Unapotoa credit kwa kitu fulani ni lazima unafanya ulinganishi(comparison) ya hiyo kitu na kitu kingine chenye uhusiano au ufanano.
Unapompa sifa Rais kikwete kuwa ameongoza vizuri, ila tu kwa sababu moja tu, amani na utulivu inakubidi ulinganishe na awamu zilizopita, binafsi natilia shaka hizi sifa kama ni sifa za dhati toka moyoni au ziko corrupted.
Je, rais ametimiza ahadi alizoahidi kwa kiwango gani?, Je, wewe unadhani aliingia madarakani kwa ajili ya kuleta utulivu na amani tu?
Tangu nchi yetu ipate uhuru, ni kipindi cha JK pekee ambacho tumeshuhudia ukosefu wa amani na utulivu kama vile mauaji ya albino, kutekwa na kuumizwa kwa watu maarufu, mapigano ya kidini yaliyosababisha mauaji sanjari na kupigwa risasi na kuuawa kwa viongozi wa dini. Haya mambo yametokea katika kipindi hiki cha JK na katika tawala zilizotangulia hatukuwahi kuyashuhudia.
Leo wewe unasimama hadharani tena mchana kweupe na kusifu kuwa ameongoza kwa amani na utulivu, huoni aibu?
Sasa ulitaka asemeje rafiki? Ila binafsi nakushukuru kwa kumtambua kwamba yeye ni Rais,kwani kufanya hivyo ni uthibitisho tosha sifa anazopewa anastahili na ndizo anazo.
Hivi usipomsifu kiongozi wako wa nchi yako, utamsifu kiongozi wa nchi gani?.Na kama utamsifia kiongozi wa nchi fulani,je ulikwisha wahi
kuishi huko? Na kama ulikwisha wahi ishi huko,ni kitu gani kilikuleta nchini Tanzania?
Ndugu yangu,jenga utamaduni wa kusifia cha nyumbani na kama kuna mapungufu ni bora ukatoa mapendekezo/maelekezo yenye tija
kuliko kuwakatisha tamaa wenzako,mbaya zaidi kuwaona wenzako ni majuha ila wewe ni bora mwenye upeo mkubwa wa kufikiri.
Mwisho,ni vema ukaelewa kuwa vyote hivyo unavyomtuhumu Mh.Rais eti vimetokea kwa sababu yake vingeweza kutokea kwa kiongozi
yoyote yule kwani masuala ya udini,usalama wa waandishi wa habari,mauaji ya ablino na utesaji yamejitokeza karibu nchi nyingi sana
duniani.Natumaini wewe ni mwelevu sana ebu fanya utafiti katika baadhi ya nchi zikiwemo nchi jirani utagundua kwamba hapa Tanzania
kuna uhuru mkubwa sana,sema tu kuna baadhi ya watu,makundi fulani yanatumika kuchafua uhuru wetu kwa maslahi yao na makundi
yao.