Rais Kikwete sio kigeugeu!

Rais Kikwete sio kigeugeu!

Ukimya ni Silaha nzuri sana bwana Salva..! wakati mwingine mnatakiwa mnyamaze tu.Kadiri mnavyojaribu kuongea mnazidi kuharibu..HAKUNA UJUMBE HAPO...narudia..HAKUNA UJUMBE HAPO..!
 
hii barua hata mtoto wa kindergarten hawezi kuandika upuuzi wa namna hii!!!kwani watanzania tunataka maelezo ya sentesi yako hii ifuatayo si vinginevyo,
Katika mjadalahuo, baadhi ya wabunge walihoji uhalali wa Wizara kuomba michango yafedha kutoka kwenye Taasisi zilizoko chini ya usimamizi wake ilikusaidia Bajeti ya Wizara hiyo kupita kwa urahisi.
Kujitetea kuwa uamuzi wa rais ulitoka kabla ya shinikizo la bunge si kweli!!Zitto aliuwasha moto siku abayo Jairo karudi kazini kesho yake Pinda ndipo akalitaarifu bunge kwa nini Luhanjo asitoke na maazimio mapya rais?hapa ni kuwa Utoh alishaambiwa amsafishe Jairo na Luhanjo atangaze,JK hakuamini reaction ya bunge iliyotekea ndipo ikabidi abadilishe mawazo

 
I don't get any significant picture on this Juha's cinema
 
aa SERIKALI NI DHAIFU,LEGELEGE,KIGEUGEU NA MDEBWEDO. SALVA THE DAYS ARE NUMBERED.
 
Tunapendakusisitiza kuwa Mheshimiwa Rais hawaja kigeugeu kwa sababu alifanyauamuzi mmoja tu baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Katibu MkuuKiongozi.
Kwanini ikulu inajihisi? nina wasiwasi......... watuambieni nani aliwaambia rais ni kigeugeu hadi waanze kujitetea au rais kahisi wimbo wa Jaguar kaimbiwa yeye
Wanasiasa vigeugeu
 

Tunapendakusisitiza kuwa Mheshimiwa Rais hawaja kigeugeu kwa sababu alifanyauamuzi mmoja tu baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Katibu MkuuKiongozi. Na uamuzi huo aliufanya kabla ya Bunge kulizungumzia sualahilo na hivyo uamuzi huo wa Rais haukutokana na shinikizo la Bunge.Pamoja na kumweleza Katibu Mkuu Kiongozi, Rais pia alimfahamishaWaziri Mkuu kuhusu uamuzi wake huo asubuhi hiyo ya tarehe 25, 2011.
[/QUOTE]

Nonesense
 
Mi naona bado wanazidi kujichanganya na kujidhalilisha mbele ya umma....Bungeni Pinda alitamka kuwa laiti angekuwa na mamlaka angechukua uamuzi wa kumwadhibu Jairo mara moja,na aliahidi atamfahamisha rais kwani ndiye mwenye mamlaka.Sasa ikiwa Rais amefanya uamuzi mmoja tu kusitisha agizo la Luhanjo kwa Jairo kurejea kazini ,je ni nani aliyemwagiza Luhanjo kumpa likizo Jairo na kumtaka CAG kufanya uchunguzi?Je ni hatua/uamuzi gani aliyochukua Rais baada ya kujulishwa jambo hili na Pinda?Kama hakuwahi kuchukua hatua zozote awali,ni kipi kimemsukuma sasa?

Yaani hii barua na hii film ya Jairo haviendani kabisa. Hii barua inaonyesha hii nchi haina kiongozi kabisa, ni madharau matupu. Kwa hii picha Mh Pinda jiuzulu tu hutendewi haki. Na ndio maana vitu vingi wanakudanganya unaumbuka kama mtoto mdogo. Kikwete ni kigeugeu anajua Pinda ndie anawajibika kumuwakilisha bungeni kwa mambo ya serikali iweje ampe Luhanjo kazi ya kumsafisha Jairo kwa waandishi wa habari wakati mkiki yote imeanzia bungeni. Kwa hii film ya Jairo unatudhihirishia maneno ya watu wanaposema watendaji wako wanakudharau kumbe na wewe unawadharau vilevile na ndio maana unapewa ripoti feki na za uongo. Mh Pinda watakuharibia sifa yako kwa umma ni afadhali uwaachie ubaki na ubunge wako.
 
They could have done this before coming to the public. What it shows is that, in President's office, people don't talk or coordinate activities as one team. Root cause of that is the weakness in leadership!
 
Wewe ambae si legelege mbona huna hata ujumbe wa nyumba kumi? unanchekesha.
<br />
<br />
mmh........... Faiza ebu post thread zenye maana acha majungu au na wewe unatumia mananiiiih kufikiria...
 
