Rais Kikwete anastahili sifa

Rais Kikwete anastahili sifa

LUMBAKALA

Senior Member
Joined
Dec 29, 2010
Posts
148
Reaction score
20
Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete anastahili sifa,mimi kama Mtanzania nampa pongezi rais Kikwete kwa kuongoza nchi katika hali ya amani na utulivu.

Kuna waliosema mheshimiwa rais hatoboi 2015 yaani angekuwa amengatuka mapema,baada ya kumtuhumu kuwa mambo mengi ameyafumbia macho.

Unajua nchi haiongozwi kwa jinsi tunavyotaka sisi.Kiukweli nchi ilifika mahali iliyumba ila mwanaume wa shoka rais kikwete alituliza akili zake akafumua uongozi mambo yakaenda shwari.

Wapo waliomuombea mabaya ila rais hakuwajali sana alijitahidi mpaka hapa tulipofika.

Imebakia miaka 2 tu akamilishe safari ngumu na nzito,basi mimi nimeona nimtakie kazi njema na yenye mafanikio,kiukweli anastahili sifa.
 
Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete anastahili sifa,mimi kama Mtanzania nampa pongezi rais Kikwete kwa kuongoza nchi katika hali ya amani na utulivu.Kuna waliosema mheshimiwa rais hatoboi 2015 yaani angekuwa amengatuka mapema,baada ya kumtuhumu kuwa mambo mengi ameyafumbia macho.Unajua nchi haiongozwi kwa jinsi tunavyotaka sisi.Kiukweli nchi ilifika mahali iliyumba ila mwanaume wa shoka rais kikwete alituliza akili zake akafumua uongozi mambo yakaenda shwari.Wapo waliomuombea mabaya ila raisi hakuwajali sana alijitahidi mpaka hapa tulipofika.Imebakia miaka 2 tu akamilishe safari ngumu na nzito,basi mimi nimeona nimtakie kazi njema na yenye mafanikio.Kiukweli anastahili sifa.
mungu mkubwa wote waliokuja na silogani ya nchi haitatawalika. Sasa wanaona aibu kila kona wanayopita, sasa wamebaki kulalama na katiba mpya, katiba ambayo wenyewe waliichekelea pale ikukummheshimiwa alipowapa nafasi ya kuwasikiliza.
 
LUMBAKALA, hope nawe ni GAMBA pumba gani unatuletea shenzi type!
 
Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete anastahili sifa,mimi kama Mtanzania nampa pongezi rais Kikwete kwa kuongoza nchi katika hali ya amani na utulivu.Kuna waliosema mheshimiwa rais hatoboi 2015 yaani angekuwa amengatuka mapema,baada ya kumtuhumu kuwa mambo mengi ameyafumbia macho.Unajua nchi haiongozwi kwa jinsi tunavyotaka sisi.Kiukweli nchi ilifika mahali iliyumba ila mwanaume wa shoka rais kikwete alituliza akili zake akafumua uongozi mambo yakaenda shwari.Wapo waliomuombea mabaya ila raisi hakuwajali sana alijitahidi mpaka hapa tulipofika.Imebakia miaka 2 tu akamilishe safari ngumu na nzito,basi mimi nimeona nimtakie kazi njema na yenye mafanikio.Kiukweli anastahili sifa.

Lakini...NI RAIS wa NCHI ana WASHAURI katika NYANJA MBALIMBALI

1. Kwanini Hajui Tanzania ni MASKINI pamoja na kuwa na MADINI; GAS; UTALII Duniani???

2. Kwanini Hajui UDINI Umeanzaje wakati wa UTAWALA wake??

3. Kwanini Familia yake Imekimbilia Madaraka NDANI ya CCM-NEC

4. Kwanini hajawatangaza Wauza MADAWA ya KULEVYA pamoja na kuwa na MAJINA yao??

5. Kwanini anapendelea kusafiri safiri kwenda NJE ya NCHI wakati hajaona UMUHIMU wa kwenda MTWARA kuongea na Wananchi wa huko kuhusu ISSUE ya GAS ???

6. Kwanini kulimbikiza UTAJIRI BAGAMOYO? Kwani BAGAMOYO kuna UTAJIRI GANI? Bandari ni ya KUCHIMBA; Bandari ya MTWARA it is naturally DEEP...


Sasa huyu ndie MGOMBEA wa URAIS ambaye 2010 alianza na matamshi ya UDINI na UKABILA ili achaguliwe

Alipochaguliwa kuwa RAIS hakuwa na HEKIMA ya kuweza kuyaongelea matukio hayo ila aliyaacha yazidi kuwasugua Wananchi...

