake. Hivyo inaonekana wazi kabisa Mh. Rais ana vita kali sana kutoka ndani ya CCM yenyewe kutokana na kugusa maslahi ya vigogo. Hapa kazi ipo, Mungu mlinde Mhe. Rais maana ana vita kali sana.
 
Magufuli akiendelea hivi,basi CCM inatapata asilimia 99 mwaka 2020,JK aliingia kwa asilimia 89 kaondoka kwa asilimia hamsini na kitu,JK kwa kweli upole ulimzidi mafisadi wamemharibia sana credibility yake.Baba Magu Rudisha heshima ya CCM kwa kuwatendea kazi watanzania waifurahie nchi yao

kwenye kasi hiii inabidi Mwanasheria mkuu awe makini watu wasijeenda mahakamani wakaigaragaza serikali tukazidi kupata hasara.
 
Mleta mada ni mwana-CCM Mzuri sana, na alikuwa anampigia debe Mh. Magufuli. Kutokana na maelezo yake ni kwamba, hafurahii utendaji kazi wa mheshimiwa Rais, na kwa maana hiyo inaonekana hawa ni miongoni mwa waliokuwa wamebweteka na kudekezwa na uongozi uliopita. Inaonekana wazi kabisa, kutokana na utendaji wa Mhe. Huyu mleta mada ana wasiwasi kuathiriwa kwa maslahi yake. Hivyo inaonekana wazi kabisa Mh. Rais ana vita kali sana kutoka ndani ya CCM yenyewe kutokana na kugusa maslahi ya vigogo. Hapa kazi ipo, Mungu mlinde Mhe. Rais maana ana vita kali sana.


Uko sawa kabisa lkn pia mie huyu mleta maada hakufikiria kabla ya kuongea.... Kwa kifupi mleta maada ni MPUUMBAAVUUU KABISA.
 
JK......Tulishamsahau siku nyingi mara ya mwisho nimemsikia eti kaibukia Ethiopia kuwapa neno Taifa star....Jipu lako nadhani limetumbuliwa mie sikuwah dhani km Muhimbili kuna wagonjwa wanalala chini aisee kumbe JK alikua anajipigisha vijipicha maeneo mazuri tu....Wewe utakua mswahili maana dhana ya kuomba omba kwako ni sawa uku mabilioni uku nchini yakitafunwa kwa kasi ya escaping velocity..
#WhatWouldMagufuliDo#
 
Mimi sitamuunga mkono Magufuli mpaka atakapotamka kuendeleza mchakato wa katiba mpya hasa kurudisha rasimu y Warioba. Haya mengine anayofanya ni just 'Cosmetic changes" na huwa hazidumu. Tusimsifie, kwanza ni mapema mno kusifia, siku 20 tu? mpeni mwaka kama hajachoka.
 
Tatizo mnapenda kutoa sifa za mtu hata pale anapobolonga nani asiejua safari nyingi za nje zilikua mzigo kwa Taifa? sio Maguguli tu hata Benard Membe amekili hazalani kua walikua wakipishana Angani kama vile huku Nyumbani kunawaka Moto! Je huyu nae? Je Ile kauli ya Prof Baregu, Mbatina Mketo juu ya safari za Raisi na Gharama zake? Kikwete karigarimu Taifa hilo liko wazi tusing'ate maneno.
 
Sina lengo baya Bali kama mtanzania nimeguswa na one man show anayofanya mh dk magufuli.
ushahidi.

Kutembelea muhimbili na kuzungumzia mambo mazito.

"" Juzi rais Magufuli alifanya ziara ya kushtukiza Muhimbili na kumwondoa mkurugenzi na bodi ingawa bodi ilishamaliza muda wake na mkurugenzi kahamishiwa wizarani tu wala hajafukuzwa.

Ikulu ikadai Magufuli alikasirishwa sana kukuta mashine za MRI hazifanyikazi ndio maana kaisimanisha bodi,Lakini jana kupitia Azam Tv Katibu mkuu wizara ya Afya Bw.Mbando alisema mashine haikutengenezwa kwa sababu Magufuli alisema bali ilikuwa tu kwamba akivyotenbekea pale mchakato wa kuikarabati mashine ulishakamilika.

Alisema tatizo lililokuwepo ni kwamba Phillips wanaidai serikali zaidi ya bil 7 ndio maana waligoma kuitengeneza hiyo nashine.

Sasa mchakato wa kupunguza deni ndio ulikuwa unaendelea na zilishapatikana bil3 kutoka hazina walizolipwa juzi hao Phillips ndipo wakakubali kuja kuifanyia mashine ukarabati.

Na hili linaleta maana zaidi kwa sababu wizara haiwezi kutoa bil3 ghafla tu bila kuwa zilikuwa kwenye mchakato.

Kwa hiyo hapa ikulu ilifanya usanii wa hali ya juu kuwaaminisha watanzania kwamba kulikuwa na uzembe pale muhimbili wakati uzembe ulikuwa serikalini. Serikali ilishindwa kulipa deni kwa wakati.

