Rais Kikwete karuhusu kampeni Urais CCM?

Rais Kikwete karuhusu kampeni Urais CCM?

OgwaluMapesa

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2008
Posts
10,942
Reaction score
437
Akiwa Lushoto leo Rais Jakaya Kikwete amemuasa january makamba awe na subira katika kugombea Urais na asipopata nafasi ,akubali tu matokeo "Nilipata bahati ya kufanya kazi Zanzibar. Kuna wakati Mzee Thabit Kombo aliniambia wakati ukifika jambo unalolitaka litakuwa hata watu wapinge na kama wakati bado hata ufanyeje halitakuwa. Mimi niligombea 1995, wakati ulikuwa bado halikuwa lakini 2005 wakati ulikuwa sahihi likawa. Kwa hiyo nawewe January lisipokuwa safari hii usiweke nongwa ila amini wakati bado".

Kitendo ch Rais kikwete kumpa wasaa January Makamba kimewashangaza viongozi wa chama na serikali waliokuwepo kwenye ziara ya mhe Rais kikwete inakuwaje aongoze kikao cha kupiga marufuku wagombea kuanza kampeni then aje Bumbuli atamke maneno mazito kama haya ikiwa na wiki mmoja tangu january atangaze nia ya kugombea Urais au kifungo cha mwaka mmoja walichofungiwa wagombea Urais kilimlenga mtu? alisikika akihoji mmoja .wa viongozi wa ccm mkoa.
 
Kosa la jk likowapi mkuu mbona jk katoa ushauri mzuri sana wewe ulitaka asemaje sasa.
 
"Nilipata bahati ya kufanya kazi Zanzibar. Kuna wakati Mzee Thabit Kombo aliniambia wakati ukifika jambo unalolitaka litakuwa hata watu wapinge na kama wakati bado hata ufanyeje halitakuwa. Mimi niligombea 1995, wakati ulikuwa bado halikuwa lakini 2005 wakati ulikuwa sahihi likawa. Kwa hiyo nawewe January lisipokuwa safari hii usiweke nongwa ila amini wakati bado"
Rais Kikwete - Soni Bumburi
9 July 2014
Source: Mkuu wa wilaya korogwe (Mh. Mrisho Gambo - Facebook page)
 
JK hakupaswa kusema hayo! kama dogo alitangaza nia ni kampeni na pia kusimama na kusema ameanza kampeni ni kampeni pia. CCM bila Lowasa 2015 hakuna ushindi.
 
Edo kanyamaza anajipanga, alianza membe, sasa kaja makamba jr, sasa akiibuka mwenyewe utasikia wanavyohangaika kumtuliza.
 
Wewe ulitaka aseme nini sasa hebu tuambie wewe unataka aseme nini.
 
Edo kanyamaza anajipanga, alianza membe, sasa kaja makamba jr, sasa akiibuka mwenyewe utasikia wanavyohangaika kumtuliza.
Usimsemee edo fanyeni yenu jamani kwanini kutwa kujadili watu kwenye haya maisha wakati ukifika atavuka mto alisema edo.
 
Dhaifu ni dhaifu tu atazunguka zunguka weeeee mwisho anakwepa wajibu wake, Hivi Mangura bado yuko in charge hapo Lumumba?

BACK TANGANYIKA
 
Kwani sasa hivi JK anaweza kucontroll nini?? Kila kitu kimemshinda
 
"Nilipata bahati ya kufanya kazi Zanzibar. Kuna
wakati Mzee Thabit Kombo aliniambia wakati
ukifika jambo unalolitaka litakuwa hata watu
wapinge na kama wakati bado hata ufanyeje
halitakuwa. Mimi niligombea 1995, wakati
ulikuwa bado halikuwa lakini 2005 wakati
ulikuwa sahihi likawa. Kwa hiyo nawewe
January lisipokuwa safari hii usiweke nongwa
ila amini wakati bado"
Rais Kikwete - Soni Bumburi
9 July 2014
 
Ushauri huu kwanini asiwape akina Membe, Sitta, Ngeleja, Wassira, Sumaye? kwani hawajui kuwa wanamsindikiza Lowassa?...
 
JK hakupaswa kusema hayo! kama dogo alitangaza nia ni kampeni na pia kusimama na kusema ameanza kampeni ni kampeni pia. CCM bila Lowasa 2015 hakuna ushindi.
tuwe wakweli hiyo afya ya Lowasa ataiweza mikikimikiki ya uchaguzi kama cyo Kutaka kumumalizia tu mzee wa watu?
 
Back
Top Bottom