JK si tu JEMBE, bali ni JEMBE NA SULULU au SHOKA kama ukipenda. Kwa maana nyingine ile alama iliyoko kwenye bendera ya CCM ndio JK. Ukitaka kumjua zaidi JK muulize MO Ibrahim, kwani yeye ndio kamaliza.
Ndugu MJENGA, mada kama hizi CHADEMA hawawezi kujibu kwa hoja, angalia ukurasa wa 3 hakuna aliyejibu hoja. Tafsiri fupi ya hali hii ni kuwa hila na vitimbi vyao vimeshindwa, kwani wao wangependa kuiona nchi haitawaliki na Tanzania inaingia katika VITA. Dua zao zote zimeshindikana, na kibaya zaidi watanzania wamekielewa CHADEMA kama chama chenye nia mbaya na WATANZANIA. Na hii imejionyesha wazi katika matokeo ya UDIWANI kama ulivyoainisha katika mada yako.
Tatizo la CHADEMA ni kushindwa kukubali hata katika yale mazuri ambayo yanaonekana wazi kwa wananchi yaliyofanywa na serikali. Kitendo hiki ndicho kitachoiua CHADEMA, kwa sababu watanzania ni watu wenye akili sana na kuelewa ni nini kinawezekana na nini ni Propaganda.
Katika mafanikio yote umeyasema, lakini kubwa lililowafunga mdomo wapinzani ni la kufanikisha UCHAGUZI MKUU WA CHAMA KATIKA NGAZI KUU MBALI MBALI MJINI DODOMA hivi karibuni. Wengi walifikiri ngumi zitapigwa na chama kitachanika vipande vidogo vidogo kama chembe za mtama. Hilo halikutokea, na ni kwa juhudi na umakini mkubwa wa Mwenyekiti, JK. Safu ilivyojipanga inaitisha CHADEMA na iaashiria mwisho wa mbio zao kuelekea IKULU. Kama kuna CHAMA kinachofahamu umahiri wa JK, basi ni CHADEMA.
Naweza kubet kuwa JK atapata zawadi ya MO Ibrahim mwaka 2016/2017, kwa ufanisi wake mzuri wa kujenga Demokrasia Tanzania ikiwa pamoja na uhuru wa kusema, kuunda urafiki na vyama vyote nchini, kukuza elimu na kuijenga Tanzania yenye matumaini.
Ukitaka kujua mafanikio ya Tanzania katika demokrasia, tathmini hali ya demokrasia katka nchi jirani kama Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda, Ethiopia na Kongo. Ukipata jibu rudi mtandaoni.
JK ni historia kwa Tanzania.