Na inasemeka hili jambo halikumfurahisha Kikwete kwa sababu lilipeleka picha kwamba serkali yake ilikuwa goigoi.

Wakati yeye anasema amefanya juhudi kubwa kuiboresha Muhimbili. Na kwamba tatizo km la juzi linajulikana kwamba ni ukata na ufinyu wa bajeti ndio kikwazo.
.Safari za nje zimeiletea serikali fedha ambazo zimetumika kujenga barabara, kuboresha miundombinu ya umeme,ujenz wa bandari mpya, ujenzi wa chuo kikuu cha tiba na mambo mengi sana kwa juhudi za kikwete.
" kuna watu wamesafiri nje kuliko safari za kwenda kumsalimia mama yake" kauli hii ya magufuli haivumiliki na kauli iliojaa jeuri.

Kila kilichofanywa na kikwete kuonekana ni tatizo kwa mh magufuli.

Kikwete aliunda baraza kubwa la mawaziri ili kurahisisha kuwahudumia wananchi kuliko kuwa na wizara chache kwa watu. million 50
sasa magufuli kudai kunawizara nyingi atazifuta naona lengo ni kuonyesha kuwa utawala wa kikwete ulikuwa dhaifu .

Conclusion.
Haina haja kudhalilisha uongozi uliopita ili uonekane u nafanya kazi. rais kama unapitia hapa JF kuna wanachama hawako satisfied kwa namna unavoenenda.

asante.

Dah. Mimi binafsi nimesikitika sana kusoma post yako mkuu. Nafikiri unacho andika hapa ni vitu ambavyo haviendani na utendaji wa kazi wa mtu mwenye kupenda mabadiliko. Kazi ya Ikulu sio kutoa fedha za kutengeneza vifaa vya hospitali wala bara bara. Hizo ni kazi za wizara na ndio maana kuna budget zinazo pelekwa bungeni kujadiliwa. Sasa kama wizara imefanya madudu na kutumia fedha pasipo na kuweka mikakati matokeo yake inafikia hapa. Si hitaji kuandika na kuelezea kila kitu kwani naamini wewe ni Great thinker. Kikwete kashapita kama walivyo pita wengine. Magufuli hawezi kufanya kazi kwa kufuata misingi ya Kikwete. Tusitake kufanya mambo yakawa magumu. Watanzania tumezoea kulalamika na kulia lia kama watoto. Mtu akiwa mtendaji mzuri, mna lalamika, mtu akiwa mbovu kama Kikwete mna lala mika. Naombeni tufanye kazi. Tu msupport Magufuli kwani Mabadiliko ndani ya nchi hii ni mimi na wewe.
 
Wee umetoka Msoga au wee mkwere pia...!! Mkwere hadi abaki uchi... Magu hamwachi...!!

Safari za nje sio za Rais tu.... WATUMISHI WA NGAZI ZA JUU SERIKALINI walikuwa wanasafiri nje kama KWENDA CHOONI VILE tena choo cha bar, mnapishana tu...!!!

Trillions of tshs lost ktk hizi safari za nje... Chukua Rais, Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu, Manaibu Katibu, Makamishna, Ma CEOs, DGs... MDs... wa mamlaka, Wakala, Taasisi, Vyuo, Mashirika ya umma, Hospitals, viongozi wa juu wote hao WALIKUWA WANASAFIRI kama wanaenda choo cha bar...!!!

Sasa ndio MWISHOOOOOOO...!!!

Ukija seminars, mikutano, warsha, sherehe za Kitaifa na makampuni, wizara yaani Serikali nzima ilikuwa ni WIZI NA KUTUMBUA FEDHA trillions...

Sasa zimefungwaaaaaaa.....!!!

Safiiiiiiiiiiiii... hiii lazima tumpongeze Rais Magufuli....!!
 
sina lengo baya Bali kama mtanzania nimeguswa na one man show anayofanya mh dk magufuli.
ushahidi.

kutembelea muhimbili na kuzungumzia mambo mazito.

"" Juzi rais Magufuli alifanya ziara ya kushtukiza Muhimbili na kumwondoa mkurugenzi na bodi ingawa bodi ilishamaliza muda wake na mkurugenz kahamishiwa wizarani tu wala hajafukuzwa.

Ikulu ikadai Magufuli alikasirishwa sana kukuta mashine za MRI hazifanyikazi ndio maana kaisimanisha bodi,
Lakini jana kupitia Azam Tv Katibu mkuu wizara ya Afya Bw.Mbando alisema mashine haikutengenezwa kwa sababu Magufuli alisema bali ilikuwa tu kwamba akivyotenbekea pale mchakato wa kuikarabati mashine ulishakamilika.

Alisema tatizo lililokuwepo ni kwamba Phillips wanaidai serikali zaidi ya bil 7 ndio maana waligoma kuitengeneza hiyo nashine.

