Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi Rais Jakaya Kikwete amewataka wajumbe wapya wa NEC wa CCM kutokulala bali kuzunguka kila kona ya nchi kufanya mikutano ya hadhara,kuingiza wanachama wapya na kueneza sera za chama hicho.
Rais Kikwete amesema kazi hiyo ikamilike kabla ya uchaguzi wa serikali za mitaa 2014 kisha iendelee mpaka uchaguzi mkuu wa 2015.Rais Kikwete amesema hiyo ndiyo njia pekee itakayokipa ushindi mkubwa chama hicho kwenye chaguzi zijazo.Rais amesema kamwe chama kisichozunguka kwa wananchi kuhutubia na kueneza sera lazima kitaangamia.
Itakumbukwa ni hivi karibuni Msajili wa vyama vya siasa nchini John Tendwa alitishia kupiga marufuku chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA kuendelea na operesheni yake ya M4C kwa kile alichodai amesitisha operesheni zote mpaka nyakati za uchaguzi.Alisema akiwa kama msajili wa vyama kamwe hatakubaliana na operesheni za CDM za kujijenga.
Naye Mhadhiri wa chuo kikuu cha DSM Dr Benson Banna alimuunga mkono Tendwa kwa kusema Operesheni ya CDM ya M4C haikubaliki kwani ni kuwasumbua wananchi na kuwanyima muda wa kufanya kazi na kuwataka CDM wasubiri kipindi cha uchaguzi.
Kama vile ni mpango mahususi ulikuwa umepangwa nayo Kamati ya kuchunguza kifo cha Daudi Mwangosi maarufu kama kamati ya Nchimbi iliungana na Tendwa katika moja ya mapendekezo yake kuitaka serikali kupitisha sheria ya kuzuia mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa mpaka nyakati za uchaguzi.Pendekezo hilo lilisema shughuli zote za siasa baada ya chaguzi zihamie bungeni.
Kauli ya Rais Kikwete ya leo imeonekana waziwazi ni kupingana na kauli ya msajili wa vyama vya siasa John Tendwa na Msajili huyo ameonekana wazi hafai kuendelea kushikilia wadhifa huo.
Source: ITV/Chanel Ten.
Rais Kikwete amesema kazi hiyo ikamilike kabla ya uchaguzi wa serikali za mitaa 2014 kisha iendelee mpaka uchaguzi mkuu wa 2015.Rais Kikwete amesema hiyo ndiyo njia pekee itakayokipa ushindi mkubwa chama hicho kwenye chaguzi zijazo.Rais amesema kamwe chama kisichozunguka kwa wananchi kuhutubia na kueneza sera lazima kitaangamia.
Itakumbukwa ni hivi karibuni Msajili wa vyama vya siasa nchini John Tendwa alitishia kupiga marufuku chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA kuendelea na operesheni yake ya M4C kwa kile alichodai amesitisha operesheni zote mpaka nyakati za uchaguzi.Alisema akiwa kama msajili wa vyama kamwe hatakubaliana na operesheni za CDM za kujijenga.
Naye Mhadhiri wa chuo kikuu cha DSM Dr Benson Banna alimuunga mkono Tendwa kwa kusema Operesheni ya CDM ya M4C haikubaliki kwani ni kuwasumbua wananchi na kuwanyima muda wa kufanya kazi na kuwataka CDM wasubiri kipindi cha uchaguzi.
Kama vile ni mpango mahususi ulikuwa umepangwa nayo Kamati ya kuchunguza kifo cha Daudi Mwangosi maarufu kama kamati ya Nchimbi iliungana na Tendwa katika moja ya mapendekezo yake kuitaka serikali kupitisha sheria ya kuzuia mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa mpaka nyakati za uchaguzi.Pendekezo hilo lilisema shughuli zote za siasa baada ya chaguzi zihamie bungeni.
Kauli ya Rais Kikwete ya leo imeonekana waziwazi ni kupingana na kauli ya msajili wa vyama vya siasa John Tendwa na Msajili huyo ameonekana wazi hafai kuendelea kushikilia wadhifa huo.
Source: ITV/Chanel Ten.