Mwana Mpotevu
Platinum Member
- Sep 7, 2011
- 3,295
- 2,506
Rais Kikwete amemteua Dr Grace Pujah na Bw Innocent Seba kuwa wabunge wapya katika bunge la Muungano kuanzia tar 20 Machi.
Kufuatia uteuzi huo, sasa JK amemaliza orodha wa wabunge wote kumi wa kuteuliwa kwa mujibu wa mamlaka aliyopewa na Katiba.
===========
Kufuatia uteuzi huo, sasa JK amemaliza orodha wa wabunge wote kumi wa kuteuliwa kwa mujibu wa mamlaka aliyopewa na Katiba.
===========
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARIRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, amewateua wabunge wawili (2) wapya wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Walioteuliwa ni Dkt. Grace Khwaya Puja na Bwana Innocent Sebba.
Rais amefanya uteuzi huu kwa mamlaka aliyopewa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 66 (I) (e) ambapo amepewa mamlaka ya kuteua wabunge wasiozidi 10.
Uteuzi huu umekamilisha idadi ya wabunge ambao Mheshimiwa Rais amepewa kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo Kikatiba.
Wabunge ambao wameshateuliwa ni:
- Mhe. Profesa Makame Mnyaa Mbarawa
- Mhe. Profesa Sospeter Mwijarubi Muhongo
- Mhe. Dkt. Asha Rose Migiro
- Mhe. Janet Zebedayo Mbene
- Mhe. Saada Salum Mkuya
- Mhe. Zakhia Hamdani Meghji
- Mhe. Shamsi Vuai Nahodha
- Mhe. James Fransis Mbatia
Uteuzi huu umeanza tarehe 20 Machi, 2015.
Imetolewa na:
Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais, Msaidizi
Ikulu-Dar-Es-Salaam