Sasa mchakato wa kupunguza deni ndio ulikuwa unaendelea na zilishapatikana bil3 kutoka hazina walizolipwa juzi hao Phillips ndipo wakakubali kuja kuifanyia mashine ukarabati.

Na hili linaleta maana zaidi kwa sababu wizara haiwezi kutoa bil3 ghafla tu bila kuwa zilikuwa kwenye mchakato.

Kwa hiyo hapa ikulu ilifanya usanii wa hali ya juu kuwaaminisha watanzania kwamba kulikuwa na uzembe pale muhimbili wakati uzembe ulikuwa serikalini. Serikali ilishindwa kulipa deni kwa wakati.

Na inasemeka hili jambo halikumfurahisha Kikwete kwa sababu lilipeleka picha kwamba serkali yake ilikuwa goigoi.

Wakati yeye anasema amefanya juhudi kubwa kuiboresha Muhimbili. Na kwamba tatizo km la juzi linajulikana kwamba ni ukata na ufinyu wa bajeti ndio kikwazo.
.
.safari za nje zimeiletea serikali fedha ambazo zimetumika kujenga barabara, kuboresha miundombinu ya umeme,ujenz wa bandari mpya, ujenzi wa chuo kikuu cha tiba na mambo mengi sana kwa juhudi za kikwete.
" kuna watu wamesafiri nje kuliko safari za kwenda kumsalimia mama yake" kauli hii ya magufuli haivumiliki na kauli iliojaa jeuri.

.kila kilichofanywa na kikwete kuonekana ni tatizo kwa mh magufuli.

kikwete aliunda baraza kubwa la mawaziri ili kurahisisha kuwahudumia wananchi kuliko kuwa na wizara chache kwa watu. million 50
sasa magufuli kudai kunawizara nyingi atazifuta naona lengo ni kuonyesha kuwa utawala wa kikwete ulikuwa dhaifu .

conclusion.
Haina haja kudhalilisha uongozi uliopita ili uonekane u nafanya kazi. rais kama unapitia hapa JF kuna wanachama hawako satisfied kwa namna unavoenenda.
asante.

Wewe umeshiba tu kande huo ubavu wa kumchagulia raisi wa nchi jinsi ya kuongoza na kuendesha serikali yake umeupata wapi?Haya ndio mambo alioahidi katika kampeni zake na unaemtetea alikuwa akimsikia na anamwelewa vyema uthubutu wake na uwezo wa kuongoza. Anayoyafanya Magufuli ndio njia sahihi za kurekebisha uchumi wetu na uelewe waswahili husema kila zama na kitabu chake.Kwanini hujiulizi madini yote yanayochimbwa,misitu na mali asili,utalii,bandari,mapato ya kodi za ndani n.k. hazina yetu ni ya kuachwa tupu bila hata senti huku deni la taifa halishikiki? Kontena 349 zimegunduliwa kuchukuliwa bandari yetu ya Dar na mapato ya zaidi ya billion 80 hazikulipwa. Jee kwa miaka mitano bandari moja hiyo hiyo imepoteza mapato ya kiasi gani kwa serikali na bado wizara na idara nyingine? Je kumfunga jela Mramba na Yona na kuwaacha mafisadi wa hela nyingi zaidi na wauza madawa ya kulevya hawa wapo juu ya sheria? Tunachotarajia kwa Magufuli mara baada ya kutangaza baraza la mawaziri ni kuturudishia AZIMIO LETU LA ARUSHA, kuunda timu ndogo ya wataalam wa kuandika katiba mpya (isiwahusishe wabunge) bali wataalam na muongozo wao uwe mapendekezo na matakwa ya wananchi waliyoyakabidhi kwa Warioba.Jambo jingine muhimu ni raisi Magufuli kama raisi wa muungano amwalike raisi wa Zanzibar na Maalim Seiff wakae pamoja na kutekeleza haki kama ilivyo. Kujidanganya kurudia uchaguzi visiwani ni kujidanganya na kukaribisha vurugu kubwa visiwani itakayomfanya Magufuli ashindwe hata kuongoza nchi badala yake aanze kushughulikia vurugu. Msijidanganye na washawasha nyingi mlizonunua wananchi wamefikia hatua nyingine na hawatatishika.
 
Duh!!huyu assady ndie alikua akisema UKAWA wataisoma namba sasa anashangaa kuona kabadilishiwa mtihani badala ya Civics kapewa kitu cha intergration,,pole sana ndugu utazoea tu kuishi katika misingi ya haki.
 
sio muda wa kucompare nani yukoje na nani hakufanya nini,cha msingi ni kufanya kwa uaminifu na uadilifu na ndivyo mheshimiwa rais anachofanya,Rais akilegeza buti ndo mnakuwa wa kwanza kumuita legelege,akikaza buti pia mnaugua,hakuna kati kwa kati,mzee wa kisukuma keshaamua kukaza buti-PISHA NJIA.
 
Back
Top Bottom