Baba Joseph17
JF-Expert Member
- Jul 15, 2013
- 9,518
- 9,806
"Nilipata bahati ya kufanya kazi Zanzibar. Kuna wakati Mzee Thabit Kombo aliniambia wakati ukifika jambo unalolitaka litakuwa hata watu wapinge na kama wakati bado hata ufanyeje halitakuwa. Mimi niligombea 1995, wakati ulikuwa bado halikuwa lakini 2005 wakati ulikuwa sahihi likawa. Kwa hiyo nawewe January lisipokuwa safari hii usiweke nongwa ila amini wakati bado"
Rais Kikwete - Soni Bumburi
9 July 2014
Source: Mkuu wa wilaya korogwe (Mh. Mrisho Gambo - Facebook page)
Kuna mzee alinitonya eti mwaka 1985 Thabiti Kombo ndiye aliyemkwamisha Salim Ahmed Salim pale JK Nyerere alipokuwa anataka awe mrithi wake wakati katiba ilikuwa haimruhusu Salim kutokana na umri Nyerere alizuga kumteua Mwinyi ili wakifika kwenye kikao mbele ya wajimbe jina lake likitajwa Mwinyi akatae ili dhamira ya Mwalim itimie. Thabiti Kombo akamfuata Mwinyi akamwambia isiwe mjinga wewe ukitajwa ukubali mzee ruksa jina lake lilipotajwa naye akakubali uteuzi we Nyerere hakuamini jinsi alivyoliwa chenga.