Rais Kikwete kuhamishiwa Hoteli Maalum

Rais Kikwete kuhamishiwa Hoteli Maalum

Jk ni president, hata km sikubaliani na uongozi wake natambua anahitaji uangalizi mzuri na linalomfika Rais athari yake sio km linalonifika mimi. Linaweza hata kugusa utulivu wa nchi.
Km imelazimika kupata matibabu maalum know Rais wa nchi siwezi kusema eti nae aende Muhimbili.
Muhimu ni ushauri wa Daktari.
Hadhi ya clerk, Director, Minister etc haiwezi kulingana, Tujenge personality na zetu competence ili tupate privilege. Huo Ndio uhalisia mengine ni politichi.
 
Waungwana,

Katika hizi picha zote za Kikwete akiwa hospitali USA sijaona hata picha moja inayomuonyesha mkewe Salma Kikwete, ni aje Wakuu? Hasa ukitilia maanani mara nyingi wanaambatana na Kikwete kwenye safari zake.
 
Hivi toka aingie ikulu miajka 8 iliyopita hajawai umwa? Kama ndivyo kwa nini kurugenzi ilikuwa haisemi? Malengo yao nini kwa sasa......?
 
Duh ila watu wanapiga maisha hiyo team aliyoenda nayo posho yao ya siku ni sh. ngapi ?
Mtu ukitoka huko ka sio kujenga kibanda basi ki vitz au ki rav 4 unacho au kiwanja
Acheni watu wamwage pesa kwenda ikulu maake pana faida kubwa sana kuliko biashara yeyote tena isio na stress zozote
Nafikiri siku 20 walizosema zitatumika tena ikibidi zitapungua hata siku 2 ili kuokoa pesa za wavuja jaso
Rais kikwete ni mtu wa watu, mpenda amani na Maendeleo.
Mungu mponye Rais wetu polepole kwa hakika ili asije pona ya haraka baada ya wiki moja akarudi huko kwa mwezi mzima.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ambaye anaendelea na matitabu yake nchini Marekani, leo, Jumatano, Novemba 12, 2014, anatarajiwa kutoka wodini katika Hospitali ya Johns Hopkins na kuhamishiwa kwenye Hoteli Maalum ambako ataendelea kuwa chini ya uangalizi wa madaktari.

Rais Kikwete amekuwa kwenye Hospitali ya Johns Hopkins tokea Jumamosi iliyopita wakati alipofanyikwa upasuaji wa tezi dume
(prostrate) na afya yake imekuwa inaimarika kiasi cha kuanza mazoezi ya kutembea.

Kutokana na kuondolewa kwa bandeji kwenye mshono ambao
nao umeanza kukauka vizuri, Rais Kikwete baadaye leo atahamishwa kutoka wodini kwenda kwenye Hospitali Maalum yenye uhusiano na Hospitali ya Johns Hopkins iliyoko karibu na hospitali hiyo.

Akiwa kwenye Hoteli Maalum hiyo, Rais Kikwete ataendelea kupatiwa matibabu, kutembelewa mara kwa mara na madaktari na kuwa chini ya uangalizi wa wauguzi muda wote. Wiki moja baadaye, Rais Kikwete atafanyiwa tathmini ya kuwawezesha madaktari kuamua hatua inayofuata ya matibabu yake.

Wakati huo huo, kwa sababu ya wingi wa ujumbe mfupi wa simu (sms) ambazo amekuwa anazipokea Rais Kikwete, imeanzishwa namba maalum ya simu ambako wananchi wanaweza kuwasiliana kwa sms na Mhe. Rais. Namba hiyo ni +1-646-309-2295.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
12 Novemba, 2014
Hapo kwenye red, ndipo pana walakini! Uangalizi wa mara kwa mara wa madaktari ambapo yupo chini ya uangalizi wa wauguzi muda wote maana yake rais yupo ICU, period!

N.B: Kwa sheria za Marekani uangalizi wa wauguzi muda wote unafanyika ICU au Hospace Care Unit na siyo mahali pengine
!
 
Waungwana,

Katika hizi picha zote za Kikwete akiwa hospitali USA sijaona hata picha moja inayomuonyesha mkewe Salma Kikwete, ni aje Wakuu? Hasa ukitilia maanani mara nyingi wanaambatana na Kikwete kwenye safari zake.
Mh. Rais ana uchungu na pesa za walipa kodi huyo angeongeza bajeti kuwa kubwa. Si unajua mambo ya mama zetu mara shopping pale mara akamsalimie fulani hapo pesa za wavuja jasho zinatumika
 
Kuna watu wapuuzi sana...huyo ni binadamu anaumwa bt siasa ndo inakufanya kufurahia Afya ya mwenzio kutokua kawaida?...
 
lingekuwa jambo jema watanzania kutenga siku maalumu ya ibada kitaifa kumwombea rais wetu.
 
Marekani Watamfaidi Sana Kiuchumi..Wanaweza Wakamshikilia Hospitalini/Hotelini Kuongeza Mapato Ya😵le Wanatanzania !
 
Hivi huyu jamaa alimkaimisha nani wakati anaondokA?

Swali nzito, ukiwekwa chini kwa ajili ya upasuaji huwezi kuwa 100% sure ya kuwa utaamka. Angekuwa open na amwache vice president in charge
 
Miaka 50 ya uhuru, lini hospitali zetu zitaweza kufanya kaoperation kama hiki?
 
Kwa hiyo huyu Profesa anataka sympathy ya wananchi baada ya kukwapua mabilioni ya pesa za walipa kodi? Huyu mtu kwa kweli tulichagua HASARA! Safari hii watanzania tumepatikana. Bill ya safari na matibabu yake wala hakuna atakayethubutu kuisema, labda ichakachuliwe!

Kauli sii sahihi. Kwa kauli kama hizi unakosa hata BARAKA za Mungu maana Kikwete ni mpakwa mteule wake. Swala kutibiwa nje ni la kawaida na watanzania wengi wamekua wanatibiwa. Kuhusu wizi hebu tungoje ripoti zisomwe tuone wahusika na hatua zitakazo chukuliwa.
 
umeongea neno!maana watu wanabwabwaja tu na lawama nyingi.kwa hadhi na status yake anastahili kwenda popote kutibiwa.nyie mnaopinga rais kutibiwa marekan kama kwel ni wa zalendo huwa mnaenda kutibiwa hospital za kwenye kata zenu?jibu ni hapana.kila mtu huwa anatafuta pale anapoona patastahili kupata huduma kutokana na hadhi yake.tuache siasa wakat mwingine tuongee ukweli.
 
Back
Top Bottom