Nilishasema Salva anachafua sana heshima ya Ikulu sijui huwa anaandika hayo matamko akiwa amelewa,anajidharilisha mwenyewe na MH.Dr Jakaya Mrisho KIkwete ,kama amenyamaza kipindi chote hiki taifa limeingia kwenye mtafaruku mkubwa mafuta,sukari,bajeti kuongezewa pesa kutoka maeneo yasiojulikana wizi wa Jairo ,leo hii ndio aje na uongo wake kama alivyozoea kuongopea watu yaani hapo IKulu hawajui kusema ukweli,Raisi mwongo,na watendaji wake wote waongo,hatundanganyiki,Raisi ni kigeugeu na hana staha kwa wananchi wake anatudharau sana anatuchukulia kama hatuwezi kupambanua mambo,pole Salve ngojeni siku zenu ziishe tuachie hiyo nyumba
 
bravo kikwete wanakupakazia wewe sio kigeugeu
 
Mambo ya Tanzania yanatisha kidogo. Watu wanapenda sana udairekta, kwa hiyo Salva ni direkta wa presidential communications na hivyo anaongoza DIRECTORATE of Presidential communications. Huo ni ujinga mtupu; iiyo ni ofisi ya mawasiliano ya ikulu, siyo Kurugenzi kwa sababu taasisis ya Ikulu haikugawanywa katika kurugenzi, na wala haitakiwi igawanywe katika kurugenzi, kwani inasaidiwa na Wizara kadhaa. Kwa mfano Ofisi ya Makamu wa Rais, na mawaziri wa Nchi Ofisi ya rais, pamoja na mawaziri wa nchi ofisi ya Makamu wa Rais.

Ila ili kuwakweza watu ndipo tukatunga kuwa DIRECTORATE of presidential communications. Je mnaweza kutuambia chini ya Directorate hiyo kuna vitengo vingapi?
 
Sina uhakika kama Mh Raisi amesoma barua hii kabla ya kwenda hewani... hainiingilii akilini kuwa imeandikwa na Ikulu, maana ina mapungufu mengi sana ni aibu kwa kweli hata ujumbe uliokusudiwa umekaa vibaya sana naasikitika

yaani, kama hadi ikulu inatumia domain ya yahoo basi kazi kweli kweli
 
Sina uhakika kama Mh Raisi amesoma barua hii kabla ya kwenda hewani... hainiingilii akilini kuwa imeandikwa na Ikulu, maana ina mapungufu mengi sana ni aibu kwa kweli hata ujumbe uliokusudiwa umekaa vibaya sana naasikitika

kabla sijafikia maudhui nilistaajabu kukutana na jina la taasisi na anuani (UNITEDREPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATEOF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS


[TABLE="class: cms_table"]
[TR]
[TD="width: 239"] Telephone:
[/TD]
[TD="width: 104"]
[/TD]
[TD="width: 252"] PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
zikiwa kwa lugha ya kiingereza wakati ujumbe umewekwa kwa lugha ya kiswahili

kama sio kukurupuka ni jitihada za fasta fasta kuwaondoa watz mashaka ya maamuzi ya ikulu
 
Salva, unatumia taaluma yako vibaya kwa kutoa taarifa potofu. Hivi nani mkubwa kimadaraka kati ya Waziri Mkuu na Katibu Mkuu Kiongozi? Tunakumbuka maneno aliyosema Waziri Mkuu ni nini angefanya kama angekuwa na mamlaka ya kutoa maamuzi juu ya kashfa ya Jairo, mwenye mamlaka hayo (si Katibu Mkuu Kiongozi) alikuwa nje ya nchi wakati huo aliahidi kumpigia simu baadae. Na simu ilipopigwa tukaambiwa kuna maelekezo (kutoka kwa rais) mengine kuhusu Jairo - ndo KMKiongozi akaibuka na maelekezo ya Cag kufanya uchunguzi.
Kakangu Salva huo mchezo wa kuigiza wa kitoto unaofanywa na hao unaowakurugenzia habari kwani ripoti imemtakasa Jairo kwamba hakutoa mlungula. Hivi hizo pesa zilitoka ktk bajeti ipi? Hizo pesa ni nyingi kutolewa kama hongo huku wanchi wakitaabika sana.
Nasikia Jairo siku aliporipti kazini alipokelewa kama shujaa hadi gari lake kusukumwa, mwambie rais jambo hilo lilituudhi sana.
Rais huyo huyo kaamuru Jairo arudi likizo kupisha uchunguzi wa tume ya bunge! KAMA SI UKIGEUGEU NI NINI?
Itafika siku hata kuhutubia watakuwa wanakuja watoto tu.

Yaani hizi sarakasi zA ****** pamja na serikali yake legevu\kigeugeu zinanipa shida kujua ilikuwaje huyu jamaa akafikiri kuwa anaweza kuwa raisi wa nchi.Mambo anayoyafanya ni kama vile hafikirii kabisa,hebu soma hiyo taarifa ya kurugenzi ya mawasiliano ya ikulu,hata mhitimu wa kidato cha nne kutoka shule za kata anaweza kukutolea mapungufu mengi tu!****** please tuachie Tz yetu!
 
<br />
<font color="#ff0000"><span style="font-family: Palatino Linotype"><font size="3">Tunapendakusisitiza kuwa Mheshimiwa Rais hawaja kigeugeu kwa sababu alifanyauamuzi mmoja tu baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Katibu MkuuKiongozi. Na uamuzi huo aliufanya kabla ya Bunge kulizungumzia sualahilo na hivyo uamuzi huo wa Rais haukutokana na shinikizo la Bunge.Pamoja na kumweleza Katibu Mkuu Kiongozi, Rais pia alimfahamishaWaziri Mkuu kuhusu uamuzi wake huo asubuhi hiyo ya tarehe 25, 2011.</font></span></font><br />
<br />
<br />
Nonesense[/QUOTE]<br />
<br />upupu kabisa mkuu hadi kichefuchefu!
 
What a shame, barua inatoka mamlaka ya juu hivyo na ina typos kibao? Hata Salva naamini hakuisoma, naamini hata Secretary aliye i type hakuisoma, alipomaliza tu ikatolewa kwa waandishi.
Yani hata hilo ni gumu kufanya?
Kheeeee!
 
Back
Top Bottom