Kwasababu ya UCHUMI MBOVU ndipo UAMSHO na SHEIK PONDA wakajitokeza sio kuwa ni WADINI PerSe... ni Sababu ya Watu wengi wa DINI yao hawana KAZI; na hii imesababishwa na UZEMBE wa CCM kuuza VIWANDA vya SERIKALI BILA kuangalia MBELE nani ataajiri waliopunguzwa na wanaomaliza SHULE as unskilled and semi-skilled labors...

*** KWAHIYO FANYA RESEARCH kabla ya mapongezi!!!
 
Anastahili sifa lakini si hiyo uliyo sema. Hata kinana anastahili sifa. Sifa ni sifa tu mbaya au nzuri
 
Mnampenda sana nyiee?

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Kila la kheri Jakaya Mrisho Kikwete
Mungu awabariki waliokaribu nawe na unaowaongoza
 
Kati ya marais Tanzania...ameharib Taifa, ushahid wa Lema ndio utakuelewesha
 
Mungu akuzidishie Maarifa na umri mkubwa Rais kipenzi cha Watanzania
 
Jk ni janga la kitaifa hakika sitamsahau na nitasimulia vizazi vyangu.
 
Kikwete tutakukumbuka sana kwa maendeleo ulio tuletea na uhuru wa kila kitu. JK hakunaga!!!.
 
Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete anastahili sifa,mimi kama Mtanzania nampa pongezi rais Kikwete kwa kuongoza nchi katika hali ya amani na utulivu.

Kuna waliosema mheshimiwa rais hatoboi 2015 yaani angekuwa amengatuka mapema,baada ya kumtuhumu kuwa mambo mengi ameyafumbia macho.

Unajua nchi haiongozwi kwa jinsi tunavyotaka sisi.Kiukweli nchi ilifika mahali iliyumba ila mwanaume wa shoka rais kikwete alituliza akili zake akafumua uongozi mambo yakaenda shwari.

Wapo waliomuombea mabaya ila rais hakuwajali sana alijitahidi mpaka hapa tulipofika.

Imebakia miaka 2 tu akamilishe safari ngumu na nzito,basi mimi nimeona nimtakie kazi njema na yenye mafanikio,kiukweli anastahili sifa.

Mh, Ndg yangu yaelekea wewe ni mgeni na unaonesha udumavu ki uelewa katik siasa za nchi hii,Hivi hujui yeye Kikwete pamoja na rundo la washauri wake hakuwahi kuiona nchi ilivyokuwa ikiteteleka mpaka tu pale "THE REGEND" Mh Zitto alipotaka sahini za wabunge zinazohitajika kikatiba ili kumg'oa Waziri Mkuu ndipo,Rais kuepusha aibu akaamua kufumua na kuusuka upya uongozi wake??So sifa hizo umezielekeza kusipo mahala pake Mpe sifa hizo Zitto Kabwe (MB).

By the-way,hivi Mh, Rais wakati akiingia madarakani moja ya sera zake ilikuwa kuwapa Watanzania maisha yaliyo bora,hivi mpaka hapo" katakwimu" kanasemaje kuhusu maisha bora aliyoyaahidi kwa kila Mtanania ili tuanzie hapo!
 
JK ameifanya nafasi ya urais inadharaulika sana enzi hizi.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
The problem ni watanzania wenyewe kuwa wajinga, na woga right ingekuwa nchi nyingine JK angekuwa amesha poteza muda mrefu. Pili alichakachua matokeo hivyo hivyo angekubali kidemokrasia leo asingekuwa rais, muda wake ungeishia phase moja. Na tatu sasa anaongoza kwa mkono wa chuma hii ni dalili ya kuwa amefail. Na mwisho ameamua kutawala kwa kuwagawanya watanzania kwa msingi wa dini ndo wapo wanaomuunga mkono kama wewe na wa dini tofauti wanampinga divide and rule
 
Yaani ukisoma posts za watu wengine hadi unasikia kichefuchefu. Lakini inawezekana ulipewa kaukuu wa wilaya kwa hiyo ni lazima umsifie.
Tokea uhuru wa nchi hii JK ndiye Rais mbovu kuliko wote waliowahi kutawala nchi hii. Sababu za kusema hivi zipo wazi kwani maisha ya watanzania walio wengi yamezidi kuwa magumu isipokua kwa wachache kama alieanzisha Uzi huu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom